CHADEMA sasa yamvuruga Zitto ACT-Tanzania

CHADEMA sasa yamvuruga Zitto ACT-Tanzania

TataMadiba

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2014
Posts
9,868
Reaction score
5,753
zitto.jpg

Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), kimehusishwa na harakati chafu za kukisambaratisha chama cha Alliance for Change and Transparent-TANZANIA (ACT-TANZANIA) ili kumkomoa mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe anayehusishwa na chama hicho.

Akizungumzia uhusika wa CHADEMA kwenye mgogoro unaoendelea ndani ya ACT-TANZANIA, Katibu Mkuu wa muda wa ACT, SAMSON MWIGAMBA amesema Mwenyekiti wa muda wa ACT-TANZANIA, KADAWI LIMBU anashirikiana na baadhi ya viongozi wa CHADEMA kukimaliza chama chao kutokana na kuhofia ACT ikiwa ni pamoja na kumshughulikia ZITTO ili aonekane ni mwanasiasa asiyefaa.

MWIGAMBA alisema baashi ya matamko na maamuzi ya chama yamekuwa yakiandaliwa kwenye moja ya CHUMBA CHA HABARI NCHINI AMBACHO MMILIKI WAKE NI MKEREKETWA WA CHADEMA.

Akithibitisha hilo, Mwigamba lisema ushahidi wa analolisema upo kwani Mwenyekiti wao ni MSHIRIKA KWENYE MOJA YA MAKUNDI YA MTANDAO WA KIJAMII WA WABUNGE WA CHADEMA, ambapo aliwahi kutuma ujumbe wenye kuwaeleza kuwa amekamilisha kazi ya KUWATIMUA yeye na prof.KITLA.


Chanzo: RAI NGUVU YA HOJA.
 
Mfamaji haishi kutapatapa.

Unapoingia vitani ukamilike na ujikamilishe, sio unaingia kichwakichwa hata huwezi kumudu vikao vyako na viongozi wako.

Ukiharibikiwa kubali kushindwa na ujipange usisingizie CDM, kwataarifa yako CDM siyo saizi ya mgonjwa ACT. waulize ccm wanaelewa vema.
 
Hii vita ni ngumu, Chadema lazima wafanye hivyo la sivyo ZITTO atawaumiza. SIASA ni kuwahiana.
 
Kwa maelezo haya ni ushahidi tosha wa uhusiano mkubwa kati ya Zitto na ACT (Alliance for Cowards and Traitors)
Ni kweli kabisa, lakini kuna tatizo gani kama CHADEMA walishamsusa? Wamuache tu kijana wa watu afanye siasa, huko ndiko kuna riziki yake.
 
chadema ni chama cha ajabu sana kazi yao kuvuruga wenzao japo zitto naye hata akivurugwa sawa tu maana ni mpuuzi tu,kwanza mwizi na mla rushwa wa kwanza.
 
Hehehehe, inachekesha jinsi ambavyo ujumbe mmoja wa simu unavyoweza kumpa mtu ujasiri wa kuita waandishi wa habari na kutoa msimamo juu jambo linalomuhusu Mwenyekiti wake. Nchi hii imejaa wambea, wapayukaji na wajinga. Hakuna anayekaa na kutafakari na kujua nini afanye katika nafasi aliyopo. Inasikitisha viongozi wakubwa ndani ya chama kichanga kuwa mapoyoyo kama huyu. ACT sioni future yake.
 
Ko kumbe zzk ni mhusika wa ACT!!! Ooookeeeeeee,,, basi sawaaaa
 
Ni kweli kabisa, lakini kuna tatizo gani kama CHADEMA walishamsusa? Wamuache tu kijana wa watu afanye siasa, huko ndiko kuna riziki yake.

mkuu mimi nadhani zitto acha avurugwe tu kazidi upuuzi juzi bungeni kupitia kamati ya PAC wamehongwa hela na mengi wamekuja kutupotosha kwa kutetea rushwa walizokula.

Jambo lingine baya zaidi zitto anapenda sana ushirikina mtu kama huyo hafai kwenye jamii yenye kumuamini mungu kama yetu akae kwa shetani na michadema yao pamoja na ICT yote majuha tu.
 
SAMSON mwigamba usaliti ndiodamu yako.
 
Last edited by a moderator:
Zitto ana akili sana. Anawatesa sana chadema. Na bado
 
hizi siasa bwana...mimi nilishauri CDM wamalize tofauti zao na zitto. Zitto kaifanyia mengi cdm leo hii msihesabu ubaya wa zitto kwa kuona mabaya tu vipi kuhusu mchango wake kuhusu kuikuza cdm. ndani ya cdm kuna wanadiplomasia walio bobea malizeni tatizo la zitto na cdm. kama mnaona hafai mwacheni akafanye siasa anapo ona panafaa
 
Jambo lingine baya zaidi zitto anapenda sana ushirikina mtu kama huyo hafai kwenye jamii yenye kumuamini mungu kama yetu akae kwa shetani na michadema yao pamoja na ICT yote majuha tu.[/QUOTE]

apo unakuny@ ama unaandika,? sijakuelewa ivi!
 
mimi niliwahi kusema kuwa chadema hawawezi kusimama wenyewe bila zitto ndiyo maana wanafanya vitimbi ili arudi japo zitto naye hewa kabisa.
 
Kwa nini ACT inamtetea ZZK ambaye yeye mwenyewe hataki chama kingine zaidi ya CHADEMA na ndio maana alipofukuzwa uanachama yeye mwenyewe akaenda mahakamani kupinga kufukuzwa?
 
chadema ni chama cha ajabu sana kazi yao kuvuruga wenzao japo zitto naye hata akivurugwa sawa tu maana ni mpuuzi tu,kwanza mwizi na mla rushwa wa kwanza.

LB7 tabia zenu hazieleweki kabisa.
 
Back
Top Bottom