Chadema Wanalipwa posho ya 30,000 Igunga!

Kumekua na malalamiko ya makada ambao wametangulia hapa Igunga kwa maandalizi ya Kampeni kwa kulipwa posho ya Tsh 30,000 kwa siku! Hapa Igunga lodge ya bei ya Chini ni 15,000! Kumekua na majibu ya hovyo kutoka kwa Ndugu Komu wa CDM hq kuwa kwa sasa kama mtu hana wito na CDM basi asishiriki kampeni hizo!
My take: Posho ya Tsh 30,000 haitoshi na inawapa wakati mgumu maafisa hawa ambao wana umhimu wa kuratibu kampeni! Kuna umhimu wa Katibu mkuu wa CDM kuingilia kati suala hili na kuipandisha posho hata kufikia 50,000 kwa kuzingatia kupanda kwa gharama za maisha!

kama watu waliingia kwenye chama kutegemea kunufaika binafsi hiyo inabidi wasahau,natumaini chadema itabidi ipigane sana na tabia ya watu wanaofikiria kuingia kwenye chama ili wanufaike zaidi,je wanachama ndo wanao toa michango yao kwa ajili ya kuendesha chama tena kwa kujitolea sasa kama mtu anahisi hawezi kuishi kwa hiyo tsh30000 ameenda kufanya nini huko,tena ashukuru kupewa hiyo tsh30000 mimi nafikiri ule wakati wa chama kuanza kuomba omba hela kwa wafanyabiashara ili kuendesha chama naomba chadema wasifike huko ndiko kutaua uhuru wa kuendesha chama kwa viongozi wa chama,wanachama tutajitolea wenyewe kwa michango au kwa hali{ kufanya kazi bila malipo}na mali{ fedha etc }kuweza kufikia uhuru tunaopigania kama mtu anahisi hawezi kupigania uhuru wake mpaka alipwe akae pembeni tu
,chama kitajengwa na wanachama watakakuwa na moyo bila kutegemea kulipwa fadhila tuondokane na uccm kuhisi chama kina fedha zinatoka wapi ,hela ya ruzuku itatumika kuendeshea chama kwa baadhi ya idara ambazo zimeajiri baada ya kuonekana ni muhimu kufanya hivyo au kwenye issue za dharura zinazotokea lakini sio kulipana posho ,je wangeambiwa wake kambini badala ya guest house je ingekuaje?
 
Chadema inatakiwa kuwa na maofisa wachache sana wa full time walipwe lakini wengine kama mimi na wewe tuijenge Chadema kwa kila aina ya uwezo wetu tulio nao .Kama mtu hana kipato anategemea Chadema this will be hard maana hakuna pesa hizo .Aende CCM wanazo sisi Chadema hakuna na tunataka watu wajue kwamba Chadema si kijiwe cha kuganga njaa ni kazi pekee pale .Posho ya 30,000 kijini ni kubwa sana sana siamini kama Igunga iko kama Nyamagana kwa mfano.Jamani isaidieni Chadema .

Mkuu igunga si kijijini.

Tatizo ni kwamba wadogo wanajitolea lakini wakubwa wakijitolea baadaye wanakuja kukidai Chama!!! Kuna mkubwa mmoja alijitolea mafuso (Uwezo wake ni mkubwa kwa hiyo kujitolea fuso ni sawa) lakini baada ya kuona ruzuku imeingia akasema hayo magari yanunuliwe na Chama!! Hapa kulikuwa na kujitolea kweli?
 
John Marwa, Rejao, na yule dada lao moja. nanihhiiii wa MAGAMBA
Hapa tumeweka itikadi za vyama vyetu pembeni!
Unawezaje kuishi nje ya kituo chako cha kazi kwa posho ya 30,000?
Hata mtumishi wa kawaida serikalini halipwi posho ndogo hivyo!
Huu ni unyanyasaji mkubwa!
 
Sakata la akina Devid Kafulila lilianza kama hivi hivi,wakilalamikia posho kule Busanda' hata hawa wanaolalamika namna hii nadhani ni type hizo! Haya basi wewe upo peke yako efu 15 haikutoshi kula mchana na jion.Maana yake ni hii kwao elfu 5 asubuhi nyingine mchana na elfu tano jioni kwao haziwatoshi! Pumbafu kabisa mbona hata kadi ya Chadema inaeleza vizuri kuhusu kujitolea kujenga chama! Mwita Mwikwabe hebu atujuze kama kweli hali ndiyo hii!
 
