CHADEMA tusiwapuuze hawa

CHADEMA tusiwapuuze hawa

Maziwafreshi

New Member
Joined
Feb 10, 2015
Posts
1
Reaction score
3
Nimekuwa msomaji na mfuatiliaji wa kawaida wa jukwaa hili lakini leo nimeamua kuzama mzimzima baada ya kuguswa na hoja kadhaa ambazo si nzuri kwa mstakabari wa mabadiliko tunayoyapigania.

Juzi kulikuwa na makala moja hapa yenye kichwa “CHADEMA ISIPOTOA TAMKO HILI LITATUGHARIMU UCHAGUZI UJAO” ambayo kimsingi iligusa mtaa wangu kwani mimi pia naishi mtaa huo wa Nyasaka B, na nyingine iliyosema “CHADEMA TOENI SEMINA ELEKEZI KWA WENYEVITI WA MITAA” ambazo zote zilichangiwa kishabiki bila kujali hoja husika.

Kwanza nikiri kuwa makala ile iliwakilisha kilio cha wengi na pia siyo kweli kuwa ukikosoa jambo unaloona aliendi sawa na matarajio yako kwa chama basi wewe ni CCM, au una chuki na kiongozi hapana. Busara ni kufanya utafiti na kutoa majibu kulingana hoja husika lakini wengi badala ya kujadili hoja wanakuja na personal attack.

Wananchi wanataka kuona utofauti wa CHADEMA na CCM ili kujenga imani zaidi wala siyo kufanya yaleyale au zaidi ya CCM kisa eti mbona nao walifanya hivyo. Hapo tutapotea njia!!

Mfano mtu anapotaka Wenyeviti wa mitaa wapewe semina elekezi anakuwa na nia nzuri kwani siyo wote wanafahamu malengo ya chama, wengi waliingia CHADEMA baada kuangalia upepo unavumaje, ilikuwa ukigombea kupitia CHADEMA unapeta…sasa hivi lengo ni moja tu kudelete kabisa CCM hivyo hatuchagui mtu bali chama.

Nilisikitika sana niliposikia kauli hizi... “Nani kakuambia kuwa hao wenyeviti wa Sisiem waliopigwa chini, walikuwa hawachukui 10% kamisheni? Tena nikusahisishe kidogo, hao wenyeviti wa magamba, walikuwa wanajimegea more than 10% commission” AU “Tupe idadi ya idadi ya askari polisi wanaofanya kazi katika jiji la mwanza Ili tujadili Kama askari wanatosha kutoa ulinzi kwa kila mkaazi wa jiji la mwanza?, msipolima wenyewe barabara mnategemea nani awalimie..”

Yaani badala ya kutafuta namna ya kuboresha barabara zetu kupitia kamati za maendeleo ya kata (WDC) tumeona njia pekee ni kuwafanya walipa kodi matrekta? Badala ya ku- harmonize na vituo vya polisi vilivyo katika maeneo yetu, kuaangalia askari wanapangaje doria zao…ufumbuzi ni kukesha tukilinda mitaa yetu? Badala ya kusaidia wananchi wamiliki ardhi na kujenga nyumba zao,tunataka kulipwa 10%?

Hoja hapa ni je matendo hayo ni sahihi na ndo msimamo wa chama? Na je yanaweza kuchochea kuaminiwa zaidi na wananchi hata kutupa dhamana kubwa?

Tunataka viongozi wabunifu wanaoendana na falsafa ya mabadiliko. Polisi hawatoshi sawa, lakini je ni kweli kuwa maeneo yote ya nchi wananchi wanakesha kujilinda wenyewe? Rekodi za ulinzi wa aina hii zikoje uko nyuma? Wizi unaotokea mchana mbona hakuna zamu ofisi moja baada ya nyingine kulinda mitaa inayowazunguka? Michango hii inayotambulishwa na uongozi mpya inatofauti gani na kodi ya maendeleo tuliyokuwa tukilipa huko nyuma? Je, ni kweli kuwa baada ya kodi hizo kupigwa stop hakuna maendeleo?

Imani yangu ni kuwa humu wamo viongozi wa CHADEMA wanapitia kila post kama nilivyokuwa nikifanya mimi kabla ya leo, hivyo hapa ni sehemu sahihi kabisa wala hakuna haja ya kupanga foreni ofisi za kata, wilaya, mkoa hata taifa na kuacha kutafuta mkate wa kila siku.

