CHADEMA wanuna Zitto kwenda CUF

CHADEMA wanuna Zitto kwenda CUF

kumbe habari iko kwenye hiyo gazeti hadi naua sisimizi kwa nyundo! ni moja ya magazeti ambayo sisomagi. nawausia acheni njaa zenu andikeni habari kwa maslahi ya nchi sisitupo tuta pita lakini tanzania itabaki.
 
Mimi siyo kilaza kama wewe niandike kila kitu, kama hauwezi kununua gazeti shauri yako.

View attachment 216645

Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuber KABWE (CHADEMA) ameitia msukosuko na kuelekea kupasuka Kambi ya Umoja wa Katiba ya Wanachi(UKAWA) baada ya kupanda katika jukwaa la Mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama cha Wananchi (CUF) mkoani Mtwara , chini ya Mwenyekiti wa CHAMA hicho, Prof. Ibrahim Harouna LIPUMBA. LIPUMBA anashutumiwa na CHADEMA kukiuka makubaliano ya UKAWA na kutaka kukigombanisha CHADEMA na wanachama wake kwani Kamati kuu ya CHDEMA ilishatoa maazimio yake kuwa ZITTO asipewe ushirikiano wowote ndani ya CHADEMA na mshirika yeyote wa CHADEMA vikiwemo vyama vya upinzani vinavyounda UKAWA. CHADEMA wanahoji kama itawapendeza CUF kuona FREEMAN MBOWE akizunguka na HAMAD RASHID kwenye majukwaa ya kisiasa.

Katika mkutano huo wa hadhara, ZITTO alimwamgia sifa Prof.Lipumba na kuonesha kuwa ni kiongozi anayefaa kuwatumikia Watanzania ikiwa watampa ridhaa.

Mytake: CHADEMA na CUF wanawatambua ZITTO KABWE na HAMAD RASHID kuwa ni wabunge wa MAHAKAMA kwa maana nyingine vyama hivyo haviwatabui kama wanachama wao na kwa maana hiyo wako huru kufanya siasa popote ilimradi tu hawafanyi hivyo kwa tiketi ya vyama vyao. Nini sasa sababu ya kauli hizi kutoka kwa CHADEMA? Ni uoga , ni wivu au ni nini?
attachment.php



Zitto ni MP wa Upinzani, hivyo kuonekana katika mikutano ya CUF siyo tatizo bali ni kuikomboa nchi yetu kutoka katika panya wanaokula mahindi ghalani.


Wewe umeweka kiushabiki zaidi, lakini ukweli tulishaujadili hapa sana, kwani mkuu Chinga One alishatuhabarisha.

Huenda wewe na gazeti lako ndio mmeiona leo.

Fuatilia hapa na mapicha kibao jinsi kuhusu habari hii. Angalieni tu msije pandisha au kushusha Pressure. bado tunawapenda mfike hadi October 2015.


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...leta-anguko-rasmi-la-ccm-mkoani-mtwara-3.html


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Last edited by a moderator:
chadema wakue sasa hata na cuf vile vile wote washike silaha moja wapambane na ADUI yao mmoja tu CCM// hao akina zitto au hamad rashid warudishwe vyamani na kupewa majukumu kwa mipaka maalumu!

Kumbe tatizo kubwa la watz kushindwa kuiondoa ccm madarakani ni UDINI uliopo. Kuliko watu fulani waichague CDM ni heri wapige kura kwa ccm. Haya mambo ya Lipumba na Zitto mikoa ya kusini sio kitu kingine ni sumu ile ile tu udini.

Zito baada ya kukosa jukwaa la kujitafutia umaarufu cdm sasa anatafuta umaarufu kwa mianya ya kidini. Hawa watu hawatafanikiwa kisisa hata siku 1 kwa mlango huu na ccm inaweza ikaendelea kubaki kwa hasara ya maskini ambao ni wengi zaidi katika mikoa fulanifulani inayosupport ccm! Wajinga ndio waliwao!!!!
 
Back
Top Bottom