CHADEMA yakana vikumbo vya urais

CHADEMA yakana vikumbo vya urais

Ni nadra saaana mtuhumiwa mbele ya mahakama kukiri kosa hata kama anajua kwa dhati kabisa kuwa ametenda kosa hilo.
Hili tamko linanirejesha kwenye ukweli huo.
 
Rejao said:

Maumivu ya kichwa huanza taratibuuu!! CDM, mnaongelea urais kitu ambacho kwenu ni ndoto!!! Labda jaribuni kuanzisha cheo cha rais wa CDM, instead of mwenyekiti! Urais wa JMT hamuuwezi!!!
ritz said:
Chadema wanaota ndoto za mchana aisee! labda Rais kivuli.

Farajianeni nyie kwa nyie!
 
Wakuu mnaona mataahira wanavyojibizana wenyewe kwa wenyewe? Avatar zao zinajieleza,oh masikini marehemu CCM uchomwe vizuri huko kuzimu.
 
Welldone kitengo cha habari mmeanza vizuri toka uptoshaji wa Sengerema na leo huu mmeukanusha on the spot, BIG UP.
Sasa si wakati wa kuhangaika na majina ni wakati wa kuhangaika na utendaji jina litakuja automatically.
 
Maumivu ya kichwa huanza taratibuuu!! CDM, mnaongelea urais kitu ambacho kwenu ni ndoto!!! Labda jaribuni kuanzisha cheo cha rais wa CDM, instead of mwenyekiti! Urais wa JMT hamuuwezi!
Mkuu Rejao,
Chadema wanaota ndoto za mchana aisee! labda Rais kivuli.!!

Limewapata hilo;kajipangeni vizuri mje na uzushi mwingine enyi CCM!!!
 
Chama cha magamba ndio kuna watu wanapigana vikumbo kwa ajili ya urais kwa kujigeuza wahubiri kwenye makanisa, wamesafiri hadi nigeria kujisafisha ingawa kwa wenye akili zetu timamu tunaona wanatwanga maji kwenye kinu.watanzania wa sasa si wa kipindi kile.
 
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Monday, 09 January 2012 21:13

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]

Shakila Nyerere

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kwa sasa hakiwezi kuanza mbio za kusaka urais. Badala yake, kinatumia muda huu kujikita kutatua matatizo ya jamii yanayozidi kuongezeka.

Pia, Chadema kinasema kumewapo na taarifa zinazosambazwa kwa umma kupitia njia mbalimbali za upashanaji habari, zikiwa na nia ya kuonyesha kuwa kuna mbio za kuwania urais ndani ya chama.

Taarifa ya chama hicho iliyotolewa jana, inasema kuna baadhi ya watu wanapewa nafasi kubwa kugombea nafasi hiyo, kiasi kwamba sasa ndani ya Chadema ni mvutano wa kuwania urais.

"Chama kinapenda kutoa taarifa sahihi kwa wanachama, wapenzi, washabiki wake na Watanzania wote kwa ujumla, juu ya suala hili ambalo linaweza kuiweka Chadema katika mizania moja na vyama vingine," inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Kinasema kimekuwa kikifanishwa na viongozi wa vyama vingine ambao wamekuwa wakilifanya suala la kugombea urais kuwa linaongozwa na kuamriwa kwa utashi binafsi wa mtu, uchu na tamaa ya cheo.

Miongoni mwa mambo ambayo yanazungumziwa kwenye taarifa hiyo, ni kwamba Serikali imekuwa ikiishia kushughulika na dalili au matokeo yanayojitokeza, hivyo kukosa majibu ya kudumu na kuishia kutoa lawama kwa wakosoaji wake.

Taarifa hiyo inasema katika chama chao, kinachopewa umuhimu ni utumishi kwa umma kwa ajili ya maendeleo ya watu siyo mbio za kusaka vyeo.

"Ni vyema hii dhana ya mtu kufuatwa na kuombwa, mara anapoonekana kuwa anafaa kuongoza, kulingana na mahitaji ya watu na sifa za nafasi hiyo, kama ambavyo imekuwa ikifanyika ndani ya Chadema, ikaenziwa na kufanywa kuwa ni namna bora ya kupata viongozi," inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Inasema hivi sasa ndani ya Chadema hakuna cha ‘kupamba moto' kwa ajili ya kuwania urais, wala hakiwezi kuwapo.

Chadema imesema suala muhimu ni namna ya kutafuta mizizi au vyanzo vya matatizo mbalimbali yanayokabili jamii pana ya Watanzania, kisha kutafuta majibu au suluhisho ya kudumu, kwa kushirikiana na Watanzania wote wenye nia njema na nchi yao.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Kwahiyo Yakana vikumbo vya Zitto, Mbowe na Katibu Mkuu... ni mapema Mno vizuri
 
Mkuu Rejao,
Chadema wanaota ndoto za mchana aisee! labda Rais kivuli.
. Eti Mkuu Rejao! Yaani kitu umeandika mwenyewe na unajipongeza mwenyewe baada ya kugundua uko peke yako!hahaaaaa Ritz si ndo Rejao!
 
Back
Top Bottom