Naomba tuache kuchangia ili kuonekana tumechangia “ni bora kukaa kimya na hata wakadhani u mjinga kuliko kuongea katika namna itakayothibitisha kuwa u mjinga”
 
Mkuu, umegonga utosini hakuna mchangiaji hapa, siwezi fukuza mke kwa ukorofi nikaoa mwingine akawa malaya nae nitamfukuza tu.
 
Maziwafreshi umeongea kashinambonyi (ukweli mtupu).

Kwa sehemu kubwa ulichoandika kinachangiwa na udhaifu mkubwa wa kiuongozi tulionao katika chama hasa kuanzia ngazi ya kanda kushuka mpaka kata. Katika mtaa wangu mimi hapa Mwanza mjini sikuwahi kumwona kiongozi hata mmoja wa kata akishiriki nasi uchaguzi serikali za mitaa (sijui ni mamluki au waliomba uongozi kuuza sura).
Mitaa na vijiji vingi hatuna kabisa uongozi wa chama na ndo maana uchaguzi wa serikali za mitaa maeneo mengi tulipigwa kirahisi sana na hata October mwaka huu Magamba watatushinda kirahisi tu.

Viongozi wa ngazi hizo nilizotaja wengi wao hawajatekeleza/hawatekelezi kwa ukamilifu na uaminifu mkakati wa Chadema ni Msingi; ambao ndiyo tool pekee tukiitumia tunaiondoa CCM. As a result tunaingia vitani very disorganized.
Mwisho wa siku tunabakia kushangilia mauzurio ya watu kwenye mikutano bila kuwa na idadi ya makisio ya kula tunazoweza kupata ngazi za mitaa na vijiji na zile tunazopata hatuna uhakika wa kuzilinda.

Haya kila nikiyatafakari nasononeka sana kwa sababu ni dhahiri tunaenda katika uchaguzi tukiwa tumeshashindwa. Kinachofanya tushindwe kinajuliakana ila hakuna hatua ZOZOTE zinachukuliwa kuweka mambo sawa.
NGUVU TUNAYO NA KURA ZA KUIONDOA CCM HAKIKA TUNAZO KAMA TUKIMUA KUJIOGANAIZI.
 
Wewe unaongea kama nani wakati wewe sisimizi tu ndani ya chadema kwanza unatumiwa na ccm.
 
Maziwafreshi umeongea kashinambonyi (ukweli mtupu).

Kwa sehemu kubwa ulichoandika kinachangiwa na udhaifu mkubwa wa kiuongozi tulionao katika chama hasa kuanzia ngazi ya kanda kushuka mpaka kata. Katika mtaa wangu mimi hapa Mwanza mjini sikuwahi kumwona kiongozi hata mmoja wa kata akishiriki nasi uchaguzi serikali za mitaa (sijui ni mamluki au waliomba uongozi kuuza sura).
Mitaa na vijiji vingi hatuna kabisa uongozi wa chama na ndo maana uchaguzi wa serikali za mitaa maeneo mengi tulipigwa kirahisi sana na hata October mwaka huu Magamba watatushinda kirahisi tu.

Viongozi wa ngazi hizo nilizotaja wengi wao hawajatekeleza/hawatekelezi kwa ukamilifu na uaminifu mkakati wa Chadema ni Msingi; ambao ndiyo tool pekee tukiitumia tunaiondoa CCM. As a result tunaingia vitani very disorganized.
Mwisho wa siku tunabakia kushangilia mauzurio ya watu kwenye mikutano bila kuwa na idadi ya makisio ya kula tunazoweza kupata ngazi za mitaa na vijiji na zile tunazopata hatuna uhakika wa kuzilinda.

Haya kila nikiyatafakari nasononeka sana kwa sababu ni dhahiri tunaenda katika uchaguzi tukiwa tumeshashindwa. Kinachofanya tushindwe kinajuliakana ila hakuna hatua ZOZOTE zinachukuliwa kuweka mambo sawa.
NGUVU TUNAYO NA KURA ZA KUIONDOA CCM HAKIKA TUNAZO KAMA TUKIMUA KUJIOGANAIZI.
Nyie ni vibaraka mnatumika na ccm kuja kuandika utumno wenu hapa.
 
...NADHANI cdm watatoa semina elekezi haraka.
 
