TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,868
- 5,753
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuber KABWE (CHADEMA) ameitia msukosuko na kuelekea kupasuka Kambi ya Umoja wa Katiba ya Wanachi(UKAWA) baada ya kupanda katika jukwaa la Mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama cha Wananchi (CUF) mkoani Mtwara , chini ya Mwenyekiti wa CHAMA hicho, Prof. Ibrahim Harouna LIPUMBA. LIPUMBA anashutumiwa na CHADEMA kukiuka makubaliano ya UKAWA na kutaka kukigombanisha CHADEMA na wanachama wake kwani Kamati kuu ya CHDEMA ilishatoa maazimio yake kuwa ZITTO asipewe ushirikiano wowote ndani ya CHADEMA na mshirika yeyote wa CHADEMA vikiwemo vyama vya upinzani vinavyounda UKAWA. CHADEMA wanahoji kama itawapendeza CUF kuona FREEMAN MBOWE akizunguka na HAMAD RASHID kwenye majukwaa ya kisiasa.
Katika mkutano huo wa hadhara, ZITTO alimwamgia sifa Prof.Lipumba na kuonesha kuwa ni kiongozi anayefaa kuwatumikia Watanzania ikiwa watampa ridhaa.
Mytake: CHADEMA na CUF wanawatambua ZITTO KABWE na HAMAD RASHID kuwa ni wabunge wa MAHAKAMA kwa maana nyingine vyama hivyo haviwatabui kama wanachama wao na kwa maana hiyo wako huru kufanya siasa popote ilimradi tu hawafanyi hivyo kwa tiketi ya vyama vyao. Nini sasa sababu ya kauli hizi kutoka kwa CHADEMA? Ni uoga , ni wivu au ni nini?
Katika mkutano huo wa hadhara, ZITTO alimwamgia sifa Prof.Lipumba na kuonesha kuwa ni kiongozi anayefaa kuwatumikia Watanzania ikiwa watampa ridhaa.
Mytake: CHADEMA na CUF wanawatambua ZITTO KABWE na HAMAD RASHID kuwa ni wabunge wa MAHAKAMA kwa maana nyingine vyama hivyo haviwatabui kama wanachama wao na kwa maana hiyo wako huru kufanya siasa popote ilimradi tu hawafanyi hivyo kwa tiketi ya vyama vyao. Nini sasa sababu ya kauli hizi kutoka kwa CHADEMA? Ni uoga , ni wivu au ni nini?