Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
TAMKO LA KAMATI KUU YA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) KUHUSU KUUNDWA KWA KAMATI YA RAIS YA UCHUNGUZI WA SHERIA NA MIKATABA YA MADINI.
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Kikao chake cha Dharura kilichofanyika Keys Hotel, Dar es Salaam leo hii tarehe 24 Novemba 2007, imejadili na kutafakari kwa kina uamuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuunda Kamati ya Rais ya Uchunguzi wa Sheria na Mikataba ya Madini na uteuzi wa Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe(Mbunge) kama mjumbe wa kamati hiyo na kufikia maazimio yafuatayo:
1. Kamati Kuu inamtaka Rais asitishe na/au kufuta uteuzi wa wajumbe wa Kamati hiyo ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi na/au kwa kuwa na mgongano wa maslahi;
2. Kamati Kuu inamtaka Rais atimize ahadi yake ya kuipa Kamati "uwakilishi mpana zaidi" kwa kuteua wawakilishi wa taasisi zisizokuwa za kiserikali ,mashirika ya dini na taasisi za kitaaluma kama wajumbe katika kamati hiyo;
3. Kamati Kuu inamshauri Rais aongeze masuala yafuatayo kwa ajili ya kuchunguzwa na Kamati katika hadidu za rejea za Kamati:
(i) Tuhuma za ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi wa wananchi waishio katika maeneo yenye migodi mikubwa ya madini;
(ii) Tuhuma za kuwepo kwa uchafuzi wa mazingira unaotishia afya za wananchi, viumbe hai na rasilimali za maeneo yenye migodi mikubwa ya madini kutokana na shughuli za uchimbaji unaofanywa na makampuni makubwa ya madini nchini;
(iii) Tuhuma za ufisadi na/au rushwa zinazohusiana na uandaaji na/au upitishwaji wa mikataba ya madini kati ya makampuni makubwa ya madini na viongozi na/au watendaji wa ngazi za juu wa serikali;
(iv) Mchango wa sekta ya madini kwa uchumi na maendeleo ya jamii ya wananchi waishio kwenye maeneo yenye migodi mikubwa ya madini.
4. Kamati Kuu inamtaka Rais kutoa hadharani na/au kwa wawakilishi wa kuchaguliwa wa wananchi Ripoti za Kamati za Uchunguzi zilizokwisha kuundwa na serikali kuchunguza matatizo mbalimbali ya madini ikiwemo Kamati ya Jenerali Mboma (2001), Kamati ya Brigedia Jenerali Mang'enya (2003), Kamati ya Dr. Kipokola (2004) na Kamati ya Masha (2006), ili wananchi wafahamu matokeo na mapendekezo ya Kamati hizo;
5. Kamati kuu inamtaka rais kuelekeza kwamba mikataba yote ya madini iliyoingiwa kati ya serikali na makampuni ya madini itolewe hadharani ili wananchi na wawakilishi wao wa kuchaguliwa waweze kufahamu yaliyomo katika mikataba hiyo;
6. Kamati Kuu inaridhia uteuzi na ushiriki wa Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe katika Kamati ya Rais ya Uchunguzi wa Sheria na Mikataba ya Madini na inaahidi kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa majukumu ya kamati hiyo;
7. Kamati Kuu inamtaka Rais atoe ahadi kwa Watanzania kwamba serikali yake itaitoa Ripoti ya Kamati ya Rais ya Uchunguzi wa Sheria na Mikataba ya Madini na kuyafanyia kazi mapendekezo yake;
8. Kamati Kuu inaagiza Sekretariati ya Makao Makuu ya Chama Taifa kuhakikisha kwamba Tamko hili linasambazwa kwa wananchi wa Tanzania kupitia vyombo vya habari na nakala zake kusambazwa katika ngazi zote za chama.
TAMKO HILI limetolewa kwa pamoja na Wajumbe wa Kamati Kuu na kusainiwa na Mwenyekiti wa Chama Taifa na Katibu Mkuu hapa Dar es Salaam leo hii tarehe 24 Novemba , 2007.
------------------------------------------------- ----------------------------------------
Freeman Aikaeli Mbowe
MWENYEKITI
7. Kamati Kuu inamtaka Rais atoe ahadi kwa Watanzania kwamba serikali yake itaitoa Ripoti ya Kamati ya Rais ya Uchunguzi wa Sheria na Mikataba ya Madini na kuyafanyia kazi mapendekezo yake;
CCM they are worse, dirty and stink chama. However CHADEMA sound like high school girls who are recommend about wear make up in school. CHADEMA can't be trusted, neither CCM. We need a party with strong strategic plan, well educated candidates, and action party.
