CHADEMA waifungulia CUF njia…

Hamad Rashid mara nyingi tu ameshazungumzia masuala yanayohusu tanzania Bara.

Umeshawahi kusikia Mbowe anazungumzia swala la Pemba?

Kweli wewe na Uelewa wako PEMBA ina Wawakilishi; Wabunge Wengi ki Mraba zaidi ya Tanganyika sasa unataka na huyo MBOWE bado aizungumzie PEMBA? sasa huo sio UKIRITIMBA ni nini?

Kweli haujui kuwa Tanganyika ina matatizo mengi zaidi ya PEMBA? na ina Utajiri lakini unachotwa na VIONGOZI wakuu wabovu wasiojua jinsi gani ni bora kutunza na kulinda Maliasili; Madini; Malighafi za nchi...

Kweli umenishitua...
 
Attitude za watu kama ZeMarcopolo ndio zinaimaliza nchi yetu. Anapoandika thread zake unapata "tone" ya mtu ambaye ni arrogant,mbinafsi,mnafiki,mzandiki,mwenye uzoefu wa mipasho isiyo na tija kwa taifa bali kwa kundi la watu fulani, mtu aliyejengwa na propaganda zaidi kuliko umahiri wa kuandika mambo yenye kuleta tafari ya maslahi mapana ya Tanzania. Kuwa yeye ni yeye tu na yeye ndiye mwenye funguo za mlango wa chumba cha fikra sahihi za ni wapi Tanzania inakopaswa kwenda. Na kwamba kila mtu anayetaka kufikiri lazima aombe funguo toka kwake. Ukiangalia mabali zaidi kwa kutumia jicho la tatu unagundua kuwa aandikacho ZeMarcopolo na ile hali inayokuja na kile aandikacho ndio kitambulisho hasa cha watawala wetu tulionao madarakani ndani ya CCM na hata serikalini. Kwa hiyo ZeMarcopolo ndani ya JF ni kielelezo halisi na ushahidi wa fikra za watawala(sio viongozi)wetu na wale wanaofaidika kupitia watawala hao.
 

Kwahiyo ni wajibu wa mbunge wa Pemba kuzungumzia maswala ya Tanzania bara lakini mbungewa Tanzania Bara hapaswi kuzungumzia maswala ya Pemba?
Najua hiyo ni sehemu ya sera ya chadema ya majimbo lakini haiko sahihi kwenye hilo.
 

Mawazo yako yanavumiliwa kadri yanavyostahili.

Hata hiyo hoja ni jinsi vurugu za chadema bungeni zinavyoipa mwanya CUF kisiasa...
 
Kwahiyo kwa hiyo ni wajibu wa mbunge wa Pemba kuzungumzia maswala ya Tanzania bara lakini mbungewa Tanzania Bara hapaswi kuzungumzia maswala ya Pemba.
Najua hiyo ni sehemu ya sera ya chadema ya majimbo lakini haiko sahihi kwenye hilo.

Pemba ina BUNGE lake Baraza la Wawakilishi halafu Ina Wabunge BUNGE la Muungano... Sasa Unataka Kiongozi wa UPINZANI pia awe anatoa kipaumbele Mambo ya PEMBA kwanza na Wakati TANGANYIKA kuna issues kibao CHAMA TAWALA cha CCM kimeirudisha NCHI NYUMA' Nchi ni kama vile enzi za STONE AGE; Hakuna UMEME; Hakuna MAJI; Hakuna Malazi; Hakuna ELIMU; Hakuna KAZI ... wewe nadhani unaishi wa upendeleo au kwa MLO wa KIFISADI hauoni hayo matatizo hata kidogo unawaza matatizo ya PEMBA kweli tutafika? changes comes from within!!! kama unaogopa kujirekebisha mwenyewe kwa Maovu yako mwenyewe then U R DONE and finished!!! Don't throw out the blame to others just because you can...
 
