Ndugu zangu,
Toka awali Rais Samia aape kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wafuasi wa CHADEMA walianza kumpangia nani awe makamu wake, akawakwepa.
Hawakuchoka, wakachachamaa avunje baraza la mawaziri. Akawapuuza.
Kwenye safu ya makatibu wakuu pia hawakuchoka, wakiendelea kupiga ramli. Akawapuuza.
Sasa hivi wamejikita kwenye safu ya Ma-RC, DC na DED, wanasambaza picha hadithi za makada wa CCM wanawataka na wale wasiowataka. Ni suala la muda tu lakini hata huku napo watapuuzwa.
Baada ya kupuuzwa watarudi kwenye hoja yao ya kudumu ya kupinga kila jambo na kuporomosha matusi.
Muda utasema
Vumbi la msiba hakika lingali kutulia. Kwani hata hawa ni chadema?
Ninashauri Rais Samia Suluhu asipewe uenyekiti wa CCM
Rais yeyote anapoingia madarakani Kuna mambo mawili hutokea. 1. Expectations za makundi mbalimbali kuwa yataguswa maslahi yao. ✓Watumishi wanafikiria kuongezwa mshahara. ✓Wanasiasa wanawaza kupanda vyeo. Waliopo nje wanatani waliopo madarakani watumbuliwe ili wao wachukue nafasi. ✓ Wakulima...
www.jamiiforums.com
Dalili za wazi kuwa mleta mada ma wenziwe wamevurugwa kweri kweri!
Au nasema uongo ndugu zangu?