CHADEMA waifungulia CUF njia…

CHADEMA waifungulia CUF njia…

ZeMarcopolo

Platinum Member
Joined
May 11, 2008
Posts
14,279
Reaction score
7,681
CHADEMA imeshindwa kuitumia vizuri nafasi yake kama chama kikuu cha upinzani kwa manufaa ya taifa.

Hali ilianza kuonekana tangu awali baada ya uchaguzi mkuu ambapo CHADEMA ilikataa kushikisha vyama vingine kwenye uongozi wa upinzani Bungeni. Uamuzi huu wa cHADEMA uliwasikitisha wapenda mabadiliko wengi.

Hii ni tofauti na chama cha wananchi CUF ambacho kiliishirikisha chadema kwenye uongozi wa upinzani Bungeni katika Bunge liliopita. Manufaa yake kwa taifa tumeyaona, Bunge la tisa liliweza kusimamia hoja nzito za kitaifa na kuitetemesha serikali mpaka Waziri Mkuu akajiuzuru. Bunge hili la 10 lina wabunge wengi zaidi wa upinzani lakini hakuna mafanikio yoyote katika kujenga hoja!

Zaidi ya hilo, mara kadhaa CHADEMA wamekuwa wakikimbia mijadala kwa mtindo wa kususa ambao haujawahi kuleta manufaa yoyote. Jambo kama la kususia hotuba ya Mkuu wa Nchi halikuwahi kutokea Bungeni wakati CUF ilipokuwa chama kikuu cha upinzani kwenye bunge la 9.

Kadri siku zinavyoenda wananchi wanazidi kushuhudia jinsi CHADEMA inavyoshindwa kuwakilisha maslahi ya taifa Bungeni. Jambo linalosikitisha zaidi ni kwamba siku hizi wabunge wa CHADEMA wakiongea taarifa pekee inayoweza kutolewa ni kwamba "wamemchana kiongozi fulani".

Anayeongoza katika tabia hii ya "kuchana" ni Sugu ambaye jana ameelezewa kuwa alimchana mbunge wa Iramba Mashariki. Huo ndio ulikuwa mchango wake kwenye bajeti ya Waziri Mkuu!!!

Kwa kweli inasikitisha pale input ya speech ya mbunge katika kuchangia bajeti ya Waziri Mkuu inapokuwa ni kumchana kiongozi! Mambo haya hayakuwepo Bungeni wakati CUF ilipokuwa chama kikuu cha upinzani Bungeni. Hamad Rashid wa CUF alikuwa maridadi zaidi katika kusimamia shughuli na hoja za upinzani Bungeni kuliko anavyofanya kiongozi wa upinzani wa Bunge hili la 10.

Picha inayowekwa na CHADEMA ni kwamba upinzani ni vurugu. Wananchi wastaarabu wanaanza kuchukizwa na tabia za uvunjifu wa kanuni na kumkosea heshima Spika zinazofanywa na wabunge wa chadema. Hamad Rashid wa CUF hakuruhusu hili, lakini kiongozi wa sasa wa upinzani Bungeni anaona vurugu na kubishana na Spika kama burudani.

Nikumbushe tu kuwa taarifa zilizopo zinaonyesha hakuna mbunge hata mmoja wa CHADEMA aliyeweza kutekeleza ahadi zake alizotoa kwa wananchi jimboni. Kwahiyo wananchi wanaweza kuwa na imani na wabunge wa CHADEMA iwapo wataona angalau Bungeni wana michango yenye tija.

Kwavile jimboni wabunge wa chadema hawatekelezi ahadi na Bungeni wanaenda "kuchanana" wananchi watakuwa hawana sababu ya kuchagua CHADEMA. Hasahasa ikizingatiwa kuwa chadema kimekuwa ni chama kinachoainisha matatizo bila kutoa jinsi yoyote ya utatuzi.