CCM they are worse, dirty and stink chama. However CHADEMA sound like high school girls who are recommend about wear make up in school. CHADEMA can't be trusted, neither CCM. We need a party with strong strategic plan, well educated candidates, and action party.
My take;CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeyapinga maazimio yote manane yaliyotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), yanayopinga muundo wa Kamati ya Rais ya Kuchunguza Mikataba ya Madini.
Msimamo huo wa CCM ulitangazwa kwa nyakati tofauti jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Kapteni John Chiligati na Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho tawala (UV-CCM, Amos Makala.
Uamuzi huo wa CCM unaendeleza malumbano ya miezi ya hivi karibuni kati ya vyama hivyo viwili, kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu uendeshaji wa serikali na maamuzi mbalimbali ya kiutendaji.
Kabla ya suala hili la kamati ya madini, viongozi wa juu wa CCM na Chadema wamekuwa wakilumbana kuhusu kashfa ya ubadhirifu wa fedha katika Benki Kuu (BoT), utiwaji wa saini wa mkataba wa Buzwagi na kabla ya hapo matamko mbalimbali ya viongozi wa Chadema yanayohusu uwezo wa serikali kiutendaji na maamuzi ya kisera na kisiasa serikalini.
Katika suala hili la sasa, Chiligati ambaye alizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alisema ni jambo la ajabu kwamba Chadema waliupokea vibaya uamuzi wa Rais Kikwete kuunda kamati hiyo ya madini, hali ambayo ilizaa malumbano miongoni mwa viongozi wa chama hicho cha upinzani.
Kwa mujibu wa Chiligati, mapokeo mabaya ya Chadema yalisababisha malumbano miongoni mwa chama hicho cha upinzani ambayo kwa kiwango kikubwa yalionyesha kushindwa kwao kuelewa dhamira ya rais kuunda kamati hiyo.
"Jambo la kusikitisha ni kwamba Chadema walipokea vibaya uteuzi huo Chama Cha Mapinduzi kinayaona maazimio hayo ya Chadema kama kushindwa kuelewa dhamira njema ya rais na mantiki ya kuunda kamati hiyo," alisema Chiligati. Akisoma tamko rasmi la chama hicho lenye kurasa nne, Chiligati alieleza kushangazwa na namna maazimio hayo ya Chadema yalivyoshindwa kutofautisha kuhusu haja ya kuundwa kwa tume au kamati ya madini.
"Ni vema ikaeleweka kuwa tume huundwa pale ambapo imethibitika kuwa kuna kosa lililotendeka au athari za wazi zimeonekana kwenye utendaji wa chombo cha serikali, lakini kamati huundwa pale ambapo mwelekeo mpya unahitajika katika utendaji wa chombo cha serikali,
"Tunapenda wananchi waelewe kuwa, alichounda rais ni kamati ya kuangalia upya sera, sheria na mikataba ya uchimbaji madini na si tume ya kuchunguza mikataba ya uchimbaji madini," alisema Chiligati akipinga pendekezo la chadema ambalo pamoja na mambo mengine lilitaka rais aunde tume badala ya kamati.
Mbali ya hilo, Chiligati katika tamko lake hilo alisema iwapo Chadema ilikuwa na mtazamo huo, basi walipaswa kumpa Kabwe Zitto ambaye ni mjumbe wa kamati, maoni yao kuhusu suala hilo badala ya kukimbilia kwenye vyombo vya habari.
Akizungumzia suala la kumtaka Rais Kikwete kufuta uteuzi wa baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, Chiligati alisema madai hayo ni sawa na mbio za sakafuni ambazo lazima zitaishia ukingoni, na kuwa Chadema wanapaswa kuelewa kuwa uteuzi wa rais haufanywi kwa shinikizo la mtu wala taasisi yoyote.
"Hakuna migongano ya kimasilahi baina ya mjumbe yeyote wa kamati na kamati yenyewe na tuhuma za ufisadi dhidi ya baadhi ya wajumbe walioteuliwa hazina uthibitisho wowote na kuwa ni hisia binafsi za uongozi wa chama hicho," alisema.
Alisema Watanzania wanapaswa kufahamu kazi za kamati ambazo miongoni mwake ni pamoja na kupitia mikataba yote ya madini na nyaraka nyingine zinazohusu migodi mikubwa na kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta hiyo.
