Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Kishindo cha CHADEMA chawavuruga CUF, CCM
Mtatiro wa CUF aivurumishia shutuma nzito
na Waandishi wetu
MAFANIKIO ya kisiasa ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) yanaonekana kuzidi kuwa kero kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), Tanzania Daima limebaini.
Hali hiyo ilizidi kujidhihirisha jana, baada ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro kuendelea kutoa matamshi yenye mwelekeo wa chuki na husuda dhidi ya CHADEMA yaliyomfikisha hatua ya kujikuta akitumia lugha isiyo na staha inayofanana na hadhi ya chama hicho cha upinzani chenye nguvu kubwa Tanzania Visiwani.
Mtatiro ambaye tangu aingie katika kiringe cha siasa za kitaifa amekuwa akifanya juu chini kupambana na CHADEMA na viongozi wake kwa namna ile ile inavyofanywa na viongozi wengine wa chama hicho, jana alieleza kusikitishwa na hatua ya CHADEMA kuamua kuunda kambi yao ya upinzani bungeni pasipo kushirikiana na wapinzani wengine.
Mtatiro ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita aligombea ubunge wa Ubungo kwa tiketi ya CUF akikataa katakata ushawishi wa vijana waliokuwa wakimtaka amwachie John Mnyika wa CHADEMA, aliibuka na kuwashambulia wapinzani wenzake hao akiwapa sifa na majina mabaya.
Mtatiro na CUF wanaonekana kukerwa na tamko la CHADEMA lililotolewa juzi na Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa aliyetangaza rasmi kuunda upinzani unaojitegemea bungeni.
Akitoa tamko lililosheheni kauli za jazba, propaganda, maneno ya mitaani na matusi, Mtatiro aliishambulia CHADEMA na viongozi wake akisema lengo lao la kukataa kushirikiana na CUF ni kutaka chama hicho kife.
Viongozi wa CHADEMA na chama chao ndio watakaokufa na kuiacha CUF ikiimarika CHADEMA ni chama popo, ndumilakuwili na wajinga, alisema Mtatiro ambaye alikwenda mbele na kuwafananisha viongozi wa chama hicho cha upinzani na Padri aliyekiuka kiapo na kukimbilia kula raha na wachumba.
Wakati akiishambulia CHADEMA, Mtatiro alisema chama chake kitaendelea kushirikiana na CCM Zanzibar kwani kilichotokea Zanzibar ndiyo matakwa halisi ya wananchi wa visiwa hivyo na kamwe hakitawalamba miguu na CHADEMA ili kushirikiana nao.
CUF tunaamini CHADEMA wamewadharau Wazanzibari, wanawaona hawana maana, wanadharau maamuzi yao, wanaona hawawezi kufikiri na kujiamulia mambo yao wenyewe, hilo hatunalo shaka, alisema Mtatiro.
Akiendelea kuishambulia CHADEMA alisema chama hicho kiliusaliti ushirikiano wa vyama vya upinzani katika chaguzi ndogo za Tarime, Tunduru, Busanda, Mbeya Vijijini na hatimaye kusababisha uvunjike, akidai kuwa mara zote kilitaka kisimamishe wagombea wake hata katika maeneo ambako kilikuwa hakina nguvu.
Huku akionekana kuwa naye aligombea ubunge Ubungo ilhali akijua CHADEMA na Mnyika walikuwa wamejizatiti, Mtatiro alitoa maelezo ambayo yalionekana yakiwa na mwelekeo wa wazi wa kujikanganya.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, chanzo cha kuvunjika kwa ushirikiano huo wa upinzani, ni hatua ya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa kauli zilizoonyesha kuunga kwao mkono tuhuma za kubuni dhidi ya viongozi hao wa CHADEMA kwamba walikuwa na mkono wao katika kifo cha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Chacha Wangwe.
Maudhui na aina ya lugha ya matusi iliyotumiwa na CUF katika tamko hilo kwa kiasi fulani vilionekana kufanana na mashambulizi yaliyofanywa na Jumuiya ya Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) hivi karibuni dhidi ya CHADEMA na Dk. Slaa ambaye wamekuwa wakimwita mwendawazimu bila kufafanua.
Katika hatua nyingine inayoashiria kuzidi kuungwa mkono kwa CHADEMA na viongozi wake, jana Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alikuwa kivutio katika sherehe ya Siku ya Sheria nchini iliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ambayo rais Jakaya Kikwete alikuwa mgeni rasmi.
Mbowe alikuwa kivutio wakati akiinuka kwenye kiti alichokaa kuelekea kwenye ngazi za Mahakama Kuu kupiga picha na viongozi mbalimbali wa serikali na mahakama ambao ni watumishi wa mahakama, mawakili na wananchi mbalimbali waliohudhuria sherehe hiyo.