Chama cha kuchana viongozi wa serikali kweli kinaongozwa na wala ganja wengi.
Suguuu sura kaa chuma
 
Anzisha mada yako kuhusu CUF. Hapa tunaijadili CHADEMA. Inaonekana shule ulikuwa unafeli sana wewe kwa ajili ya kushindwa ku concentrate kwenye kitu kimoja :smile-big:

Ni wewe uliyesema Chadema ni CCM B sasa inaonyesha jinsi ulivyofaulu shule hizo ulizokwenda... mimi ni wa kufeli nikataka kujua Je, CUF ni wapi ? Swali na ELIMU haina hasira...
 

siasa za tanzania taabu sana, mijitu kama hii ambayo haina uchungu na nchi yetu ni janga la taifa, ccm imeongoza miaka 50 hakuna la maana badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma, angalia rwanda nchi ndogo ambayo uchumi wake unapaa kama ndege, sisi tumekalia kukomalia vitu visivyo na maana, ona kampuni za simu zinavyotuibia, mikataba mibovu, ona ufisadi , elimu kuporomoka, leo hii mtu anasimama na kuanza kuitetea ccm, shame on you. Maendeleo yeyote yanatokana na uongozi bora. Ccm wameshindwa kabisa. Lazima tuwe na uchungu wa nchi tuseme ukweli. Na bila chadema hali ingekuwa mbaya sana. Mungu ibariki tanzania
 
Upuuzi mtu!!

Wakati unalinganisha Bunge la 10 unakosa kulinganisha Makinda na Sitta, kulinganisha Hamad na Mbowe!! Unalinganisha vipindi na matukio, na havileti picha unayotaka kuieleza.

Kuhusu kutekeleza ahadi. Kila kona CCM inaendelea kusema yanayotendwa ni Ilani ya Uchaguzi ya CCM!! Kuna ahadi ngapi ambazo Rais wa Jamhuri kashindwa kutekeleza? Au na yeye ni Chadema??
 
Mawazo yako yanavumiliwa kadri yanavyostahili.

Hata hiyo hoja ni jinsi vurugu za chadema bungeni zinavyoipa mwanya CUF kisiasa...

Kuna vurugu gani Bungeni?? Hata Spika unasikia kafuta iliyodaiwa kuwa kesi dhidi ya wabunge wa Chadema na waliweka wazi kuwa hawatahojiwa. Usijifanye unasahau, Chadema wanafahamu tafsiri ya Sheria za Bunge kuliko unavodhani. Na hii ndio tofauti usiyoiona kati ya kambi za Upinzani za Bunge la 10 na 11!!!

Kwa taarifa yako tu, CUF inaweza kufanya vizuri Pemba na Zanzibar, sio Bara!! Uthibitisho wa hili ni nguvu inayotumiwa na CCM na serikali kudhibiti mafanikio ya kisiasa ya Chadema. Zamani ilisemwa Chadema iko mijini na kwamba mtaji wa CCM uko vijijini. Hatusikii msemo huu tena baada ya Chadema kuanza kushinda chaguzi kadhaa huko vijijini tena kwenye strongholds za CCM kama mkoa wa Tanga. Wakati CUF inafifia, Chadema inajipanua na CCM inafanya kazi ya kudhibiti upinzani kwa hila badala ya kuleta maendeleo au kutekeleza wanachoita Ilani ya Uchaguzi.

PS. Mimi si muumini wa vyama!!
 
Snoopy Doggy Doggy. Wewe na Chemba cha choo na Nepi inatakiwa muimbe bendi moja.
 
Mkuu umechambua hoja kwa umakini mkubwa Chadema inaelekea walipo UMD.
 
CHADEMA imechoka kiasi kwamba Mh. Sugu anachangia pumba bungeni na Mh. Nassari yeye hajui umuhimu wa Nyuki, kwa kweli 2015 CUF njia nyeupe kwao ya kuwa chama kikuu cha upinzani.
Na yule wa Nkasi anasema tulime bangi liwe zao la biashara...Bado yule wa Korogwe hajasema serikali itambue uchawi nk
 
hatuwezi kushirikiana na vibaraka wa ccm. bora tuwe wachache wanao elewana bila kuzungukana. wewe utashirikiana na mbatia, lyatonga au ccm b?. mia
 
hatuwezi kushirikiana na vibaraka wa ccm. bora tuwe wachache wanao elewana bila kuzungukana. wewe utashirikiana na mbatia, lyatonga au ccm b?. mia

Chadema ikiwa peke yake ni vurugu tupu kama unavyoona. Mijadala ya kitaifa inafeuzwa ngonjera!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…