Elections 2010 CHADEMA stop the campaigns NOW!!!!

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Nimeweka title kali kidogo kwa sababu nataka kudraw attention ya wadau wa CHADEMA. Actually mi ni mdau wa CHADEMA na niko huku jimboni, bega kwa bega na mgombea ubunge tunapambana na mwanaccm mmoja.

Pamoja na umuhimu na juhudi tunazofanya katika kampeni zetu, naomba, timu za wagombea udiwani, ubunge, na rais, zifikirie kutoa muda (pengine kwa kusimamisha kampeni), na kujipanga jinsi ya kuzuia wizi wa kura. Nimegundua kuwa inaweza kuwa ni sawa na mtu unapita ukipanga miche bora, kumbe nyuma yako shetani anapita akizingoa na kupanda magugu. Mwisho wa siku ukigeuka nyuma huna kitu.

Yafuatayo (naamini yamefanyiwa kazi), naomba tuyape majibu yake

Tutahakikishaje kura zetu zinalindwa katika maeneo ambayo hamna wagombea ubunge na/au udiwani? Hii Tanzania ni kubwa aisee, tusi assume tu kuwa kuna watu watakuwa mawakala, CCM are very smart in that. Ni nani atakayepita na kuhakiki majina na idadi ya wapiga kura katika maeneo haya ya pembezoni yatakapobandikwa hizo cku 8 kabla ya uchaguzi? Yapo mengi ambayo inabidi tuyaangalie...

Naomba pamoja na mbinu nyingine, tuangalie kama hizi zitatusaidia; Kuweka mawakala zaidi ya mmoja kila kituo (kwa ticket ya vyama vingine vidogo vinavyoshiriki uchaguzi) ili kupunguza urahisi wa kununuliwa, kuanza kuunda timu za mawakala kila jimbo, na pengine Dr Slaa anapopita aseme sentensi chache kuwapa moyo na hamasa (ikiwezekana hata kukutana na baadhi yao wakati wa mapumziko), kuwasiliana na wagombea wote wa ubunge na kuwaelekeza namna ya kuomba kopi ya daftari la wapiga kura kwa maeneo yao, ili kulikagua na kujipanga kutokana na kila kituo kinavyoonekena (huku kwetu tunafanya juhudi, karibia tunalipata), wanaCHADEMA naomba muongeze mbinu hapa...
 
Tupo wote kwenye hilo lakini karata turufu ya CCM ni kuwanunua mawakala wa Chadema ili wasaini matokeo ya mezani badala ya kuhesabu kura.

Chadema wakiweza hilo basi ushindi hauna utata hata kidogo.
 
Yes. Insemekana wameshaandaa mabilioni kwa kazi hiyo. Hata hivyo inabidi tufanye kila linalowezekana kuifanya hiyo kazi ngumu. majimboni, waandaliwe wapiganaji wa kupita kila kituo kuangalia hali halisi siku ya kampeni (pikipiki inatosha kwa kazi hiyo). Camera (za kawaida au za simu), ziwepo standby, hasa yale maeneo korofi, kurekodi hali au tukio lolote linalotia mashaka

CHADEMA people, where are you? Toeni mbinu bw. saa nane naenda kwenye kikao cha kujipanga kwenye jimbo letu. Nipeni inputs za kwenda kudiscuss huko...
 
Tuko nakubaliana na wewe kwa asilimia kubwa, naongezea - CHADEMA iwekeze zaidi katika kuhakiki wapiga kura na kuhakikisha mawakala wao (wa uhakika) wanakuwepo katika vituo vyote (namaanisha katika majimbo yote) katika ile wiki ya uchaguzi hadi matokeo yanatangazwa. Ni vyema kuanza kudunduliza fedha sasa kwa ajili ya kuwawezesha mawakala. Gharama za mawakala nchi nzima ni kubwa kuliko tunavyodhani, hivyo ni vyema mipango ifanyike sasa. Watanzania wapenda maendeleo tutawachangia kwa kadri tutavyoweza.
 
