Dkt Kilembwe
Senior Member
- Apr 25, 2015
- 154
- 102
CHADEMA WANAWEWESEKA
Baada ya ziara ya ACT Mbeya chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema chazidi kuweweseka huku ngome zao zikiwa zinavunjwa kwa siasa na hotuba safi za wana ACT.
Chadema wametengeneza kipande cha video kinachoonesha watu kuzomea, ila hakioneshi anazomewa nani ingawa wao wanadai ni Zitto.
Kwa mujibu wa Afande Sele ni kwamba hawakuwa na ratiba ya mkutano Tunduma hivyo yeye na Zzk hawakushuka ndani ya gari, kauli ambayo imethibitishwa na wana ACT wengine waliokuwa katika msafara huo.
Mwanahabari wetu aliamua kuwatafuta wakazi wa Tunduma mkoani mbeya na kuwahoji juu ya hili.
Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Mahenge Regan anadai wao ndio waliosimamisha msafara na kuomba wapatiwe hata neno moja, ndipo mwenyekiti wa ACT na katibu mkuu waliposhuka na kuongea machache kisha wakaondoka. Alipoulizwa kuhusu zomea zomea anasema kuna vijana wachache wa Chadema wakiongozwa na kada maarufu wa Chadema anayejulikana sana kwa jina Mdude Chadema ndio waliokuja na kutaka kuharibu ila Msafara ulikua ushaanza kuondoka.
Ikumbukwe mkakati wa zomea zomea Mbeya uliratibiwa na Mbunge wa Mbeya mjini Mbilinyi akisirikiana na Mary Mwanjerwa wa viti maalumu Ccm.
Kiongozi wa chama ACT Zitto amedai kutokushuka Tunduma na video hizozinazosambazwa ni muendelezo wa siasa chafu za Chadema.
Ikumbukwe pia moja ya mtihani waliopewa watangaza nia na wabunge wa Chadema ni kuhakikisha Ziara za ACT hazifanikiwi ili wapitishwe na chama kuelekea Uchaguzi mkuu, hili limeelezwa na kada mmoja wa Chadema aliyeombwa kuhifadhiwa jina kwa usalama wake.
Wananchi wa mkoani Mbeya wamesikitishwa sana kuhusishwa na uhuni huu unaoratibiwa na mbunge wao na kuonesha kuchoshwa na tabia zake za kuwafanya vijana wao misukule huku yeye anatengeneza pesa.
Mwandishi Huru
Mbeya
Baada ya ziara ya ACT Mbeya chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema chazidi kuweweseka huku ngome zao zikiwa zinavunjwa kwa siasa na hotuba safi za wana ACT.
Chadema wametengeneza kipande cha video kinachoonesha watu kuzomea, ila hakioneshi anazomewa nani ingawa wao wanadai ni Zitto.
Kwa mujibu wa Afande Sele ni kwamba hawakuwa na ratiba ya mkutano Tunduma hivyo yeye na Zzk hawakushuka ndani ya gari, kauli ambayo imethibitishwa na wana ACT wengine waliokuwa katika msafara huo.
Mwanahabari wetu aliamua kuwatafuta wakazi wa Tunduma mkoani mbeya na kuwahoji juu ya hili.
Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Mahenge Regan anadai wao ndio waliosimamisha msafara na kuomba wapatiwe hata neno moja, ndipo mwenyekiti wa ACT na katibu mkuu waliposhuka na kuongea machache kisha wakaondoka. Alipoulizwa kuhusu zomea zomea anasema kuna vijana wachache wa Chadema wakiongozwa na kada maarufu wa Chadema anayejulikana sana kwa jina Mdude Chadema ndio waliokuja na kutaka kuharibu ila Msafara ulikua ushaanza kuondoka.
Ikumbukwe mkakati wa zomea zomea Mbeya uliratibiwa na Mbunge wa Mbeya mjini Mbilinyi akisirikiana na Mary Mwanjerwa wa viti maalumu Ccm.
Kiongozi wa chama ACT Zitto amedai kutokushuka Tunduma na video hizozinazosambazwa ni muendelezo wa siasa chafu za Chadema.
Ikumbukwe pia moja ya mtihani waliopewa watangaza nia na wabunge wa Chadema ni kuhakikisha Ziara za ACT hazifanikiwi ili wapitishwe na chama kuelekea Uchaguzi mkuu, hili limeelezwa na kada mmoja wa Chadema aliyeombwa kuhifadhiwa jina kwa usalama wake.
Wananchi wa mkoani Mbeya wamesikitishwa sana kuhusishwa na uhuni huu unaoratibiwa na mbunge wao na kuonesha kuchoshwa na tabia zake za kuwafanya vijana wao misukule huku yeye anatengeneza pesa.
Mwandishi Huru
Mbeya