Kazi nyingine ni kupitia mifumo ya usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali kuchambua na kuainisha haki na wajibu wa mwekezaji na mwenye rasilimali ambaye ni serikali.
Alisema chama chake kinayaona maazimio hayo kuwa ni matokeo ya kushindwa kuendesha siasa zenye hoja ndani ya jamii ya Kitanzaniaa.
Wakati Chiligati akitoa maoni yake hayo, UVCCM nao walitoa tamko la kurasa mbili wakieleza kushangazwa kwao na maazimio hayo ya Chadema.
Taarifa ya UVCCM iliyotolewa na Makala iliyaelezea maazimio hayo ya Chadema kuwa yaliyojaa upotoshaji, dalili za kutapatapa, uzushi pamoja na ubinafsi na kuwa, hoja hizo zinalenga kudhoofisha jitihada za Rais Kikwete zenye lengo la kulinda rasilimali za nchi.
"UVCCM ina imani na wajumbe wa kamati na tuna imani kamati iliyoundwa itafanya kazi kwa uhuru na zaidi imejaa watu makini na wapenda maendeleo na masilahi ya taifa," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
CCM inatoa matamko hayo mawili tofauti siku moja tu baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, kutangaza maazimio manane kuhusu kamati hiyo ya kuchunguza mikataba ya madini.
Chadema katika maazimio yao hayo walimtaka rais afute uteuzi wa baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo ambao wanadaiwa kutuhumiwa kwa ufisadi huku wengine wao wakitajwa kuwa na mgongano wa kimasilahi.
Azimio jingine la chama hicho linamtaka rais kutimiza ahadi yake ya kutoa uwakilishi mpana zaidi kwa kuteua wajumbe wengine kutoka taasisi zisizokuwa za kiserikali (NG'Os), mashirika ya dini na taasisi za kitaaluma.
Chama hicho pia kilipendekeza kuongezwa kwa hadidu za rejea ambazo zilitakiwa kujumuisha masuala yanayohusu ukiukwaji wa haki za binadamu katika maeneo yenye migodi mikubwa ya madini na uchafuzi wa mazingira unaotishia afya za wananchi, viumbe hai na rasilimali katika maeneo hayo.
Kwa mujibu wa Chadema, hoja nyingine zinazotakiwa kufanyiwa kazi ni madai ya kuwapo kwa tuhuma za rushwa wakati wa uandaaji na uchapishaji wa mikataba ya madini kati ya kampuni kubwa za madini na viongozi au watendaji wa serikali.
Nyingine ni mchango wa sekta ya madini kwenye uchumi na maendeleo ya jamii ya wananchi waishio kwenye maeneo yenye migodi mikubwa ya madini.
Azimio jingine linamtaka rais kutoa hadharani ripoti ya kamati za uchunguzi zilizokwisha kuundwa na serikali kuchunguza matatizo mbalimbali yanayohusu sekta ya madini tangu mwaka 2001.
Azimio la tano linamtaka rais kuelekeza mikataba yote iliyoingiwa kati ya serikali na kampuni za madini kuwekwa hadharani, ili wananchi waweze kuelewa yaliyomo katika mikataba hiyo.
Azimio la sita ni kuridhia uteuzi na ushiriki wa Kabwe Zitto katika kamati hiyo ya rais na kuweka kipengele kinachoiagiza Kamati Kuu ya Chadema kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa majukumu ya Kamati ya Rais.
Azimio la saba linamtaka rais binafsi au kwa kupitia mwenyekiti wa kamati hiyo atoe ahadi kwa wananchi kuwa utekelezaji wa kamati na ripoti yake vitakuwa hadharani na kuwa ushauri wa kamati hiyo utafanyiwa kazi.
Azimio la mwisho limeiagiza sekretarieti ya chama hicho kusambaza tamko hilo nchi nzima kupitia vyombo vya habari na nakala zake kusambazwa katika ngazi zote za chama.
----------------------------------MWISHO------------------------------------------
Chadema Vs Ccm Nani Mbabaishaji? ...Chadema waongeze bidii na kuwa watu makini wengi zaidi, kama CCM ambayo leo unaweza kuwaondoa wote walioko kwenye uongozi na kuanza na wengine wapya na bado ukawa na timu tano zaidi...
Chadema Vs Ccm Nani Mbabaishaji?
