abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Chadema wagoma kuzungumza
Na Richard Makore
30th January 2011
Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana ilikutana Jijini Dar es Salaam kujadili masuala mbalimbali yanayohusu chama hicho ingawa hadi jioni viongozi wake waligoma kusema kilichojadiliwa.Habari za ndani zinasema Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepanga kutarisha Mandamano ya Nchi mzima kuiondosha ccm ikiwa demand za Wtanzania walio wengi hazito sikilizwa.
Akizungumza na NIPASHE jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, Erasto Tumbo alikiri kamati hiyo kujadili mambo mazito lakini alikataa kuyataja japo kwa kifupi.
Tumbo alisema moja ya agenda zilizowasilishwa jana na kujadiliwa ni pamoja na hali ya kisiasa hapa nchini na mikakati ya kazi ndani ya chama kwa mwaka huu.
Kamati hiyo jana ilijifungia ndani siku nzima ambapo baadhi ya wajumbe wake walipoulizwa na NIPASHE kuhusu kilichozungumzwa walikwepa kusema na kumuomba mwandishi avute subira hadi leo itakapotolewa taarifa rasmi ya chama.
Mkutano huo ulifunguliwa na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ambapo wajumbe mbalimbali wakiwemo baadhi ya wabunge walishiriki.
Awali taarifa zilisema moja ya agenda ya kikao hicho ilikuwa ni kupokea taarifa ya wazee wa chama hicho iliyochunguza mwenendo wa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe na baadhi ya wabunge wa chama hicho ambao hawakuhudhuria kikao cha kwanza cha Bunge la 10 mjini Dodoma mwaka jana ambapo Rais Kikwete alihutubia.
Zitto alionekana mwenye furaha na amani wakati akitoka ndani ya kikao hicho kwa ajili ya kupumzika nje huku wajumbe wengine wakiwa wanaendelea na kikao chao na muda mfupi alirejea tena kuungana na wenzake.
Itakumbukwa Zitto alinusurika kufukuzwa katika nafasi ya Unaibu Katibu Mku wa chama hicho kufuatia wabunge wenzake wa chama hicho kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Habari zingine za awali zilibashiri kuwa huenda kikao hicho kitajadili pia tukio la wafuasi wa chama hicho kupambana na polisi mkoani Arusha Januari 5, mwaka huu ambapo watu watatu walipigwa risasi na kufariki dunia.
Chama cha democrasia na maendeleo (Chadema)
[caption id="attachment_27753" align="aligncenter" width="300" caption="Ccm enough kutawala nusu karne tunataka kuona mwanga mpya na matumaini mapya."]