Vilevile CUF watakuwa na sababu ya kuwaambia wananchi kuwa CHADEMA wameharibu image ya upinzani Bungeni - jambo ambalo ni kweli. Jambo hilo litaiwezesha CUF kuchukua kura nyingi za wapenda upinzani ambazo zingeweza kuwa za CHADEMA katika majimbo ya Tanznia Bara. Kwa vigezo hivyohivyo CHADEMA itaendelea kukosa kura za Zanzibar.

Bottomline: CHADEMA imeligeuza Bunge kuwa jukwaa la kampeni. CUF walipokuwa wanaongoza upinzani Bungeni walisimamia hoja kwa maslahi ya taifa. Tabia ya vurugu na kumkosea heshima Spika inayofanywa na CHADEMA ni mtaji wa kisiasa kwa CUF.

Ushauri: CHADEMA ijiepushe na tabia za mipasho mbele ya TBC mkiwa Bungeni. Sugu apewe mafunzo maaluma ya kuchagua maneno ya kuongea Bungeni – itafaa zaidi iwapo hotuba zake zitapitiwa na Mnyika kabla hajazisoma.


Addendum:

.....Wewe unapaswa kufa kabisa.
Watanzania wengi wanakuombea ufe....

wengi tunakuombea usiku na mchana ufe tujue tumedondosha msaliti mmoja

Rais Kikwete aliposema kuna watu wamemuombea AFE kuna watu hawakuamini.

Sasa haya mnayoandika hapa yanadhihirisha kuwa kweli watu wa namna hiyo mpo.

Hizi ni hulka mpya kabisa mnazozileta vijana wa bavicha kwenye siasa!!!

Inasikitisha sana kwa sababu lengo la kunzishwa kwa bavicha na jinsi ilipo sasa na inakoelekea ni tofauti kabisa.
Bavicha siku hizi inatumiwa kama organ ya kuwasababishia watu vifo - INASIKITISHA...
 
Ni vizuri umefahamu kuwa siasa za Tanzania ya leo zinahusisha CUF na CHADEMA pekee hivyo CCM imeshajifia. Hongera sana kwani sasa umeanza kuona mwanga kwani ulikuwa kipofu haswaaa.
 
unabweka kama jibwa lilopewa bangi mbona umeshindwa mkanda uliouandaa na akina mwigulu umebuma huna msaada kwa nchi hii wengi tunakuombea usiku na mchana ufe tujue tumedondosha msaliti mmoja njia
lete mada za maana sio chadema kila siku ukingojea mkono undondoke kama fisi
Kikwete alihongwa suti pair sita amemega pande la nchi amempatia Brigedia Ali akiua wanayama wa kila aina akitumbua hata mimba za wanyama kupelekea watoto wa mfalme dubai wakati watoto wakimasai wakitanga tanga hujadili hayo wewe na chadema kwa sababu ikiwepo mwaka 2015 usalama wa taifa watakupoteza kuondoa ushaidi

NNyamongo wananchi wanababuka midomo mifugo inakufamimea haioti kwa ajili ya sumu barrick wanamimina kwenye mito hata mirahaba na kodi haijakusantwa wewe husemi uko na chadema ambayo imekuinua wewe na familia yako mukahamia mjini na kuacha kupaa dagaa

Bagamoyo imeuzwa kwa wachina kwa sababu ya kuwahonga kama jason alivyosema kwa kumuokoa mtto wa kikwete Ridhiwani mfanya biashara ya madawa ya kulevya hayo huyaleti tujadili kujua mkataba ukoje ili tuokoe kizazi hiki na kijacho wewe na chadema iliyokutoa mpaka usalama wa taifa wakakuona mtu wakutumika

Tangu Kinana awe katibu mkuu tembe asilimia 42 amekuwa wakiuliwa kwa kasi hutaki achunguzwe ili kulinda wanyama wetu kwa kizazi hiki na kijacho wewe na chadema ili uimalize kwa sababu unajua safari yako ya kisiasa imeisha kutokana na kujikoroga
Asilimia 62 ya watoto wamefeli na hii ni mlolong wa miaka mitano mfululizo huongei kitu uko na chadema inayokupa tija kwenye jamii kuonekana n muana siasa
Wananchi wanakula mlo mmoja,mitaani watoto wamejaa wakati wakikwete wakivimbiwa ikulu kwa fedha za wala jasho hayo husemi
huna hoja wewe , na nina imani wana JF wanajua mission yako ambayo imeabort umejifix mwenyewe na huta inuka
 
Ni vizuri umefahamu kuwa siasa za tanzania ya leo zinahusisha cuf na cdm pekee hivyo ccm imeshajifia. Hongera sana kwani sasa umeanza kuona mwanga kwani ulikuwa kipofu haswaaa.

