CHADEMA Siwaelewi mnachokisimamia

CHADEMA Siwaelewi mnachokisimamia

Kauli zilizowahi kutolewa na mmiliki mwenza wa Chadema Lowassa kwamba yeye ameshikilia amani ya nchi kwani watu kwa kauli yake wanaweza kuingia mitaani siyo kauli ndogo

Namhusisha pia na Maalim Seif kwamba vijana wanamsumbua wakitaka awape ruhusa walianzishe hiyo kauli aliitoa alipokuwa anahojiwa na kituo kimoja cha luninga.

Lowassa amekuwa akiirudia kauli hii kila apatapo nafasi kuelezea uchaguzi wa 2015 alivyotolewa kamasi.

Kinachoendelea Arusha kuhusu suala la watoto wetu waliofariki ni jambo la aibu kubwa ambapo Watanzania wenzetu viongozi wa siasa za upinzani wameshiriki kwa kiwango kikubwa kwenye aibu hii. Badala ya kuwafariji wafiwa na kuwaacha watoto wapumzike kwa amani watu hawa wamekuwa wakielezea umma propaganda za rambirambi za wafiwa huku wakijipa kazi ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu za rambirambi hio.

Sasa maombolezo yamegeuka mtaji wa kisiasa. Nakumbuka kauli ya Lema alipokuwa anaelezea kutopata nafasi kusema lolote uwanjani, alisema ....Ni wazi sasa kwamba tofauti yetu sisi kama nchi na Syria ni wakati.... (Mwisho wa kunukuu). kwa wenye akili ya kutafakari unajua anachokitafuta Lema ni kuona nchi inaingia kwenye machafuko.

Mchungaji Msigwa (Mbunge) aliwahi kuonyeshwa katika video mitandaoni akitaka kutekeleza kwa vitendo sera ya chama chake kutaka kumpiga mkuu wa Wilaya Richard Kasesera....

Turudi kwa Sugu (Mbunge) amekuwa mara kwa mara akitaka kupigana ndani ya Bunge pale anapoona jambo analolazimisha kukataliwa.

Halima Mdee naye hivi karibuni amejadiliwa na Kamati ya Nidhamu na Hadhi ya Wabunge kwa kauli zenye uchu wa vurugu na kulivunjia heshima Bunge alizozitoa wakati Bunge linaendelea.

Inawezekana haya yanayofanyika leo watu wasijue nini hatima yake lakini ni wazi hawa ndugu zetu hawapo tayari kudumisha amani na mshikamano wa nchi yetu. Wapo tayari kuona watu wakifarakana na inawauma sana wanapoona serikali inatimiza wajibu wake ndiyo maana wanajitahidi kuchafua hali ya hewa kila inapobidi ili kuondoa utulivu wa kisiasa.

Mitandaoni hali ni tete kabisa, vitisho, kebehi hata wananchi ambao wengine walionyesha kushangilia pale polisi wetu walipopoteza maisha wakiwa kazini hata wengine waliokamatwa kwakuwatukana viongozi walijitokeza mawakili kutoka upinzani kuwatetea mahakamani.

Sijasema ya Tundu Lisu maana kila mmoja anajua nini mefanya, anafanya na matarajio yake kwa amani ya nchi yetu.

Ni wakati sasa wa Watanzania kupitia viongozi wao kuungana kuleta maendeleo chanya ikiwemo kushiriki shughuli za kiuchumi na kuhakikisha wanatekeleza sera za umoja wa kitaifa.

Kinyume na hapo, nawaambia CHADEMA kuwa roho za watanzania wasiziweke rehani kwa uchu wao wa madaraka. Wafanye siasa safi
Asante kwa pumba. Haya nenda kazini sasa
 
Tumekusikia mla rambi rambi. Nyie mnakoelekea mtahamisha hata reli ili mpate rambi rambi.
Mejichokea sana mpaka mnavizia rambi rambi mziingize kweny matumiz ya serikali km kujenga hospital, kujenga shule n.k
Increment mkalala nazo mbele, watoka pabaya nyie. Kweli nyie Mafisi
Hii nchi ishakuwa ya ovyo sana. Hongera mkuu naona Rambi rambi za watu unazifanyia fujo humu na bundle za internet.
Wazee wa rambi rambi
Unakandia bure, hiyo hospital ikijengwa nyie ndo mtakuwa wa kwanza kutibiwa
 
Umeongea ukweli mtupu,, hili ni jambo lipo wazi hata kama ulipata FAFAFAFAAA huwezi shindwa kuelewa hili.

Umetoa ushauri mzuri sana, Chadema na wengine mlioko upinzani angalieni tatizo lipo wapi? Je ni kweli hampigiwi kura kwa wingi? Na kama mnapata hizo kura tatizo lipo wapi? Hilo ndo la kushughulikia. Na siyo mengine.

Ukweli mfumo usiposhughulikiwa afadhali hata uchaguzi usiwepo ni kupoteza tu hela nyiingi, zinaweza jenga hata kiwanda kimoja watu wakapata ajira.

Barabosa leo Lumumba lazima wakutoze faini huwezi kuwasaidia timu pinzani namna hii.
 
Hamuwezi kushinda Uchaguzi TanZania hata iweje, hata kama ikitokea Miujiza labda Watanzania siku moja wakawaamini na kuwapigia kura nyingi lkn bado hamtaweza kuiondoa CCM kwa maana mfumo wa Tanzania hauko tayari kwa hilo, na huwo ndiyo ukweli anzieni hapo kwanza, mengine yote ni kupoteza muda tu, ...
Hivi nyie huwa mnashinda sio?
 
