CHADEMA watoana macho Bungeni

Ah ah ah ah yani chizi siyo lazima avue nguo ndipo umtambue kuwa ni chizi habari kama hizi zimeshaandikiwa sana hapa JF ww siyo wa kwanza lakini mwisho wake ni aibu kwa sababu akuna hata mmoja anayeunga mkono ujinga, kwa sababu saizi kila mtanzania anajua nini kinafanyika kwenye nchi yake matatizo yanayokabili taifa na wanajua yamesababishwa na CCM na serikali yake iweje leo hii ulete hoja yako hapa ambayo aina msingi na manufaa kwenye taifa letu na sisi watanzania wenye akili timamu.

Tunajua chama pekee cha kutuletea ukombozi ni CHADEMA tu na hilo linajulikana na ndo maana wanaungwa mkono na wananchi kwa kiasi kikubwa, sasa nakushauri soma alama za nyakati na ujaribu kuwa makini unapokuwa unaleta hoja yako mezani wanajf kuijadili, pia kajivue gamba alafu urudi tena hapa labda twaweza kukusaidia nini ufanye.
 
Kumbe habari yenyewe imetoka kwenye kipeperushi cha magamaba kiitwacho HABARI LEO.
 

Mkuu mbona kichwa cha habari kimeandikwa namna hii? "Posho yawagawa wabunge Chadema, watatu wapinga" yaani wabunge watatu kati ya 48 kupinga unaita kutoana macho? Hizi mbona ni propaganda cheap sana? Kingine kikubwa ni kwamba mnapoamua kujadiliana jambo ndiyo demokrasia yenyewe hiyo na wanapotokea wengine kutokukubaliana ndiyo demokrasia zaidi. By the way 3/48 ni sawa na 6.25% ina maana wanaokubaliana na hoja ni 93.75%, karibu mara mbili ya kura za kikwete 2010.
 
@Madaya - ccm walisema (categorically) kuwa uchaguzi wa mayor Arusha umeisha. Sasa kwa nini Waziri mkuu akampigie magoti Mbowe na hiki cheo cha unaibu? CCM watakula matapishi mpaka lini? walianza kwa majigambo hakuna haja ya katiba mpya, sasa u-mayor. Mwishoni mtakabidhi (wenyewe) funguo za magogoni maana mambo yanazidi kuwa magumu kila kukicha. By they way, have you agreed kwenye issue ya posho maana Pinda anasema posho inabaki, mjumbe wa NEC -Makamba posho inaondoka, wakati huo huo mpango wenu wa taifa wa maendeleo unasema poshi mwiko. Tell me who is on the ANGUKO?
 
wabunge 48 ila waliokataa ni 3
 

hapo kwenye red ndo ishu ninazozichukia kupindukia, kwanini wamtaje mnyika wawaache hao wengine?? mnamficha nani?
 
hapo kwenye red ndo ishu ninazozichukia kupindukia, kwanini wamtaje mnyika wawaache hao wengine?? mnamficha nani?
Hawa waandishi wa habari wanakera kwa kucreate negative mind kwa watu kisha kuwaacha na maswali bila majibu
 
hapo kwenye red ndo ishu ninazozichukia kupindukia, kwanini wamtaje mnyika wawaache hao wengine?? mnamficha nani?
Hata mimi nakerwa sana. Watajwe tu ili tujue ni nani hao? Kama kweli wapo tusubiri Mwanahalisi Jumatano watasema nani alisema nini na wapi? Ila sio fair kumtaja Mnyika na kuficha majina mengine, kwani wanaogopa nini kama msimamo wao una maslahi kwa Umma?
 

Ama kweli wafuasi wa CHADEMA ni ndege walionaswa kwenye ulimbo, maana hawaambiliki hata kama wakiuona ukweli ukinenwa wanaweka blanketi ili wasiuone.Yaani hata hili hamlioni hatari kwelkweli.
 

mbowe ametoka kuongea mida hii so ukweli umejulikana
 
 
hapo kwenye red ndo ishu ninazozichukia kupindukia, kwanini wamtaje mnyika wawaache hao wengine?? mnamficha nani?

Hapo kweli kabisa, wanawaficha wa nini wakati wamepinga kwenye kikao!? hii habari ya kupikwa kama ni kweli angewataja tu, si walipinga kweupe kwenye kikao?, pia kama ni watatu 3 kati ya 48, tatizo lipo wapi? inamaana 45 wamekubaliana na dio msimamo wa chama, kwani Waziri mkuu akipigiwa kura Bungeni huwa anapata 100%? mbona huwa anaapishwa! na je magamba wao wote wakubaliana kwa kila jambo! na pamoja na kuunga kwao budget kinafiki kwa 100% lakini huwa wanaikosoa sasa kwa nini wanakosoa halafu wanaunga kwa 100%?,

Chadema imewakata pabaya mtaiota mpaka mwisho.
 
Naona chama cha magamba kinazidi kuongeza mgambo wake ndani ya JF kuhakikisha mafisadi wanaendelea kutanua na kuwanyonya wananchi as usual. HATUDANGANYIKI TENA Mpaka tuwatoe. tumeanza na posho ambayo CDM watashinda tu maana wanabaraka zote za Mwenyezi Mungu na wananchi. endeleeni kuchakachua tu lakini shetani wenu anayewasaidia kufanya ufisadi ameishiwa nguvu. peoples power itashinda tu.
 
Kwa mara ya kwanza nina shaka na gazeti la mwananchi kuhusu taarifa hii.gazeti limetaja mwasilisha hoja kuwa ni mnyika.limeenda mbali kidogo na kuelezea mgogoro wa zito na makinda,swali majina ya wachangiaji walio afiki wazo la kukatwa posho yako wapi?majina ya waliopinga posho yako wapi?je hakukuwa na wasioegemea upande wowote?chadema ina wabunge 48 je hakukuwa na muafaka kweli maana nafatilia bunge kila siku na wabunge wote wa cdm hawakubaliani na hoja ya posho,iweje leo washindwe kuafikiana?si kweli
 

mmmmh! HOVYOOOOO KABISA!
 
Hakika nawaambia POSHO itatugawa. POSHO si jambo jema! POSHO inaleta kero. Hakika kuna wabunge wa CHADEMA nimewasikia wakisema suala la posho ni la watu binafsi si la kichama. Jamani kama hakuna sintofahamu kwa nini wote wasiache kusaini wakawa kama Zitto? Hiyo ndi ile unasikia NATAKA SITAKI. Wasisaini basi tujue moja kwamba wana msimamo wa jumla na hawazitaki posho. Ningependa wabunge Kama akina Mh. Selasini, Shibuda, nk. wajitokeze waseme hatusaini kwa kuwa hatuzitaki posho na tunamuunga mkono Zitto kama ni kufukuzwa tufukuzwe wote. Lakini loooh hilo limewakwama kooni.
 
Akifikiri ataungwa mkono, Mnyika aliwataka wabunge kuonyesha moyo huo wa kishujaa kwa kutosaini kitabu cha mahudhurio bungeni, lakini wawepo ndani ya vikao.

Source: Posho yawagawa wabunge Chadema, watatu wapinga

Wako wapi mashujaa wetu? Tunalia nyikani posho za vikao ziondolewe lakini mashujaa wako chini ya uvungu
 
Umbea hauna kwao ...ccm kama tot taarabu mpaka mkuu wao, mtachoka.......posho si za wabunge tu mpaka za jk tumechoshwa na safari zisizo na tija kwa wtz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…