Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,100
- 5,649
Naomba kuweka mambo sawa kidogo.
Kuna watu ambao wanaonyesha kila dalili za kuweweseka, ama kuchanganyikiwa au kupumbaa au kuwehuka au kufamiwa na mapepo na kuwa kama mapunguhani fulani hizi wameibuka siku za hivi karibuni na kukisakama CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO katika mpangilio mzuri sana wa mbinu za kiushindani za kihayawani.
Nimeonelea kuweka mambo sawa ili isijie ikaonekana watu wote ni wapungufu wa uelewa wa mambo ya ulimwengu huu hasa hapa nchini.
Kwanza, na ieleweke wazi kwa viongozi wa CHADEMA kwamba, kuna viashiria vya kutosha kuthibitisha kwamba UMA wa watanzania umekwisha amua kukifanya kuwa chama tawala nchini. Maamuzi haya yamefanyika baada ya kupata uelewa kwamba matitizo yooote yanayotukabili watanzania yanachangiwa kwa kiwango kikubwa na uongozi mbovu wa kisiasa uliopo nchini na hivyo wamejawa na imani kubwa sana kwamba CHADEMA ndio mkombozi wao.
Pili, wananchi wanatambua kwamba, serikali na chama kinachoiongoza kinafahamu maamuzi haya ya UMA wa watanzania na hivyo kiko tayari kufanya kitu chochote kile katika kuhakikisha kwamba mapenzi haya ya UMA hayatimiliki kwa namna yoyote ile, wananchi wanatambua kwamba ufanyaji kampeni wa kinyama unaofanywa na chama hiki kuanzia uchaguzi mkuu wa 2010 na chaguzi ndogo za igunga na sasa Arumeru Mashariki unalengo la kuwazuia wananchi wasitimize kwa matendo matakwa yao, wanatambua kwamba uharamia unaofanywa na tume ya uchaguzi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama nchini wa kubaridisha matokeo ya maamuzi ya wananchi juu ya viongozi waliowachagua ni muendelezo ya kuweweseka kwao na ishara za maamuzi ya wananchi dhidi yao, watanzania tunajua kwamba, mbinu zote chafu za kuwadhihaki, kuwapakazia na kuwapiga, kuwanyanyasa, kuwakamata na kuwafungulia mashtaka yasikuwa kuwa na maana yoyote ile katika mahakama zilizo chini yao ni muendelezo wa hujuma za serikali iliyo chini ya ccm dhidi ya matakwa ya wananchi.
Tatu, kutokukata tamaa kwa wananchi na ongezeko kubwa la muamko wa kutaka mabadiriko linalothibitishwa na viashiria kadha wa kadha ni ushahidi kwamba, pamoja na hayo yote yaliyotajwa hapo juu, Imani ya wanchi kwa CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO imekuwa ikiongezeka na kupanuka zaidi na zaidi katika jamii yote ya Jamhuri ya Muungano wa watanzania. Na hivyo basi, Hii inawapa viongozi wote wa CHADEMA jukumu la kutokukata tamaa kwa namna yoyote ile katika mapambano haya ambayo hakika wamekuwa vinara wa kuyasambaza kama moto nchini mwetu.
Nne, Ukianzia na maamuzi waliyoyachukua watanzania kwenye uchaguzi wa Rais Mwaka 2010 hata baada ya kampeni chafu katika historia ya nchi yetu dhidi ya Mgombea Urais wa CHADEMA, DR SLAA NI ushahidi wa kutosha kwamba hakuna propaganda, ushawishi, uchafu, shirki na ghirza za namna yoyote zinaweza kubadirisha kiu ya mabariko iliyotanda nchini kwa mategemeo makubwa sana ya wanchi kwa viongozi na CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO.
Tano, Hivyo basi, wale wote ambao ama wamejitoa akili au wametumwa kufanya uchafuzi wa hali ya hewa kwa CHADEMA na viongizi wake wanapaswa kujua kwamba, wanachokifanya ni sawa sawa kabisa ni kujaribu kufungua kufuri bila funguo, hakuna Mwananchi hata mmoja anayeweza kudanganyika kwa kampeni za kishenzi na hoja zisizokuwa na mashiko,
Hivi sasa watanzania mashtaka yetu yote ni dhidi ya serikali ya chama cha mapinduzi sababu ndicho chenye dhamana ya uongozi wa serikali yetu ambayo imeshindwa kabisa kabisa kufikia hata malengo ya Taifa letu kudai uhuru kutoka kwa mkoroni takrani miaka 50 iliyopita.Na kwamba tunawachukulia nyie viongozi wa CHADEMA kama malaika katika swala zima la uongozi mbovu wa nchi yetu.
LAKINI MTAMBUE KITU KIMOJA, KWAMBA WAKATI TUTAWAONDOA CCM MADARAKANI HUKU TUKISHANGIRIA NA KURUKARUKA KWA FURAHA, ENDAPO MTAFANYA USALITI WA NAMNA YOYOTE ILE BAADA YA KUINGIA MADARAKANI MKAANZA KUENDESHA SERIKALI KATIKA NAMNA INAYOPINGANA NA MATARAJIO YETU WANANCHI ADHABU TUTAKATOWAPA ITASIKIKA MPAKA MASHARIKI ZA MBALI SABABU TUTAWAADHIBU HUKU TUKILIA NA KUTOA MACHOZI YA DAMU.
