Wengi watashangaa kichwa cha habari lakini ukweli watu wawili waliopo chadema ndio waliofikisha nchi hapa
Hii hali ngumu wanayoipigia kelele chadema na kusema deni la taifa limepanda nchi imeingia mikataba mibovu,kila kukicha mali za nchi zinakamatwa
inasikitisha kua hawa waliokua vinara wa kusababisha cancer hii ,
wao ndio wamekua mstari wa mbele kulalama kama ni malaika ambao wameshushwa upya toka mbinguni na hawajafanya chochote wala hawakuwepo serikalini
Fedrick sumaye ndie waziri mkuu aliekaa muda mrefu madarakani kwa miaka 10
ndio kipindi ambacho taifa lilishuhudia uza uza kwa bei ya kutupa kwa kisingizio cha kubinafsisha
ikiwa yeye alikua ni mshauri wa rais na boss wa mawaziri wote mchango wake ulikua ni upi kipindi chake nchi ndio ilioingia mikataba mahotelini
yeye hakua mzalendo wala na uchungu kipindi hicho uzalendo huo uzaliwe sasa ni mengi madudu yake lakini tusiogope kumuhoji mtu huyu bila soni haijalishi ni mwenyekiti wala nini
Lowassa utetezi wake usio na mashiko vurugu zote za awamu ya nne yeye alishiriki kwa namna moja ama nyingine hata alipofukuzwa uwari mkuu aliendelea kulihujumu taifa akiwa nje ya baraza la mawaziri kupitia vyeo vyake vya kamati za bunge na chama
Hawa watu wawili si watu wa kuwachekea kama ni china siku nyingi wangekua wamekufa kifo cha kishujaa cha kitanzi,
Leo hii bila haya wanasimama jukwaani kuwakejeli wananchi wenye hali mbaya kiuchumi na bado pia mazuri yanayofanywa na magufili hawataki kuyaunga mkono wanayapinga ili waendelee kuneemeka na maovu yao
Tusiogope kuwahoji chadema na tusikubali hoja nyepesi za mbowe na hao watu wawili
Tanzania bila ufisadi inawezekana
Tumuunge mkono juhudi za maendeleo zimeanza kuonekana changamoto kila mahali duniani hazikosekani!