Nafikiri wananchi wa Tanzania, walishaamua siku nyingi sasa kuhusiana na hili swali ambalo, sina uhakika kama ni valid argument, isipokuwa in case likiwa, then wananchi wameshajibu mara nyingi sana, kupitia kwenye kura za uchaguzi,
CCM ina miaka karibu 45 sasa, na Chadema ina miaka karibu 20 sasa, hivi kweli within miaka yote hiyo ya uhai wa Chadema, na CCM hili swali halijajibiwa? Kama ni mafisadi ni ishu ya sheria sio siasa it has nothing to do na CCM kwa ujumla,
Swali nafikiri hapa lilipaswa kuwa je Chadema, wanafanya kazi yao waliyopewa na wananchi toka waanzishe chama chao, ya kuisaidia serikali ya CCM katika kuvumbua mapungufu yao ili waweze kutawala vyema? Ukweli ni kwamba so far so good, Chadema wamekuwa wakijitahidi sana kuisaidia serikali ya CCM na hasa kuikumbusha mapungufu yake katika uongozi wake wa kutawala jamhuri, je Chadema inawea kuaminiwa kutawala jamhuri, wananchi wamesema hata udiwani hawawezi kuwaamini nao hii ni kutokana na majibu ya uchaguzi wa majuzi tu.
Heshima kwa Chadema, kwamba angalau wanajitahidi sana kuliko vyama vingine vya siasa huko upande wa pili nchini, na tunawatakia mafanikio mema huko kwenye sidelines, lakini kutawala jamhuri bado sana, maana hatuwezi kuwapa nchi Zitto, Slaaa, na Lisu tu no way, Freeman mpaka amalize shule ndio ajaribu ku-apply kwenye siasa zetu za taifa aliyoyasoma huko shuleni, kwa kweli hatuwezi ku-afford hayo ya experiment na taifa letu, Chadema waongeze bidii na kuwa watu makini wengi zaidi, kama CCM ambayo leo unaweza kuwaondoa wote walioko kwenye uongozi na kuanza na wengine wapya na bado ukawa na timu tano zaidi.
Kukosoa watawala, au kuwakumbusha watawala mapungufu yao, sio dhana ya kuweza kutawala, tumeyaona hayo wazi Kenya, Zambia, Malawi, Poland, na Ukraine.
Ahsanteni Wakuu!
Chadema Vs Ccm Nani Mbabaishaji?
Nafikiri wananchi wa Tanzania, walishaamua siku nyingi sasa kuhusiana na hili swali ambalo, sina uhakika kama ni valid argument, isipokuwa in case likiwa, then wananchi wameshajibu mara nyingi sana, kupitia kwenye kura za uchaguzi,
CCM ina miaka karibu 45 sasa, na Chadema ina miaka karibu 20 sasa, hivi kweli within miaka yote hiyo ya uhai wa Chadema, na CCM hili swali halijajibiwa? Kama ni mafisadi ni ishu ya sheria sio siasa it has nothing to do na CCM kwa ujumla,
Swali nafikiri hapa lilipaswa kuwa je Chadema, wanafanya kazi yao waliyopewa na wananchi toka waanzishe chama chao, ya kuisaidia serikali ya CCM katika kuvumbua mapungufu yao ili waweze kutawala vyema? Ukweli ni kwamba so far so good, Chadema wamekuwa wakijitahidi sana kuisaidia serikali ya CCM na hasa kuikumbusha mapungufu yake katika uongozi wake wa kutawala jamhuri, je Chadema inawea kuaminiwa kutawala jamhuri, wananchi wamesema hata udiwani hawawezi kuwaamini nao hii ni kutokana na majibu ya uchaguzi wa majuzi tu.
Heshima kwa Chadema, kwamba angalau wanajitahidi sana kuliko vyama vingine vya siasa huko upande wa pili nchini, na tunawatakia mafanikio mema huko kwenye sidelines, lakini kutawala jamhuri bado sana, maana hatuwezi kuwapa nchi Zitto, Slaaa, na Lisu tu no way, Freeman mpaka amalize shule ndio ajaribu ku-apply kwenye siasa zetu za taifa aliyoyasoma huko shuleni, kwa kweli hatuwezi ku-afford hayo ya experiment na taifa letu, Chadema waongeze bidii na kuwa watu makini wengi zaidi, kama CCM ambayo leo unaweza kuwaondoa wote walioko kwenye uongozi na kuanza na wengine wapya na bado ukawa na timu tano zaidi.
