Benson Mramba
JF-Expert Member
- Oct 29, 2013
- 766
- 1,884
Vikao vikuu vya Kikatiba vya CHADEMA 2016 viliazimia kuwa Uchaguzi wa Mwenyekiti Taifa ufanyike mwaka huu 2018 ili kutoa fursa kwa Chama kujiandaa na chaguzi za Serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 ila mpaka sasa hakuna dalili yoyote ya jambo hili kufanyika.
Azimio kama hili lilifanyika mwaka 2006 kuwa uchaguzi ufanyike 2008 ukafanyika 2009 na likarudiwa tena mwaka 2011 kuwa uchaguzi ufanyike 2013 lakini ukafanyika 2014.
Jambo ambalo ni wazi ni kuwa Mwenyekiti Freeman Mbowe amekuwa akitumia mbinu hii ya kutangaza tarehe ya mapema ili ya uchaguzi ili kutambua wapinzani wake, na mara akishawatambua huahirisha uchaguzi kwa mwaka mmoja kwa madai kuwa maandalizi hayakamilika na kuwa muda wake kikatiba haujaisha.
Katika muda huu wa nyongeza ndio huutumia kushughulika na timu pinzani hadi anaimaliza yote. Haya ndio yalimkuta Chacha Wangwe na Zitto Kabwe wakati huo kwa nyakati tofauti.
Ni vema sasa Taifa na Wana CHADEMA wakajulishwa ratiba kamili ya Uchaguzi wa CHADEMA na pia ni wakati muafaka kwa Mwenyekiti Mbowe kulitangazia Taifa kama anagombea tena ama la ili kufungua mjadala wa kitaifa ikiwa ni pamoja kuandaa mrithi wake.
Azimio kama hili lilifanyika mwaka 2006 kuwa uchaguzi ufanyike 2008 ukafanyika 2009 na likarudiwa tena mwaka 2011 kuwa uchaguzi ufanyike 2013 lakini ukafanyika 2014.
Jambo ambalo ni wazi ni kuwa Mwenyekiti Freeman Mbowe amekuwa akitumia mbinu hii ya kutangaza tarehe ya mapema ili ya uchaguzi ili kutambua wapinzani wake, na mara akishawatambua huahirisha uchaguzi kwa mwaka mmoja kwa madai kuwa maandalizi hayakamilika na kuwa muda wake kikatiba haujaisha.
Katika muda huu wa nyongeza ndio huutumia kushughulika na timu pinzani hadi anaimaliza yote. Haya ndio yalimkuta Chacha Wangwe na Zitto Kabwe wakati huo kwa nyakati tofauti.
Ni vema sasa Taifa na Wana CHADEMA wakajulishwa ratiba kamili ya Uchaguzi wa CHADEMA na pia ni wakati muafaka kwa Mwenyekiti Mbowe kulitangazia Taifa kama anagombea tena ama la ili kufungua mjadala wa kitaifa ikiwa ni pamoja kuandaa mrithi wake.