Wewe unaongea kama nani wakati wewe sisimizi tu ndani ya chadema kwanza unatumiwa na ccm.

hii hatari sna kama mtu unaweza kuangalia ni nani anayezungumza badala ya kuja na hoja ya utaifa mbele tutakufa kibudu cc wa afrika bwana hatuwez kupigania utaifa wetu ni ma classes tu yamejaa.
 
CHADEMA na UKAWA iongeze kazi kwenye Capacity building kwenye grass root ... CCM must go ...
 
Tatizo kubwa ni kuwa chama hakina rasilimali fedha za kutosha hivyo viongozi wa chini wanakosa motivation.
 
Maziwafreshi umeongea kashinambonyi (ukweli mtupu).

Kwa sehemu kubwa ulichoandika kinachangiwa na udhaifu mkubwa wa kiuongozi tulionao katika chama hasa kuanzia ngazi ya kanda kushuka mpaka kata. Katika mtaa wangu mimi hapa Mwanza mjini sikuwahi kumwona kiongozi hata mmoja wa kata akishiriki nasi uchaguzi serikali za mitaa (sijui ni mamluki au waliomba uongozi kuuza sura).
Mitaa na vijiji vingi hatuna kabisa uongozi wa chama na ndo maana uchaguzi wa serikali za mitaa maeneo mengi tulipigwa kirahisi sana na hata October mwaka huu Magamba watatushinda kirahisi tu.

Viongozi wa ngazi hizo nilizotaja wengi wao hawajatekeleza/hawatekelezi kwa ukamilifu na uaminifu mkakati wa Chadema ni Msingi; ambao ndiyo tool pekee tukiitumia tunaiondoa CCM. As a result tunaingia vitani very disorganized.
Mwisho wa siku tunabakia kushangilia mauzurio ya watu kwenye mikutano bila kuwa na idadi ya makisio ya kula tunazoweza kupata ngazi za mitaa na vijiji na zile tunazopata hatuna uhakika wa kuzilinda.

Haya kila nikiyatafakari nasononeka sana kwa sababu ni dhahiri tunaenda katika uchaguzi tukiwa tumeshashindwa. Kinachofanya tushindwe kinajuliakana ila hakuna hatua ZOZOTE zinachukuliwa kuweka mambo sawa.
NGUVU TUNAYO NA KURA ZA KUIONDOA CCM HAKIKA TUNAZO KAMA TUKIMUA KUJIOGANAIZI.
No need to beat around the bush,viongozi wa ngazi za chini hawako motivated kihivyo katakana na mgawanyo usio na usawa wa rasilimali za chama.Hivi unajisikiaje unapowaona viongozi wako wa ngazi wa juu wakilipana posho na malipo mengine mengi yanayokaribia mamilioni ya pesa huku nyinyi wa huku chini mkiambiwa mkitumikie chama kwa kujitolea yaani bila malipo?Ukiangalia na hali ya maisha ilivyo na wewe una ndoto zako za kimaisha hivi wakitokea CCM na fungu zuri la fedha wakakutaka uhujumu chama kwenye uchaguzi hujakubali?Kama CHADEMA inataka kuwa na loyal and devoted army basi ni budi waangalie upya Kwenye masuala ya malipo,kama suala ni kukitumikia chama kwa kujitolea basi ni vizuri viongozi wa juu wakaonyesha mfano ili kujenga uamini kwa hawa viongozi wa chini,la sivyo wasaliti watazaliwa kila siku na mtawafukuza kila siku,sasa sijui mtawafukuza wangapi.Ni vyema kikatafutwa chanzo cha hili tatizo kwanza halafu kitafutiwe ufumbuzi haraka badala ya kuhangaika na matokeo.
 
No need to beat around the bush,viongozi wa ngazi za chini hawako motivated kihivyo katakana na mgawanyo usio na usawa wa rasilimali za chama.Hivi unajisikiaje unapowaona viongozi wako wa ngazi wa juu wakilipana posho na malipo mengine mengi yanayokaribia mamilioni ya pesa huku nyinyi wa huku chini mkiambiwa mkitumikie chama kwa kujitolea yaani bila malipo?Ukiangalia na hali ya maisha ilivyo na wewe una ndoto zako za kimaisha hivi wakitokea CCM na fungu zuri la fedha wakakutaka uhujumu chama kwenye uchaguzi hujakubali?Kama CHADEMA inataka kuwa na loyal and devoted army basi ni budi waangalie upya Kwenye masuala ya malipo,kama suala ni kukitumikia chama kwa kujitolea basi ni vizuri viongozi wa juu wakaonyesha mfano ili kujenga uamini kwa hawa viongozi wa chini,la sivyo wasaliti watazaliwa kila siku na mtawafukuza kila siku,sasa sijui mtawafukuza wangapi.Ni vyema kikatafutwa chanzo cha hili tatizo kwanza halafu kitafutiwe ufumbuzi haraka badala ya kuhangaika na matokeo.

Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa sana hasa kwenye hili swala la malipo. Nimeishi Songea viongozi wa ngazi ya mkoa wanaishi kwa kuomba omba. Pia nimeishi Dodoma hali ni hiyo hiyo.

Lakini kwani kiongozi akikihujumu chama kwa sababu tu hajalipya ndo anakuwa kakisaidiaje chama?? Hivi kweli kiongozi wa namna hii ana uelewa na nia ya dhati ya kufanikisha mageuzi katika hii nchi??

Na hayo malipo wanayopewa na CCM ili kuhujumu upinzani hivi huwa ni hela ya kula siku ngapi hasa!!??
Kuna watu hawako makini tu na hii ya malipo haiwezi kuwa sababu pekee ya watu kuharibu chama. Ni mtu mwenye tabia ya umamluki tu ndo anaweza kujiingiza katika vitendo vya kiharamia dhidi ya chama. Wapo baadhi ya viongozi na wanachama ngazi hizo za chini hawalipwi na yeyote lakini wanapigania mageuzi kwa moyo wa dhati kabisa na mimi ugomvi wangu ni dhidi ya viongozi wanaotuhujumu bila kujali wanaleta sababu yoyote ile kutuhujumu.

By the way CHADEMA haijawahi kuzuia viongozi wa chini kuanzisha vyazo zaidi vya mapato kwa chama ambayo nadhani yangesaidia sana kupata gharama za kuendeshea ofisi na malipo kwa viongozi wa ngazi husika. Hii ingepunguza kulilia hela ya ruzuku na kila mtu kutaka hii ruzuku ndo ifanye kila kitu. Kwanza ruzuku yenyewe ni shilingi ngapi hata itoshe kugharamia shughuli zote za chama nchi nzima?? CCM wenyewe na mahela yote ya ruzuku na vyanzo lukuki vya mapato bado hawana uwezo wa kukigharamia chama chao kwa kila kitu.

Viongozi lazima wawe wabunifu na pia wasiache kukomaa hiyo ruzuku walau kiduchu ifike na ngazi za chini kusaidia shughuri za chama. CHADEMA makao makuu hili la ruzuku lilishalalamikiwa sana na nyie mnajifanya mawe sana. Hili ni tatizo kwa chama makao makuu.
 
Maziwafresh hoja uliyoleta jukwaani ina mashiko kwa ustawi na maendeleo ya chama chetu CHADEMA.ni lazima wananchi waone tofauti ya utawala wa CHAMA CHAKAVU (CCM) na chama tumaini la watanzania (CHADEMA).Kama viongozi waliochaguliwa kwa imani kubwa na watanzania watafanya mambo mabaya kama ya viongozi waliopita wa CCM,wananchi watakata tamaa,kisha litafuata pigo kubwa la chama pendwa,chama tumaini la watanzania (CHADEMA) kitaanguka kwa kishindo kikubwa kwenye uchaguzi mkuu ujao.Hapo tutaanza kumtafuta mchawi na wala hatutampata kisha kwa masikitiko makubwa chama chetu kitaparaganyika "EE MUNGU MWENYEZI NAOMBA HILO LISITOKEE KWA CHAMA CHETU PENDWA CHADEMA".Ila kuzuia hayo yasitokee,kila aliyepata heshima ya kuchaguliwa na wananchi atekeleze wajibu wake kwa uadilifu."MUNGU IBARIKI TANZANIA,MUNGU IBARIKI CHADEMA"
 
Maziwafreshi umeongea kashinambonyi (ukweli mtupu).

Kwa sehemu kubwa ulichoandika kinachangiwa na udhaifu mkubwa wa kiuongozi tulionao katika chama hasa kuanzia ngazi ya kanda kushuka mpaka kata. Katika mtaa wangu mimi hapa Mwanza mjini sikuwahi kumwona kiongozi hata mmoja wa kata akishiriki nasi uchaguzi serikali za mitaa (sijui ni mamluki au waliomba uongozi kuuza sura).
Mitaa na vijiji vingi hatuna kabisa uongozi wa chama na ndo maana uchaguzi wa serikali za mitaa maeneo mengi tulipigwa kirahisi sana na hata October mwaka huu Magamba watatushinda kirahisi tu.