Watumishi wa mahakama pamoja na wananchi hao walisikika wakimshangilia kwa sauti ya juu Mbowe Mbowe, Mbowe na kiongozi huyo kulazimika kuwapungia mkono na kutabasamu.
Akitoa hotuba yake katika sherehe hizo, Rais Kikwete aliutaka mhimili wa mahakama kushirikiana na vyombo vya habari kutoa elimu kwa umma kuhusu utendaji kazi na muundo wa mahakama ukoje kwani kwa kufanya hivyo kutamuondolea adha anayoipata hivi sasa ya wananchi kufika Ikulu na kumtaka atengue hukumu mbalimbali wakilalamika kutotendewa haki.
Wananchi wamekuwa wakijazana pale ofisini wakitaka nitengue hukumu zilizokwishatolewa na mahakama na mimi nimekuwa nikiwaambia sina mamlaka ya kufanya hivyo wananchi hao wamekuwa wakinijibu kama siwezi kufanya hivyo watamchagua rais anayeweza kufanya hivyo na kwamba ndiyo maana wanataka katiba mpya lakini yote hii inasababishwa na umma kuwa na uelewa finyu wa sheria na muundo wa mahakama, alisema Kikwete na kusababisha watu kuangua vicheko.
Wakati huo huo Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga juzi alilazimika kutumia salamu za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ili kuwashawishi wanafunzi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Mbeya (MIST) waweze kumsikiliza.
Kitwanga alilazimika kukikubali japo kwa muda Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kutokana na hatua ya wanafunzi wa chuo hicho kuguna kila alipoitaja ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi wakati akizungumza nao kuhusu inavyotekeleza sera ya elimu.
Waziri huyo alilazimika kuwasalimia wanafunzi hao akisema CHADEMA hoyee!!, na ukumbi mzima ulizizima kwa mayowe na vifijo vya wanafunzi waliopaza sauti zao wakimjibu Oyeeee huku kila mmoja akimpungia alama ya vema kwa kuonyesha vidole viwili.
Kitendo cha Waziri Kitwanga kutumia jina la CHADEMA katika kibwagizo hicho kilitokana na hatua ya wanafunzi hao kuguna pale alipoanza kujibu maswali yao kwa kusema katika Ilani ya ya CCM .. bila kumalizia kusema alishtushwa na miguno.
Mtatiro wa CUF aivurumishia shutuma nzito
na Waandishi wetu
Hali hiyo ilizidi kujidhihirisha jana, baada ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro kuendelea kutoa matamshi yenye mwelekeo wa chuki na husuda dhidi ya CHADEMA yaliyomfikisha hatua ya kujikuta akitumia lugha isiyo na staha inayofanana na hadhi ya chama hicho cha upinzani chenye nguvu kubwa Tanzania Visiwani.
Mtatiro ambaye tangu aingie katika kiringe cha siasa za kitaifa amekuwa akifanya juu chini kupambana na CHADEMA na viongozi wake kwa namna ile ile inavyofanywa na viongozi wengine wa chama hicho, jana alieleza kusikitishwa na hatua ya CHADEMA kuamua kuunda kambi yao ya upinzani bungeni pasipo kushirikiana na wapinzani wengine.
Mtatiro ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita aligombea ubunge wa Ubungo kwa tiketi ya CUF akikataa katakata ushawishi wa vijana waliokuwa wakimtaka amwachie John Mnyika wa CHADEMA, aliibuka na kuwashambulia wapinzani wenzake hao akiwapa sifa na majina mabaya.
Mtatiro na CUF wanaonekana kukerwa na tamko la CHADEMA lililotolewa juzi na Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa aliyetangaza rasmi kuunda upinzani unaojitegemea bungeni.
Akitoa tamko lililosheheni kauli za jazba, propaganda, maneno ya mitaani na matusi, Mtatiro aliishambulia CHADEMA na viongozi wake akisema lengo lao la kukataa kushirikiana na CUF ni kutaka chama hicho kife.
Viongozi wa CHADEMA na chama chao ndio watakaokufa na kuiacha CUF ikiimarika CHADEMA ni chama popo, ndumilakuwili na wajinga, alisema Mtatiro ambaye alikwenda mbele na kuwafananisha viongozi wa chama hicho cha upinzani na Padri aliyekiuka kiapo na kukimbilia kula raha na wachumba.
Wakati akiishambulia CHADEMA, Mtatiro alisema chama chake kitaendelea kushirikiana na CCM Zanzibar kwani kilichotokea Zanzibar ndiyo matakwa halisi ya wananchi wa visiwa hivyo na kamwe hakitawalamba miguu na CHADEMA ili kushirikiana nao.
