Nkobe
JF-Expert Member
- Feb 17, 2013
- 2,162
- 3,162
Mimi nashangaa sana kuona Baadhi ya Watanzania wanailaumu Chadema eti kwanini inapokea watu wanaotuhumiwa na Ufisadi mfano Lowasa. Chadema imewapigia ngoma Watanzania kuhusu ufisadi lakini bado Watanzania walio wengi hawaoneshwi na kuchukizwa na Ufisadi. Utaona hivi siku za karibuni kwenye mchakato wa kutangaza nia ndani ya CCM Watuhumiwa wa Ufisadi walionekana kuwa na wafuasi wengi. Hivyo, kama Watanania hawachukizwi na ufisadi, kuna tatio gani Chadema ikiwapokea mafisadi ili kuwafurahisha Watanzania?. Mimi nasema CHADEMA pokeeni mafisadi ili siku moja Watanzania wajue Umuhimu wenu wa wakati ule mlipokuwa mkipinga Mafisadi.