OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 228
Ndiyo Wakuu, Heshima kwenu!
Hatimaye ile kauli ya Mjinga akijitambua mwelevu yupo matatani ime endelea kujidhihirisha jana baada ya cdm kuigalagaza vibaya ccm katika uchaguzi wa serikali za vijiji na vitongoji wilayani Magu .
Kwa mujibu wa matokeo ni kuwa vijiji vilivyo kuwa vinagombaniwa jumla yake ni 5 ambapo CHADEMA imeshinda vijiji 3 vya Kahangara, Kabila na Ihayabuyaga.
CCM imeambulia kijiji 1 cha Langi na UDP nacho pia kime ambulia kijiji 1.
Katika upande wa vitongoji, jumla kulikuwa na vitongoji 37 ambapo vitongoji 17 CCM imepita bila kupingwa kwasababu ya jiografia na maandalizi. Hivyo kwenye vitongoji 20 vilivyo gombaniwa cdm imepata vitongoji 14 na ccm imeambulia vitongoji 6.
Vilevile ndani ya vitongoji 14 vilivyochukuliwa na CHADEMA kuna kitongoji cha Bugando kijiji cha Lemeji kata ya Sukuma anakotoka Mbunge Dkt Festus Limbu.
Pia kuna kitongoji cha Mtaa wa bank -NMB Magu mjini kilichopo kwenye makao makuu ya CCM Magu mjini kimebebwa na CHADEMA kwa kura nyingi.
Mwl Nyerere ktk Kitabu cha "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" -1973 alipata kusema
"WATU WANAWEZA WAKACHOKA NA KUSEMA POTELEA MBALI WAKACHAGUA CHAMA CHOCHOTE ILI MRADI TU WAONDOKANE NA KANSA YA UONGOZI WA CCM. HAINIFURAHISHI KUYASEMA HAYA ,LAKINI UHAI WA NCHI YETU UNATAKA YASEMWE ."
Hatimaye ile kauli ya Mjinga akijitambua mwelevu yupo matatani ime endelea kujidhihirisha jana baada ya cdm kuigalagaza vibaya ccm katika uchaguzi wa serikali za vijiji na vitongoji wilayani Magu .
Kwa mujibu wa matokeo ni kuwa vijiji vilivyo kuwa vinagombaniwa jumla yake ni 5 ambapo CHADEMA imeshinda vijiji 3 vya Kahangara, Kabila na Ihayabuyaga.
CCM imeambulia kijiji 1 cha Langi na UDP nacho pia kime ambulia kijiji 1.
Katika upande wa vitongoji, jumla kulikuwa na vitongoji 37 ambapo vitongoji 17 CCM imepita bila kupingwa kwasababu ya jiografia na maandalizi. Hivyo kwenye vitongoji 20 vilivyo gombaniwa cdm imepata vitongoji 14 na ccm imeambulia vitongoji 6.
Vilevile ndani ya vitongoji 14 vilivyochukuliwa na CHADEMA kuna kitongoji cha Bugando kijiji cha Lemeji kata ya Sukuma anakotoka Mbunge Dkt Festus Limbu.
Pia kuna kitongoji cha Mtaa wa bank -NMB Magu mjini kilichopo kwenye makao makuu ya CCM Magu mjini kimebebwa na CHADEMA kwa kura nyingi.
Mwl Nyerere ktk Kitabu cha "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" -1973 alipata kusema
"WATU WANAWEZA WAKACHOKA NA KUSEMA POTELEA MBALI WAKACHAGUA CHAMA CHOCHOTE ILI MRADI TU WAONDOKANE NA KANSA YA UONGOZI WA CCM. HAINIFURAHISHI KUYASEMA HAYA ,LAKINI UHAI WA NCHI YETU UNATAKA YASEMWE ."