Ni vema kusoma thread na kuelewa kabla ya kujibu.
Usiwe kama Sugu.
 
unabweka kama jibwa lilopewa bangi mbona umeshindwa mkanda uliouandaa na akina mwigulu umebuma huna msaada kwa nchi hii wengi tunakuombea usiku na mchana ufe tujue tumedondosha msaliti mmoja

Hizi hulka za kuombeana kufa sio za kitanzania. Inasikitisha kuona siku za karibuni vijana wa bavicha mmeingiwa na shetani anayewachochea muwe na hulka za namna hii katika siasa!!!

Ushauri: Kama lengo ni kujenga nchi, hakuna sababu ya kuombeana vifo. Tamaa ya madaraka itawafanya maadui wa nchi yetu wawatumie kuiharibu nchi. Kuweni makini vijana wa bavicha.
 
Sina shaka na upeo wa kamanda ZeMarcopolo bali najua ni uchovu na usingizi ndio uliopelekea mpaka kutema pumba hizi.
 
Last edited by a moderator:
Hizi hulka za kuombeana kufa sio za kitanzania. Inasikitisha kuona siku za karibuni vijana wa bavicha mmeingiwa na shetani anayewachochea muwe na hulka za namna hii katika siasa!!!

Ushauri: Kama lengo ni kujenga nchi, hakuna sababu ya kuombeana vifo. Tamaa ya madaraka itawafanya maadui wa nchi yetu wawatumie kuiharibu nchi. Kuweni makini vijana wa bavicha.


Wewe unapaswa kufa kabisa kwenye nchii hii kwa sababu hakuna nchi unajenga watu wamekatwa mikono wakachomewa nyumba wakavunjwa miguu,wakapigwa risasi,wakafurumishwa matumbo wakitaka mabadiriko wewe kwa kalamu yako na nyanja yako kuwa kwenye siasa unavuruga mstakbali wa demokrasia huru, unapenda sana kuisema bavicha na kuunganisha wana jf na bavicha au chadema kwa sababu ndio hila zako na mission zako unachotaka kwa sababu unakaa kwenye vikao vyenu unakuja hapa kushusha juhudi za chama chako huna aibu ,hupaswi kuishi msaliti mkubwa
Trend ya post zako hazijawahi kuwa za kujenga nchi ni zakukandamiza demokrasia
unahasira sana na bavicha ulitoa gari ili uweze kuwacontrol umeshindwa gari wanatumia na umiliki wa bavicha umeyeyuka ulidhani utakuwa ridhiwani anavyotawala uvccm umekaushiwa mission imekwenda na maji ya mafuriko umehonga viongozi wa bavicha eti millioni tano, ulidhani zitawazuzua ukiwa tanga eti kilimo cha mkonge hujaongea tena kuhusu mkonge mission ya kuhonga ilivoshindwa
Watanzania wengi wanakuombea ufe kiongozi wewe wa chama chako unachokiasi ili hesabu isiwepo ya kwako wakati huna mssada zaidi ya kubomoa
lete mada hapa za mikataba ya wachina 17 tujadili badala ya kila siku unataka tujadili chadema umeambiwa hapa ni baraza la wadhamini la chadema unabore
 