Kuna watu ambao wanaonyesha kila dalili za kuweweseka, ama kuchanganyikiwa au kupumbaa au kuwehuka au kufamiwa na mapepo na kuwa kama mapunguhani fulani hizi wameibuka siku za hivi karibuni na kukisakama CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO katika mpangilio mzuri sana wa mbinu za kiushindani za kihayawani.
Nimeonelea kuweka mambo sawa ili isijie ikaonekana watu wote ni wapungufu wa uelewa wa mambo ya ulimwengu huu hasa hapa nchini.
Kwanza, na ieleweke wazi kwa viongozi wa CHADEMA kwamba, kuna viashiria vya kutosha kuthibitisha kwamba UMA wa watanzania umekwisha amua kukifanya kuwa chama tawala nchini. Maamuzi haya yamefanyika baada ya kupata uelewa kwamba matitizo yooote yanayotukabili watanzania yanachangiwa kwa kiwango kikubwa na uongozi mbovu wa kisiasa uliopo nchini na hivyo wamejawa na imani kubwa sana kwamba CHADEMA ndio mkombozi wao.
Pili, wananchi wanatambua kwamba, serikali na chama kinachoiongoza kinafahamu maamuzi haya ya UMA wa watanzania na hivyo kiko tayari kufanya kitu chochote kile katika kuhakikisha kwamba mapenzi haya ya UMA hayatimiliki kwa namna yoyote ile, wananchi wanatambua kwamba ufanyaji kampeni wa kinyama unaofanywa na chama hiki kuanzia uchaguzi mkuu wa 2010 na chaguzi ndogo za igunga na sasa Arumeru Mashariki unalengo la kuwazuia wananchi wasitimize kwa matendo matakwa yao, wanatambua kwamba uharamia unaofanywa na tume ya uchaguzi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama nchini wa kubaridisha matokeo ya maamuzi ya wananchi juu ya viongozi waliowachagua ni muendelezo ya kuweweseka kwao na ishara za maamuzi ya wananchi dhidi yao, watanzania tunajua kwamba, mbinu zote chafu za kuwadhihaki, kuwapakazia na kuwapiga, kuwanyanyasa, kuwakamata na kuwafungulia mashtaka yasikuwa kuwa na maana yoyote ile katika mahakama zilizo chini yao ni muendelezo wa hujuma za serikali iliyo chini ya ccm dhidi ya matakwa ya wananchi.
Tatu, kutokukata tamaa kwa wananchi na ongezeko kubwa la muamko wa kutaka mabadiriko linalothibitishwa na viashiria kadha wa kadha ni ushahidi kwamba, pamoja na hayo yote yaliyotajwa hapo juu, Imani ya wanchi kwa CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO imekuwa ikiongezeka na kupanuka zaidi na zaidi katika jamii yote ya Jamhuri ya Muungano wa watanzania. Na hivyo basi, Hii inawapa viongozi wote wa CHADEMA jukumu la kutokukata tamaa kwa namna yoyote ile katika mapambano haya ambayo hakika wamekuwa vinara wa kuyasambaza kama moto nchini mwetu.
Nne, Ukianzia na maamuzi waliyoyachukua watanzania kwenye uchaguzi wa Rais Mwaka 2010 hata baada ya kampeni chafu katika historia ya nchi yetu dhidi ya Mgombea Urais wa CHADEMA, DR SLAA NI ushahidi wa kutosha kwamba hakuna propaganda, ushawishi, uchafu, shirki na ghirza za namna yoyote zinaweza kubadirisha kiu ya mabariko iliyotanda nchini kwa mategemeo makubwa sana ya wanchi kwa viongozi na CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO.
Tano, Hivyo basi, wale wote ambao ama wamejitoa akili au wametumwa kufanya uchafuzi wa hali ya hewa kwa CHADEMA na viongizi wake wanapaswa kujua kwamba, wanachokifanya ni sawa sawa kabisa ni kujaribu kufungua kufuri bila funguo, hakuna Mwananchi hata mmoja anayeweza kudanganyika kwa kampeni za kishenzi na hoja zisizokuwa na mashiko,
Hivi sasa watanzania mashtaka yetu yote ni dhidi ya serikali ya chama cha mapinduzi sababu ndicho chenye dhamana ya uongozi wa serikali yetu ambayo imeshindwa kabisa kabisa kufikia hata malengo ya Taifa letu kudai uhuru kutoka kwa mkoroni takrani miaka 50 iliyopita.Na kwamba tunawachukulia nyie viongozi wa CHADEMA kama malaika katika swala zima la uongozi mbovu wa nchi yetu.
LAKINI MTAMBUE KITU KIMOJA, KWAMBA WAKATI TUTAWAONDOA CCM MADARAKANI HUKU TUKISHANGIRIA NA KURUKARUKA KWA FURAHA, ENDAPO MTAFANYA USALITI WA NAMNA YOYOTE ILE BAADA YA KUINGIA MADARAKANI MKAANZA KUENDESHA SERIKALI KATIKA NAMNA INAYOPINGANA NA MATARAJIO YETU WANANCHI ADHABU TUTAKATOWAPA ITASIKIKA MPAKA MASHARIKI ZA MBALI SABABU TUTAWAADHIBU HUKU TUKILIA NA KUTOA MACHOZI YA DAMU.