Moja la nyongeza, hata kabla ya wakati wa kupiga kura kufika tumeisha habarishwa juu ya watu wanaotumwa kununua kadi za kupigia kura kwa wananchi. Hilo nalo ni muhimu sana kuliangalia katika kipindi hiki na pia kutafuta kujua hizo kadi za kupigia kura baada ya kununuliwa wanaozinunua watazitumiaje katika kuchakachua matokeo? Dr. Slaa na wagombea wengine iwe wa urais, ubunge na udiwani katika kampeni zao juu ya mbinu hiyoa na kuwashauri wananchi wasikubali kuuza vitambulisho vyao kwa sababu wakikamatwa watafunguliwa mashtaka na watakaopata shida ni wao. Wasidanganyike!
 
Ninaiunga mkono hoja. Mwaka 2000 nilishududia kwa macho yangu majulimsho ya Kura katika jimbo la Uchaguzi. Siku kura zilipojulimshwa na kwa mabishano makali, Prof. Lipumba alimzidi Mkapa kwa kura zaidi ya 500. lakini kesho asubuhi yalipobandikwa kwenye mbao za matangazo, Mkapa alimzidi Prof. Lipumba kwa zaidi ya kura 2000.

CHADEMA kama mnasikia, bila kuwa na Mpango-mkakati wa kulinda Kura, harakati zote zitakwenda na maji.
 
CHADEMA kama mnasikia, bila kuwa na Mpango-mkakati wa kulinda Kura, harakati zote zitakwenda na maji.
[/QUOTE]

Hili si la Chadema, ni la wapenda mageuzi wote. popote ulipo uwe tayari kuwa wakala, uwe tayari kulinda kura zisichakachuliwe. tukishirikiana tutawashangaza.
 
Nimeweka title kali kidogo kwa sababu nataka kudraw attention ya wadau wa CHADEMA. Actually mi ni mdau wa CHADEMA na niko huku jimboni, bega kwa bega na mgombea ubunge tunapambana na mwarabu mmoja.

Pamoja na umuhimu na juhudi tunazofanya katika kampeni zetu, naomba, timu za wagombea udiwani, ubunge, na rais, zifikirie kutoa muda (pengine kwa kusimamisha kampeni), na kujipanga jinsi ya kuzuia wizi wa kura. Nimegundua kuwa inaweza kuwa ni sawa na mtu unapita ukipanga miche bora, kumbe nyuma yako shetani anapita akizingoa na kupanda magugu. Mwisho wa siku ukigeuka nyuma huna kitu.

Yafuatayo (naamini yamefanyiwa kazi), naomba tuyape majibu yake

Tutahakikishaje kura zetu zinalindwa katika maeneo ambayo hamna wagombea ubunge na/au udiwani? Hii Tanzania ni kubwa aisee, tusi assume tu kuwa kuna watu watakuwa mawakala, CCM are very smart in that. Ni nani atakayepita na kuhakiki majina na idadi ya wapiga kura katika maeneo haya ya pembezoni yatakapobandikwa hizo cku 8 kabla ya uchaguzi? Yapo mengi ambayo inabidi tuyaangalie...

Naomba pamoja na mbinu nyingine, tuangalie kama hizi zitatusaidia; Kuweka mawakala zaidi ya mmoja kila kituo (kwa ticket ya vyama vingine vidogo vinavyoshiriki uchaguzi) ili kupunguza urahisi wa kununuliwa, kuanza kuunda timu za mawakala kila jimbo, na pengine Dr Slaa anapopita aseme sentensi chache kuwapa moyo na hamasa (ikiwezekana hata kukutana na baadhi yao wakati wa mapumziko), kuwasiliana na wagombea wote wa ubunge na kuwaelekeza namna ya kuomba kopi ya daftari la wapiga kura kwa maeneo yao, ili kulikagua na kujipanga kutokana na kila kituo kinavyoonekena (huku kwetu tunafanya juhudi, karibia tunalipata), wanaCHADEMA naomba muongeze mbinu hapa...