30,000 kwa siku ngapi? na kwa watu wangapi? Na hawa makada wanalipwa mishahara vile vile au ni hizi posho tu?

Mkuu hawa wabunge wana napewa mshahara na bado huko waendako wanalipiwa hotel za kulala ni kujipanga na jinsi ngani mtakavyo tumia pesa yenu, kwahiyo hiyo posho ya elfu 30 Tsh. sidhani kama ni mbaya.
 
Kama inahusu, waongezewe tu. Katika misingi 8 ya uchumi, incentive ni mojawapo
 
katika mazingira ya kawaida posho si mshahara bali ni incentive ya kumfanya mtu afanye kazi kwa kujituma zaidi na kwa moyo mkunjufu. Lakini mara myingi kiwango cha posho kinatakiwa kifanane na mazingira na hali halisi ya kiuchumi wa eneo husika na hali ya kiuchumi wa chama kinachotoa posho hiyo. kwa ruzuku ya chadema kwa sasa wanaweza kutoa posho zaidi ya hiyo na ikiwa imethibitika kuwa kwa sasa hali ya maisha ndani ya igunga ipo juu kutokana na idadi ya watu kuongezeka na pilika za uchaguzi. Ikiwa iliwezekana kwa Dr slaa kulipwa mshahara wa zaidi ya milioni saba mbali na posho anazopewa, vipi ishindikane kwa watu hawa wapiganaji kulipwa elfu hamsini....!
 
..........................................Nakubaliana na wewe mkuu 30,000 ni ndogo,hiki chama ni cha umma wa watanzania tofauti na CCM ambacho kimenunuliwa na mafisadi,kinatakiwa kujengwa na wenye moyo tu....itafika pindi unapaswa kujitolea kwa ajili ya kutetea taifa lako halafu unadai posho....naomba kuwaasa makada wenzangu wa CDM kuwa "CHADEMA ITAJENGWA NA WENYE MOYO,NA WENYE MOYO NDIO WATAOIJENGA CHADEMA...." Na wenye moyo ndio wao...kazeni buti sisi tuko nyuma yenu kwa maombi na vita ya maneno kama tunavyofanya hapa JF na kwenye vyombo vingine vya habari...........VIVA CHADEMA,GO CHADEMA........
 
Hivi hao maofisa ni wanafunzi au watu wazima? Mtu mzima unampaje 30,000 kwa siku? Hiyo familia yake anaiachaje? Moyo wa kujitolea ni mhimu lakini hapahapa JF tuliambiwa Katibu Mkuu wa Chademu Dr Slaa anapewa Posho ya 7milioni kwa mwezi na ndio ukawa utetezi hata hapa JF kuwa asilipe kodi kwakuwa ni posho tu! Kujitolea kwa ajiri ya Chama kusiwe na madaraja kwa wanaoneemeka na wanaopewa sound ya kujitolea kujenga Chama!
 
CDM kwa kweli hawana dhamira ya dhati ya kuwatumikia Wananchi wa Tanzania huu ndio ukweli!
Suala la posho kwa CDM mbona nilimekuwa ni tatizo hata kipindi kile walivyokuwa wanafanya maandamano yasiokuwa na tija kwa taifa kulikuwa na malalamiko makubwa ya posho za maandamano.
Viongozi wa juu Mbowe, a loser Dr Slaa, Lissu, hawa walikuwa wanachukuwa posho kila maandamano 650.000 hii ni nje ya malipo ya hoteli na malazi.
Wabunge kina Regia, Lema, Wenje, Selasini, kila mmoja analipwa posho ya maandamo 400.000 hii ni nje
ya hotel na malazi, sasa leo mnakwenda kuwalipa watu wazima posho ya 30,000 kwa siku huu ni udhalilishaji wa hali ya juu kabisa, wakati chama kinapokea mamilioni kila mwezi kama ruzuku
 
Hivi hao maofisa ni wanafunzi au watu wazima? Mtu mzima unampaje 30,000 kwa siku? Hiyo familia yake anaiachaje? Moyo wa kujitolea ni mhimu lakini hapahapa JF tuliambiwa Katibu Mkuu wa Chademu Dr Slaa anapewa Posho ya 7milioni kwa mwezi na ndio ukawa utetezi hata hapa JF kuwa asilipe kodi kwakuwa ni posho tu! Kujitolea kwa ajiri ya Chama kusiwe na madaraja kwa wanaoneemeka na wanaopewa sound ya kujitolea kujenga Chama!

