kitambiheshima
JF-Expert Member
- May 27, 2013
- 452
- 116
Hali ya chama cha demokrasia na maendeleo mkoani Ruvuma kina hali mbaya kufuatia mwenyekiti wake wa mkoa Joseph Fuime na Katibu wa jimbo Mbogolo kutokuwa na maelewano kwa muda mrefu sasa.
Chanzo cha mgongano ni ubunge 2015 ambapo Joseph Fuime ana mpango wa kugombea nafasi hiyo huku nae Mbogolo anaitaka kwa udi na uvumba.
Imefikia hatua baadhi ya wanachama wameanza kufungasha virago na kutimkia vyama vingine.
Aidha baadhi ya madiwani wamegawanyika ambapo wengine wako upande wa Fuime na wengine kwa Mbogolo.
Tarehe 28.11.2013 chama hicho kinafanya kikao na moja ya agenda inaedaiwa kuwa itahusu msimamo wa CHADEMA kuhusu kunyang'anywa madaraka ya chama Zitto Kabwe.
Chanzo cha taarifa kutoka ndani ya CHADEMA kimetonya kuwa swala la Zitto limeongeza mpasuko ambapo kundi kubwa la viongozi wa wilaya na mkoa liko upande wa Zitto Kabwe,kundi hilo linaongozwa na Fuime
Chanzo cha mgongano ni ubunge 2015 ambapo Joseph Fuime ana mpango wa kugombea nafasi hiyo huku nae Mbogolo anaitaka kwa udi na uvumba.
Imefikia hatua baadhi ya wanachama wameanza kufungasha virago na kutimkia vyama vingine.
Aidha baadhi ya madiwani wamegawanyika ambapo wengine wako upande wa Fuime na wengine kwa Mbogolo.
Tarehe 28.11.2013 chama hicho kinafanya kikao na moja ya agenda inaedaiwa kuwa itahusu msimamo wa CHADEMA kuhusu kunyang'anywa madaraka ya chama Zitto Kabwe.
Chanzo cha taarifa kutoka ndani ya CHADEMA kimetonya kuwa swala la Zitto limeongeza mpasuko ambapo kundi kubwa la viongozi wa wilaya na mkoa liko upande wa Zitto Kabwe,kundi hilo linaongozwa na Fuime