Kukosoa watawala, au kuwakumbusha watawala mapungufu yao, sio dhana ya kuweza kutawala, tumeyaona hayo wazi Kenya, Zambia, Malawi, Poland, na Ukraine.
Ahsanteni Wakuu!
Chadema Vs Ccm Nani Mbabaishaji?
Nafikiri wananchi wa Tanzania, walishaamua siku nyingi sasa kuhusiana na hili swali ambalo, sina uhakika kama ni valid argument, isipokuwa in case likiwa, then wananchi wameshajibu mara nyingi sana, kupitia kwenye kura za uchaguzi,
CCM ina miaka karibu 45 sasa, na Chadema ina miaka karibu 20 sasa, hivi kweli within miaka yote hiyo ya uhai wa Chadema, na CCM hili swali halijajibiwa? Kama ni mafisadi ni ishu ya sheria sio siasa it has nothing to do na CCM kwa ujumla,
Swali nafikiri hapa lilipaswa kuwa je Chadema, wanafanya kazi yao waliyopewa na wananchi toka waanzishe chama chao, ya kuisaidia serikali ya CCM katika kuvumbua mapungufu yao ili
waweze kutawala vyema? Ukweli ni kwamba so far so good, Chadema wamekuwa wakijitahidi sana kuisaidia serikali ya CCM na hasa kuikumbusha mapungufu yake katika uongozi wake wa kutawala jamhuri, je Chadema inawea kuaminiwa kutawala jamhuri, wananchi wamesema hata udiwani hawawezi kuwaamini nao hii ni kutokana na majibu ya uchaguzi wa majuzi tu.
Heshima kwa Chadema, kwamba angalau wanajitahidi sana kuliko vyama vingine vya siasa huko upande wa pili nchini, na tunawatakia mafanikio mema huko kwenye sidelines, lakini kutawala jamhuri bado sana, maana hatuwezi kuwapa nchi Zitto, Slaaa, na Lisu tu no way, Freeman mpaka amalize shule ndio ajaribu ku-apply kwenye siasa zetu za taifa aliyoyasoma huko shuleni, kwa kweli hatuwezi ku-afford hayo ya experiment na taifa letu, Chadema waongeze bidii na kuwa watu makini wengi zaidi, kama CCM ambayo leo unaweza kuwaondoa wote walioko kwenye uongozi na kuanza na wengine wapya na bado ukawa na timu tano zaidi.
Kukosoa watawala, au kuwakumbusha watawala mapungufu yao, sio dhana ya kuweza kutawala, tumeyaona hayo wazi Kenya, Zambia, Malawi, Poland, na Ukraine.
Ahsanteni Wakuu!
mkuu, kweli tumeona timu makini za ccm tangu izaliwe ambazo kwa umakini wao ndio maana kama nchi tupo tulipo leo. kweli safari bado ndeeefu
Heshima mkuu,
Unamaanisha nini ukisema tuko tulipo?
Yaani unamaanisha kwenye huduma bora za afya,miundombinu imara,ajira nje nje, hakuna ubabaishaji katika mfumo wetu wa elimu na vijana wetu vyuo vikuu wanasoma na wanapata elimu bora katika mazingira mazuri,hatuna kashfa za kijinga kama kwa nchi jirani za kifisadi, sarafu yetu inanguvu kubwa,hakuna watoto wa mitaani,machinga hawakandamizwi, kuna maadili ya kiuongozi,demokrasia imepanuka sana,hakuna ujambazi uliokithiri,mtoto wa tajiri na wa maskini anaweza kukaa sehemu moja bila kuona tofauti,kuna usimamizi mzuri wa raslimali zetu,na bajeti yetu haitegemei wahisani kwa asilimia kubwa kwani hilo haliwezekani kabisa na huwa tunalisikia kwa nji jirani tu.
Kweli tumeshuhudia watu makini ndani ya CCM hasa wanaosaini mikataba ya Madini mahotelini.Kweli hpo kulikua na umakini mkubwa kwani Lihoteli hilo lilikua na ulinzi mkali na mkataba huo ulikua nyeti sana
mkuu nisome vizuri. mimi nashangaa hizo timu makini kutuweka hapa tulipo. yaani hizo timu makini zimeshindwa kutukwamua na kutufikisha kwenye neema! oops nimesahau kwamba kapteni wa timu iliyopo hajui kiini cha matatizo yetu. ni mawazo tuu