A very well written article and a genuine concern that need addressing.

Itabidi nimtafute mgombea wangu wa ubunge nijitolee kusaidia kwenye kituo changu
 
Mugo"The Great";1108786 said:
Ninaiunga mkono hoja. Mwaka 2000 nilishududia kwa macho yangu majulimsho ya Kura katika jimbo la Uchaguzi. Siku kura zilipojulimshwa na kwa mabishano makali, Prof. Lipumba alimzidi Mkapa kwa kura zaidi ya 500. lakini kesho asubuhi yalipobandikwa kwenye mbao za matangazo, Mkapa alimzidi Prof. Lipumba kwa zaidi ya kura 2000.

CHADEMA kama mnasikia, bila kuwa na Mpango-mkakati wa kulinda Kura, harakati zote zitakwenda na maji.


Kama unakwenda kwenye kikao wakumbushe wenzako kwamba CHADEMA ni ya wote kwa sasa hakikisheni kwamba;
  1. Ziundwe kamati za wakereketwa kwa majimbo yote bila kujali kuna wagombea udiwani na ubunge ktk jimbo husika, lengo ni kulinda kura za rais msiweke wa vyama tofauti.
  2. Kumbukeni kwa kila jimbo lazima wapo wanpenzi wa Dr.Slaa hata kama hakuna wagombea ubunge
  3. Leo asubuhi nimeongea na jamaa yangu yuko Ludewa anasema Dr.Slaa anao wapiga kura wengi lakini chadema hakijaweka wagombea ubunge na udiwani ni vema kupwapata wapenzi wa chadema ili walinde kura za slaa Ludewa.Chama kiwalipe posho na kuwapa ahadi pia baada ya ushindi-post election benefits
  4. Kwa kufanya hivyo lazima tutapata watu ambao hawatakubari kurubuniwa na hata wakiwepo ni wachache kwani watu wanataka mabadiliko.
  5. CHADEMA msipuuze hata jimbo moja msiangalie uwakilishi wa wabunge an diwani tu kwani Dr.Slaa anapendeka nchi nzima hasa Ludewa wanalalamika hamjawafikia
  6. WEKENI WAKALA KWA KILA JIMBO MKUBALI HASARA KWANI MANUFAA YATAFUTA HASARA HIYO.HUUU NI NUWEKEZAJI KWA CHADEMA REWARDS WILL BE REALIZED COME 1st september2010
Nawasilisha
 
Chadema sio Dr Slaa na Mh Mbowe pekee yao,CHADEMA ni ya watanzania wote wapenda mabadiliko.
Haya ni mabadiliko ya Lazima.na lazima tushinde.
Tanzania bila ku-overhaul serekali nzima tutarudi kwenye utumwa na umaskini wa kutupwa.
Sasa kazi ya kulinda kuhesabu kura ni yako na mimi
.pale ulipo.
 
historia inaonyesha vyama tawala huwa haviogopi yote hayo, huwa vina-deal na mtangaza matokeo tu!sijui umejitayarishaje!
 
Kuna vituo vingapi vya kupiga kura Tanzania nzima? Je kila mkoa/wilaya (chama) unaweza kushiriki vipi kuandaa wasimamizi wake, na pale inapobidi kuwasambaza siku ya kupiga kura bila kujali eneo analoishi ili kuzuia uwezekano wa kuhongeka hata kabla ya siku ya kura. Naamini kila mkoa/wilaya/jimbo likijipanga vyema kwa kufuata maelekezo na usimamizi wa taifa, mabadiliko yanaweza kuonekana.
 
Tupo wote kwenye hilo lakini karata turufu ya CCM ni kuwanunua mawakala wa Chadema ili wasaini matokeo ya mezani badala ya kuhesabu kura.

Chadema wakiweza hilo basi ushindi hauna utata hata kidogo.

