CHADEMA Yaanikwa Bungeni Jioni Hii!

CHADEMA Yaanikwa Bungeni Jioni Hii!

MAFILILI

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2011
Posts
2,377
Reaction score
1,200
Waziri wa Kilimo Mhandisi Chiza ameichambua HOTUBA ya waziri kilimo wa CHADEMA kuwa haina viwango ilijikita kutoa lawama badala ya majibu muafaka.

Kwa kweli ukifuatilia hotuba ya Waziri Chiza utagundua CCM ipo makini kutatua matatizo ya kilimo wakati CHADEMA wamebaki kupiga kelele kwa kutumia mawaziri vivuli wasio na viwango
 
Hata profesa wao hamna kitu.Mawaziri wao vivuli hawajai hata mkononi. hv kweli wakipewa nchi wataweza kuongoza??
 
Unajua anachofanya waziri chiza ni kuiponda hotuba ya waziri kivuli wa kilimo mh.rose kamili ili wale wabunge wa ccm waliotishia kutoinga mkono bajeti ya w.wa kilimo wabadili msimamo wao.chezea ccm wewe!
 
Kazi ya Chadema ni kukosoa siyo kupigia makofi serikali ndo maana ya vyama vya ushindani/upinzani duniani kote. Kazi ya Serikali ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa kutumia kodi za watanzania wote , wakiwepo wanachadema, na siyo kwa kutumia mishara yao. kukoselewa siyo kulaumiwa.
 
Tumezoea siku hizi kila hotuba ya upinzani eti imejaa lawama,hapa nashindwa kuelewa hivi hawa jamaa wanataka wasifiwe tu
 
Kazi ya Chadema ni kukosoa siyo kupigia makofi serikali ndo maana ya vyama vya ushindani/upinzani duniani kote. Kazi ya Serikali ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa kutumia kodi za watanzania wote , wakiwepo wanachadema, na siyo kwa kutumia mishara yao. kukoselewa siyo kulaumiwa.

Unajua M.P.A , ccm wanachukuwa mda mwingi kukosoa au maoni ya upinzani huku wakichukua ya mwaka jana ya CDM na kuyaweka kwenye mwaka unaofuata
 
Huyu waziri anapaswa kusikiliza Ushauri wa mstahiki mbunge Livingstone Lusinde alisema kazi ya kuwajibu Chadema aachiwe yeye na Mwigulu si umeona wengi wao wamekimbia bunge sasa wako Iringa kuchochea ghasia baada ya makombora ya Mwigulu kulenga shabaha na kuteketeza mpaka ghala lao la silaha feki. Mawaziri tekelezeni Ilani za Uchaguzi kundi la wahuni woteamekabidhiwa Mwigulu akisaidiwa na Mstahiki Lusinde, wakijitutumua tunamuongeza Engineer Stela Manyanya (RC). Sasa hivi wako nyang'anyang'a wanasubiri uamuzi wa kuzima mashine ya kupumulia October,2015 Dkt Jakayaatapomaliza shift yake!
 
Nawashangaa sana magamba kila mwaka bungeni sera zilezile kwenye kilimo,hutasikia wakulima wamenufaika vipi,hutasikia wakulima wameboreshewa masoko ila utasikia wawekezaji wamepewa maeneo ya wananchi,wananchi kunyang'anywa ardhi wakapewa wawekezaji,kila siku bungeni mgogoro wa kuuza pamba alafu leo mnasema mmeboresha kilimo.,endeleen kudanganyana mkifikiri watanzania mambumbumbu..mnakera sana nyie
 
Ccm ni chama cha walanguzi na wachuuzi ndo maana wameanza kugawa mamilioni kule Arusha. Ccm kwa rushwa ni nooma!
 
Kazi ya Chadema ni kukosoa siyo kupigia makofi serikali ndo maana ya vyama vya ushindani/upinzani duniani kote. Kazi ya Serikali ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa kutumia kodi za watanzania wote , wakiwepo wanachadema, na siyo kwa kutumia mishara yao. kukoselewa siyo kulaumiwa.

Wandugu tuwe makini wakati wa kuwachagua mawaziri vivuli angalau wawe na ujuzi wa cheo husika
 
Back
Top Bottom