Nahis kama natamani hivi kutaka kukuunga mkono kwa 100%... ila kama ndivyo maoni yako ndo haya kwanini uliacha kuniunga mkono wakati napigia upatu suala la what's so called "Good Governance" ambayo ingawaje ni mfumo wenye jina tamu na la kuvutia lakini kimsingi ni mfumo unaotumika kama kichaka cha mafisadi na viongozi wazembe... mfumo unaoshadidia utawala wa sheria, yaani utawala wa sheria utoke kwa mafisadi na wazembe... what a ----! Nasi kama mazuzu tumekuwa tukishadadia kwa mbwembwe na vifijo bila kujiuliza ni kwanini leo viongozi wa Afrika ambao kwa miongo kadhaa wamekuwa wakipinga mifumo inayoletwa na watu wa magharibi, hivi sasa viongozi wetu wanaunga mkono mfumo wa utawala bora walioletewa na hao hao watu wa magharibi... hatutaki kujiuliza, WHY? Kumbe jibu ni simple, wanaushabikia mfumo huu coz' kichaka cha uovu wao... huwezi kuwafanya chochote coz' ni mfumo unaozingatia utawala wa sheria... whereas, a person atabaki mtuhumiwa hadi ithibitike beyond reasonable doubt kwamba ametenda kosa analotuhumiwa! Kama si utawala wa kijeshi kama unavyopendekeza basi tu-replace Approved Dictatorship Governance with Good Governance!