Wewe inaonyesha ni mtaalamu sana wa mbinu za kuiba kura. Je huko CCM ndiyo ilikuwa shughuli yako huko kabla mwaka huu hujaruka ukuta? :becky:
 
Wameanza kuandikisha shahada za kupigia kura siku zote sikujua kwamba hii kazi inafanyika jana usiku mnamo saa nne nilitembelewa na mjumbe wa nyumba kumi kwa sababu wanajua mimi ni mwana CCM wakaniambia wanataka kujua kama shahada yangu niliihakiki wakati tume ilipita kuandikisha upya daftari la wapiga kura ,nikawambia sikuhakiki kwa sababu niliwasikia tume kama huna tatizo na kipande chako huna sababu ya kwenda huko wakasema basi tunataka kuandikisha wanachama wetu ili tuone wangapi watatupigia kura ,mimi nikawambia mwaka huu mimi nitapigia upinzani kwa sababu naipenda sana nchi yangu siwezi kuiweka rehani kwa miaka mingine mitano
Basi wakaniambia eti watakuja kuongea tena na mimi leo kwani wanaona labda nilikuwa na uchovu wa Kazi kwa hiyo haukuwa muda mwa faka wa kuongea wakiondoka waliataka kuacha chupa ya mvinyo
nikajiuliza hivi kweli kura yangu naweza nikaiiuza kwa chupa ya mvinyo
Lazima mkakati thabiti ufanyike wa kuhakikisha tunalinda kura wenzetu wa pinzani wanaweza kuandikisha watu watakao jitolea hata bila kulipwa na vyama na kushirikiana na wananchi wenye mapenzi mema kuhakikisha haki inatendeka leo nimetayarisha maji ya pilipili wakija nawamwagia ha ha
 
Wameanza kuandikisha shahada za kupigia kura siku zote sikujua kwamba hii kazi inafanyika jana usiku mnamo saa nne nilitembelewa na mjumbe wa nyumba kumi kwa sababu wanajua mimi ni mwana CCM wakaniambia wanataka kujua kama shahada yangu niliihakiki wakati tume ilipita kuandikisha upya daftari la wapiga kura ,nikawambia sikuhakiki kwa sababu niliwasikia tume kama huna tatizo na kipande chako huna sababu ya kwenda huko wakasema basi tunataka kuandikisha wanachama wetu ili tuone wangapi watatupigia kura ,mimi nikawambia mwaka huu mimi nitapigia upinzani kwa sababu naipenda sana nchi yangu siwezi kuiweka rehani kwa miaka mingine mitano
Basi wakaniambia eti watakuja kuongea tena na mimi leo kwani wanaona labda nilikuwa na uchovu wa Kazi kwa hiyo haukuwa muda mwa faka wa kuongea wakiondoka waliataka kuacha chupa ya mvinyo
nikajiuliza hivi kweli kura yangu naweza nikaiiuza kwa chupa ya mvinyo
Lazima mkakati thabiti ufanyike wa kuhakikisha tunalinda kura wenzetu wa pinzani wanaweza kuandikisha watu watakao jitolea hata bila kulipwa na vyama na kushirikiana na wananchi wenye mapenzi mema kuhakikisha haki inatendeka leo nimetayarisha maji ya pilipili wakija nawamwagia ha ha

Unaishi Mbezi ama Kimara? :becky:
 
CUF na CHADEMA na vyama vingine (kasoro TLP) vinapaswa kushirikiana kuhakikisha CCM haifanikiwi kuiba kura zao. Tofauti zao zibaki kisera ila vita yao iwe kuingoa CCM tuu. Kati yao yeyote akishinda kuna uwezekano wa kushirikiana katika kuijenga upya nchi hii.
Nimesema kasoro TLP kwa vile tayari bosi wa TLP anampigia kampeni kiongozi wa CCM, tunadhani huo ndio msimamo wa chama chao maana hakuna kiongozi mwingine wa TLP aliyempinga mwenyekiti wao katika hizo kauli zake
 
Kweli wanatakiwa mawakala walio na moyo wa uzalendo, hapa tu ndio ccm wanaposubiri kuwashangaza watu wanaotegemea kuona mabadiliko.
 
Back
Top Bottom