Viongozi wa ngazi hizo nilizotaja wengi wao hawajatekeleza/hawatekelezi kwa ukamilifu na uaminifu mkakati wa Chadema ni Msingi; ambao ndiyo tool pekee tukiitumia tunaiondoa CCM. As a result tunaingia vitani very disorganized.
Mwisho wa siku tunabakia kushangilia mauzurio ya watu kwenye mikutano bila kuwa na idadi ya makisio ya kula tunazoweza kupata ngazi za mitaa na vijiji na zile tunazopata hatuna uhakika wa kuzilinda.

Haya kila nikiyatafakari nasononeka sana kwa sababu ni dhahiri tunaenda katika uchaguzi tukiwa tumeshashindwa. Kinachofanya tushindwe kinajuliakana ila hakuna hatua ZOZOTE zinachukuliwa kuweka mambo sawa.
NGUVU TUNAYO NA KURA ZA KUIONDOA CCM HAKIKA TUNAZO KAMA TUKIMUA KUJIOGANAIZI.
Una hoja ya Msingi sana kuna baadhi ya Maeneo Pamoja na uwapo wa Changamoto lukuki uwajibikaji umekuwa msamiti,

Kuna Viongozi ambao ni Mizigo hawaendani na kasi na mahitaji ya Chama na hili lipo wazi rejea Matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
 
Binafsi naona chadema wanafanana mengi tu na upande wa pili yaani ccm. Ukishauri unaambiwa wewe ni kibaraka wa ccm. Kwa mfano tumeshauri mara nyingi kwamba chama kianzishe media zake kama redio, magazeti na hata tv, lakini tangu mwaka 2011 hakuna kinachotendeka. Pia tumeshauri chama kiwe na mpango mkakati wa kujitanua na kujiimarisha hasa maeneo ya vijijini, lakini viongozi wengi wa cdm hasa wabunge wako mijini wanakula bata tu, ccm itashinda kwenye uchaguzi wa mwaka huu kwa uzembe wa upinzani. Kusini mwa taifa letu kama ruvuma, lindi, njombe na hata iringa maeneo ya vijijini ccm imetaga. Cdm na ukawa wanasubiri mpaka wakati wa kampeni ndo waende. Kwa staili hii upinzani hauna malengo ya dhati ya kutwaa dola zaidi ya ulaghai.
 
Binafsi naona chadema wanafanana mengi tu na upande wa pili yaani ccm. Ukishauri unaambiwa wewe ni kibaraka wa ccm. Kwa mfano tumeshauri mara nyingi kwamba chama kianzishe media zake kama redio, magazeti na hata tv, lakini tangu mwaka 2011 hakuna kinachotendeka. Pia tumeshauri chama kiwe na mpango mkakati wa kujitanua na kujiimarisha hasa maeneo ya vijijini, lakini viongozi wengi wa cdm hasa wabunge wako mijini wanakula bata tu, ccm itashinda kwenye uchaguzi wa mwaka huu kwa uzembe wa upinzani. Kusini mwa taifa letu kama ruvuma, lindi, njombe na hata iringa maeneo ya vijijini ccm imetaga. Cdm na ukawa wanasubiri mpaka wakati wa kampeni ndo waende. Kwa staili hii upinzani hauna malengo ya dhati ya kutwaa dola zaidi ya ulaghai.
ccm sana hali mbaya hakuna uwezekano wa kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu.ccm kutegemea watashinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu ni sawa na kumpa mgonjwa uji wenye sumu ukitegemea atapona kumbe ndo atakufa.
 
ccm sana hali mbaya hakuna uwezekano wa kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu.ccm kutegemea watashinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu ni sawa na kumpa mgonjwa uji wenye sumu ukitegemea atapona kumbe ndo atakufa.
mkuu kwa vile unajifurahisha sawa, lakini kiukweli upinzani wanaingia kwenye uchaguzi huu huku wameshindwa, kuna maeneo hakuna upinzani, na kina mbowe, lipumba na wenzao wanatapa kwamba ccm itaondoka ikulu kwenye uchaguzi wa mwaka huu. Sijaona maandalizi ya dhati ya ukawa kuchukua nchi sijaona! Sijaona. Nenda maeneo mengi ya vijijini kwenye taifa letu utakubali nisemalo.
 
Back
Top Bottom