Wewe unataka wasimame nini? Maana kwenye huwezi kwenda na moja na mambo habadilika kulingana na wakati, kama ni rushwa bado zipo kulingana na ripoti ya CAG, nchi inamakandokando mengi sana ndio lowassa akiongea kidogo ccm. Mapovu!
 
Tanzania siyo Nigeria, jaribu kuusoma mfumo wa Tanzania kwanza, CCM ni zaidi ya Chama cha Siasa!

Tanzania ni kama Kenya labda au pia haiwezi kuwa hivyo? Ninavyofahamu nchi zilizoiga mfumo wa kijamaa vyama vyake vilivyokuwepo tangu kudai uhuru vinafanana kimfumo na kitabia sasa tuangalie kuanzia hapo.
 
Hamuwezi kushinda Uchaguzi TanZania hata iweje, hata kama ikitokea Miujiza labda Watanzania siku moja wakawaamini na kuwapigia kura nyingi lkn bado hamtaweza kuiondoa CCM kwa maana mfumo wa Tanzania hauko tayari kwa hilo, na huwo ndiyo ukweli anzieni hapo kwanza, mengine yote ni kupoteza muda tu, ...
You're right kwa sababu aliye draft huo mkataba wa hatimiliki yenu NSSF Tanzania ni Mungu wa mbinguni
 
Kauli zilizowahi kutolewa na mmiliki mwenza wa Chadema Lowassa kwamba yeye ameshikilia amani ya nchi kwani watu kwa kauli yake wanaweza kuingia mitaani siyo kauli ndogo

Namhusisha pia na Maalim Seif kwamba vijana wanamsumbua wakitaka awape ruhusa walianzishe hiyo kauli aliitoa alipokuwa anahojiwa na kituo kimoja cha luninga.

Lowassa amekuwa akiirudia kauli hii kila apatapo nafasi kuelezea uchaguzi wa 2015 alivyotolewa kamasi.

Kinachoendelea Arusha kuhusu suala la watoto wetu waliofariki ni jambo la aibu kubwa ambapo Watanzania wenzetu viongozi wa siasa za upinzani wameshiriki kwa kiwango kikubwa kwenye aibu hii. Badala ya kuwafariji wafiwa na kuwaacha watoto wapumzike kwa amani watu hawa wamekuwa wakielezea umma propaganda za rambirambi za wafiwa huku wakijipa kazi ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu za rambirambi hio.

Sasa maombolezo yamegeuka mtaji wa kisiasa. Nakumbuka kauli ya Lema alipokuwa anaelezea kutopata nafasi kusema lolote uwanjani, alisema ....Ni wazi sasa kwamba tofauti yetu sisi kama nchi na Syria ni wakati.... (Mwisho wa kunukuu). kwa wenye akili ya kutafakari unajua anachokitafuta Lema ni kuona nchi inaingia kwenye machafuko.

Mchungaji Msigwa (Mbunge) aliwahi kuonyeshwa katika video mitandaoni akitaka kutekeleza kwa vitendo sera ya chama chake kutaka kumpiga mkuu wa Wilaya Richard Kasesera....

Turudi kwa Sugu (Mbunge) amekuwa mara kwa mara akitaka kupigana ndani ya Bunge pale anapoona jambo analolazimisha kukataliwa.

Halima Mdee naye hivi karibuni amejadiliwa na Kamati ya Nidhamu na Hadhi ya Wabunge kwa kauli zenye uchu wa vurugu na kulivunjia heshima Bunge alizozitoa wakati Bunge linaendelea.

Inawezekana haya yanayofanyika leo watu wasijue nini hatima yake lakini ni wazi hawa ndugu zetu hawapo tayari kudumisha amani na mshikamano wa nchi yetu. Wapo tayari kuona watu wakifarakana na inawauma sana wanapoona serikali inatimiza wajibu wake ndiyo maana wanajitahidi kuchafua hali ya hewa kila inapobidi ili kuondoa utulivu wa kisiasa.

Mitandaoni hali ni tete kabisa, vitisho, kebehi hata wananchi ambao wengine walionyesha kushangilia pale polisi wetu walipopoteza maisha wakiwa kazini hata wengine waliokamatwa kwakuwatukana viongozi walijitokeza mawakili kutoka upinzani kuwatetea mahakamani.

Sijasema ya Tundu Lisu maana kila mmoja anajua nini mefanya, anafanya na matarajio yake kwa amani ya nchi yetu.

Ni wakati sasa wa Watanzania kupitia viongozi wao kuungana kuleta maendeleo chanya ikiwemo kushiriki shughuli za kiuchumi na kuhakikisha wanatekeleza sera za umoja wa kitaifa.

Kinyume na hapo, nawaambia CHADEMA kuwa roho za watanzania wasiziweke rehani kwa uchu wao wa madaraka. Wafanye siasa safi
Kichwa kikiwa kikubwa halafu kisiwe na akili mara nyingi shingo hupata shida sana Naionea huruma shingo lako
 
Chadema wlifurahi sana kufa wale watoto kule arusha....kila siku ni kiki za hao watoto...Chadema ni janga la Taifa
Ni yupi anayefurahia?

Anayeng'ang'ania kumuuguza mgonjwa ili anywe uji wake au yule anayeng'ang'ania mgonjwa apewe uji wake??
 
Back
Top Bottom