Mkuu wakubwa huwa hawajitolei, wanajitolea wadogo tu. Katibu anajitolea kwa kulipwa posho ya mil. 7 na mwenyekiti alijitolea mafuso yake lakini baada ya kuona ruzuku imeingia akaamua kukilazimisha chama kiyanunue!! Tunajtolea kwa mafungu sasa!!
 
Hapa tumeweka itikadi za vyama vyetu pembeni!
Unawezaje kuishi nje ya kituo chako cha kazi kwa posho ya 30,000?
Hata mtumishi wa kawaida serikalini halipwi posho ndogo hivyo!
Huu ni unyanyasaji mkubwa!
Leo mbwa atapiga mswaki ni ajabu John Marwa, Rejao, Mlengo wa kati, Ritz na mama lao kuwa watetezi wa Chadema, siku hizi mmeshindwa kabisa kuja kwa hoja imebaki ni hizi zisizo na mashiko.
 
Leo mbwa atapiga mswaki ni ajabu John Marwa, Rejao, Mlengo wa kati, Ritz na mama lao kuwa watetezi wa Chadema, siku hizi mmeshindwa kabisa kuja kwa hoja imebaki ni hizi zisizo na mashiko.
Feedback,
mimi nyumbani mbona mbwa wangu watatu wote napiga mswaki kila siku.
Hizi hoja wewe lazima uzione hazina mashiko sababu CDM wameishakupa upofu ujitambui tena, akili imefunikwa na blanket jeusi umekuwa mateka wa Mbowe!
Lakini raia wa Tanzania wapenda amani na haki hizi hoja zina mashiko
 
Hivi hao maofisa ni wanafunzi au watu wazima? Mtu mzima unampaje 30,000 kwa siku? Hiyo familia yake anaiachaje? Moyo wa kujitolea ni mhimu lakini hapahapa JF tuliambiwa Katibu Mkuu wa Chademu Dr Slaa anapewa Posho ya 7milioni kwa mwezi na ndio ukawa utetezi hata hapa JF kuwa asilipe kodi kwakuwa ni posho tu! Kujitolea kwa ajiri ya Chama kusiwe na madaraja kwa wanaoneemeka na wanaopewa sound ya kujitolea kujenga Chama!


Hapo mikwaju ya wenyewe kwa wenyewe inaanza,sisi tunashangilia tu kwani hawatakuwa makini katika zoezi zima la usimamizi na hapo ndo tunapiga bao.Vita vya panzi.
 
30,000 kwa siku ngapi? na kwa watu wangapi? Na hawa makada wanalipwa mishahara vile vile au ni hizi posho tu?
<br />
<br />
Elfu 30,000 kwa siku mkuu mtoa maada nae ni mzushi igunga gesti ya elfu 10,000 ni nzuri mno,unapata self safi inabaki 20,000 unakula chakula safi na bia juu na chenji inabaki kabisa hapo.
 
Elfu 30,000 kwa siku mkuu mtoa maada nae ni mzushi igunga gesti ya elfu 10,000 ni nzuri mno,unapata self safi inabaki 20,000 unakula chakula safi na bia juu na chenji inabaki kabisa hapo.
Hawa ndio viongozi wa BAVICHA angalia mawazo yake anawaza pombe tu! Mtu katoka Moshi kaicha familia yake kaenda Igunga kukitetea Chama chenu mnapa 30,000 huko nyumbani Moshi atatuma kiasi gani na yeye atumie kiasi gani!
Kwanza Igunga hakuna hoteli ya 10,000 labda uende igunga vijijini, Igunga hoteli rahisi ni 15.000 mpaka 18.000 halafu mnataku kushinda ubunge
 
Back
Top Bottom