CUF tunaamini CHADEMA wamewadharau Wazanzibari, wanawaona hawana maana, wanadharau maamuzi yao, wanaona hawawezi kufikiri na kujiamulia mambo yao wenyewe, hilo hatunalo shaka, alisema Mtatiro.
Akiendelea kuishambulia CHADEMA alisema chama hicho kiliusaliti ushirikiano wa vyama vya upinzani katika chaguzi ndogo za Tarime, Tunduru, Busanda, Mbeya Vijijini na hatimaye kusababisha uvunjike, akidai kuwa mara zote kilitaka kisimamishe wagombea wake hata katika maeneo ambako kilikuwa hakina nguvu.
Huku akionekana kuwa naye aligombea ubunge Ubungo ilhali akijua CHADEMA na Mnyika walikuwa wamejizatiti, Mtatiro alitoa maelezo ambayo yalionekana yakiwa na mwelekeo wa wazi wa kujikanganya.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, chanzo cha kuvunjika kwa ushirikiano huo wa upinzani, ni hatua ya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa kauli zilizoonyesha kuunga kwao mkono tuhuma za kubuni dhidi ya viongozi hao wa CHADEMA kwamba walikuwa na mkono wao katika kifo cha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Chacha Wangwe.
Maudhui na aina ya lugha ya matusi iliyotumiwa na CUF katika tamko hilo kwa kiasi fulani vilionekana kufanana na mashambulizi yaliyofanywa na Jumuiya ya Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) hivi karibuni dhidi ya CHADEMA na Dk. Slaa ambaye wamekuwa wakimwita mwendawazimu bila kufafanua.
Katika hatua nyingine inayoashiria kuzidi kuungwa mkono kwa CHADEMA na viongozi wake, jana Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alikuwa kivutio katika sherehe ya Siku ya Sheria nchini iliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ambayo rais Jakaya Kikwete alikuwa mgeni rasmi.
Mbowe alikuwa kivutio wakati akiinuka kwenye kiti alichokaa kuelekea kwenye ngazi za Mahakama Kuu kupiga picha na viongozi mbalimbali wa serikali na mahakama ambao ni watumishi wa mahakama, mawakili na wananchi mbalimbali waliohudhuria sherehe hiyo.
Watumishi wa mahakama pamoja na wananchi hao walisikika wakimshangilia kwa sauti ya juu Mbowe Mbowe, Mbowe na kiongozi huyo kulazimika kuwapungia mkono na kutabasamu.
Akitoa hotuba yake katika sherehe hizo, Rais Kikwete aliutaka mhimili wa mahakama kushirikiana na vyombo vya habari kutoa elimu kwa umma kuhusu utendaji kazi na muundo wa mahakama ukoje kwani kwa kufanya hivyo kutamuondolea adha anayoipata hivi sasa ya wananchi kufika Ikulu na kumtaka atengue hukumu mbalimbali wakilalamika kutotendewa haki.
Wananchi wamekuwa wakijazana pale ofisini wakitaka nitengue hukumu zilizokwishatolewa na mahakama na mimi nimekuwa nikiwaambia sina mamlaka ya kufanya hivyo wananchi hao wamekuwa wakinijibu kama siwezi kufanya hivyo watamchagua rais anayeweza kufanya hivyo na kwamba ndiyo maana wanataka katiba mpya lakini yote hii inasababishwa na umma kuwa na uelewa finyu wa sheria na muundo wa mahakama, alisema Kikwete na kusababisha watu kuangua vicheko.
Wakati huo huo Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga juzi alilazimika kutumia salamu za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ili kuwashawishi wanafunzi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Mbeya (MIST) waweze kumsikiliza.
Kitwanga alilazimika kukikubali japo kwa muda Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kutokana na hatua ya wanafunzi wa chuo hicho kuguna kila alipoitaja ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi wakati akizungumza nao kuhusu inavyotekeleza sera ya elimu.
Waziri huyo alilazimika kuwasalimia wanafunzi hao akisema CHADEMA hoyee!!, na ukumbi mzima ulizizima kwa mayowe na vifijo vya wanafunzi waliopaza sauti zao wakimjibu Oyeeee huku kila mmoja akimpungia alama ya vema kwa kuonyesha vidole viwili.
Kitendo cha Waziri Kitwanga kutumia jina la CHADEMA katika kibwagizo hicho kilitokana na hatua ya wanafunzi hao kuguna pale alipoanza kujibu maswali yao kwa kusema katika Ilani ya ya CCM .. bila kumalizia kusema alishtushwa na miguno.