Wewe unapaswa kufa kabisa kwenye nchii hii kwa sababu hakuna nchi unajenga watu wamekatwa mikono wakachomewa nyumba wakavunjwa miguu,wakapigwa risasi,wakafurumishwa matumbo wakitaka mabadiriko wewe kwa kalamu yako na nyanja yako kuwa kwenye siasa unavuruga mstakbali wa demokrasia huru, unapenda sana kuisema bavicha na kuunganisha wana jf na bavicha au chadema kwa sababu ndio hila zako na mission zako unachotaka kwa sababu unakaa kwenye vikao vyenu unakuja hapa kushusha juhudi za chama chako huna aibu ,hupaswi kuishi msaliti mkubwa
Trend ya post zako hazijawahi kuwa za kujenga nchi ni zakukandamiza demokrasia
unahasira sana na bavicha ulitoa gari ili uweze kuwacontrol umeshindwa gari wanatumia na umiliki wa bavicha umeyeyuka ulidhani utakuwa ridhiwani anavyotawala uvccm umekaushiwa mission imekwenda na maji ya mafuriko umehonga viongozi wa bavicha eti millioni tano, ulidhani zitawazuzua ukiwa tanga eti kilimo cha mkonge hujaongea tena kuhusu mkonge mission ya kuhonga ilivoshindwa
Watanzania wengi wanakuombea ufe kiongozi wewe wa chama chako unachokiasi ili hesabu isiwepo ya kwako wakati huna mssada zaidi ya kubomoa
lete mada hapa za mikataba ya wachina 17 tujadili badala ya kila siku unataka tujadili chadema umeambiwa hapa ni baraza la wadhamini la chadema unabore

Hii inaitwa Paranoia. Sio kosa lako...
 
Nadhani unachotaka kusema ni kuwa unatamani ingekuwa hivyo, kumbuka wananchi hawachagui chama wakati wa uchaguzi bali wanaanza na vyama tangu mapema vinapokuwa bungeni na katika majimbo yao, hao Cuf unaowasema hawajafa, wapo bungeni na hakuna anayewazuia kujenga hoja lakini niambie ni hoja gani za maana zinajengwa na Cuf? wamezidiwa hata na NccR!
 
Hizi hulka za kuombeana kufa sio za kitanzania. Inasikitisha kuona siku za karibuni vijana wa bavicha mmeingiwa na shetani anayewachochea muwe na hulka za namna hii katika siasa!!!

Ushauri: Kama lengo ni kujenga nchi, hakuna sababu ya kuombeana vifo. Tamaa ya madaraka itawafanya maadui wa nchi yetu wawatumie kuiharibu nchi. Kuweni makini vijana wa bavicha.

Ni sawa na CCM wanavyosema CHADEMA kifikia mwaka 2015 kitakuwa kimekufa, si ni sawa tu na mawazo ya huyu bwana kwani tofauti iko wapi hapo
 
Wewe ndio wakuambia watu waelewe thread? Maana kila threaad jibu lako ni Dr slaa!
Hebu onesha mfano kwanza na wenzio wafate!

Ni vema kusoma thread na kuelewa kabla ya kujibu.
Usiwe kama Sugu.
 
Sasa tangia lini kukawa na utofauti kati ya CUF na CCM? Yani ulitaka tuwape CCM-b uongozi?
 
Naunga mkono hoja. 2015 CHADEMA kikichukua dola CUF kitakuwa chama kiikuu cha upinzani. CCM itaanguka vibaya hivyo haitaweza kuwa chama kikuu cha upinzani. Kutatokea METAMORPHIC CHANGES zitakazoigeuza ndoa ya CCM na CUF ambapo CUF itageuka kuwa baba na CCM kuwa mama.
 
CHADEMA imechoka kiasi kwamba Mh. Sugu anachangia pumba bungeni na Mh. Nassari yeye hajui umuhimu wa Nyuki, kwa kweli 2015 CUF njia nyeupe kwao ya kuwa chama kikuu cha upinzani.
 
ZeMarcopolo Nadhani UNAJIFUNZA SIASA... Haujui kuwa CUF ndio iliyoanza kuwa CHAMA CHA UPINZANI cha kwanza Halafu CHADEMA 2015 ndio Mara yake ya KWANZA?

HIVI Unaandika HOJA HIZI kiushabiki au KIUNAFIKI???
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom