KWASASA CHADEMA NI CHAMA KIKUBWA KULIKO CCM!
Kwanza hongera sana Mbowe na Jopo zima lililopo ndani ya CHADEMA kwa kujenga chama kikubwa kuliko CCM kwa wakati huu na kuendelea.
Kuna watu hawawezi kuniamini kirahisi lakini napenda kuwaambia kuwa siku si nyingi CCM itakuwa chama cha UPINZANI na hapa ndipo nchi hii itakuwa kwenye mstari wa maendeleo.
KWALEO NISISEME MENGI NGOJA NIJIKITE KWENYE MSINGI WA HOJA YA MSINGI!
Katika historia ya Tanzania haijawahi kutokea wakati ambapo ccm ikawa na haja ya wanachama kama wakati huu, huu ni wakati ambao ccm wanafanya kukutafuta na kukubembeleza ili uhamie kwao, hata kama ulikuwa diwani tu watakutangaza kwenye vyombo vya habari na hata Rais atakushika mkono huku akikusifia.
Huu ni wakati ambao hata fedha inatumika kuwanunua wapinzani ili wahamie ccm kwani kimsingi hakuna sababu ya kimsingi ya kumtoa mtu upinzani aende ccm na ndio maana wakishakubali kuhamia utaratibu wa media coverage kuwatangaza lazima ufanyike.
Hii ni kwasababu kuna uhaba mkubwa wa watu huko ccm.
CCM inapitia kipindi kigumu sana, inapitia kipindi ambacho watu wamekosa imani na chama hicho huku pia ikionekana kwenye jamii kwamba kuwa mwanaccm ni ushamba.
Katika uwepo wake madarakani kwa miaka tangu UHURU ccm haina tena cha kuwadanganyia wananchi kwani bado Tanzania ni kati ya nchi masikini sana duniani Na hata Afrika, ni nchi ambayo ina kiwango kikubwa cha ujinga, ni nchi ambayo ina kiwango kikubwa cha maradhi kiasi kwamba Meli ya wachina ikija kutoa huduma za afya watu maelfu wanagombania huduma utadhani hakuna serikali kwenye hili taifa.
Katika hali kama hii ccm itawaambia nini tena wananchi, yote waliyoahidi hawajatekeleza na bado hali ya masiha ni ngumu mno!
Kilichopo kwa sasa ni kwamba wanajitahidi sana kuhakikisha wanaendelea kubaki madarakani ndio maana wanatumia nguvu nyingi mno za haki na zisizo za haki.
Katika awamu hii nguvu kubwa mno ya vyombo vya dola inatumika kuangamiza upinzani. Kama CHADEMA isingekuwa kuliko CCM yanini kutumia nguvu hizo?
Wakati mwingine hata hatari za kiuhai zipo na ishara zinaonekana ili madaraka yaendelee kushikwa.
Katika hali kama hii hata sheria zinapindishwa ili ikiwezekana wapinzani(CHADEMA) Wasiwasiliane kabisa na wananchi.
Hapa hata kama wewe ni mbishi kiasi gani lazima ukubaliane na mimi kwamba aliyeko madarakani ana hofu mno ya kuondoka kwani anaujua huu ukweli ambao wewe unataka kuupinga.
Nataka nieleweke kwamba ingelikuwa kuna uwanja sawia wa kufanya siasa kwa sasa kati ya CCM na UPINZANI hapo ndipo ungeamini kwa asilimia 100 hiki ninachokisema.
Hebu fikiria kidogo kwamba katika wakati ambao CCM imekimbiwa na mawaziri wake wakuu wawili, MZEE KINGUNGE NGOMBALE MWIRU, mawaziri, wabunge na wengi wengineo lazima wawe waoga kwani uzani kwasasa umelalia kwenye UPINZANI.
Wakati wa JK ilifika hatua watu wakihamia ccm sio ishu kabisa kwani CCM ilikuwa imejaa na hata unaweza ukaenda ccm ukakosa cheo kabisa kwani kumejaa. Hali ni tofauti sana kwa sasa kwani unaweza ukahama upinzani leo na kesho ukawa MKUU wa MKOA, DC,MKURUGENZI n.k Hii ni ili kuwavutia watu waje na maana yake ni kwamba MPINZANI KWENDA CCM KWASASA NI HADI AAHIDIWE AU APEWE FEDHA, MADARAKA, OPPRTUNITY n.k bila hivyo hakuna sababu nyingine.
Hebu fikiria hoja kama za KATAMBI na KAFULILA, yani hazina mashiko kabisa, eti Kafulila anasema amehama upinzani kwasababu ufisadi sio agenda tena ya upinzani… hivi kweli tatizo la TANZANIA linaloleta mkwamo ni UFISADI PEKEE? Jiulize.
Nawaambia ukweli na naomba mniamini kuwa endapo PATROBAS KATAMBI, KAFULILA, MASHA na wengineo wangekuwa na vyeo ambavyo dau lake ni kubwa kuliko hilo wanaloenda kupewa na ccm kamwe wasingehama.
Pamoja na hoja hizo lakini pia haya yanafanyika katika wakati huu ambapo CCM inaogopa kupoteza kata zote katika huu uchaguzi mdogo wa madiwani.
Dalili zinazoonekana huko katika msimu huu wa kampeni ni kwamba wataznania kwa sasa hawaitaki ccm kabisa na hali hii ni tishio mno ndio maana sasa kodi za watanzania inabidi zitumike kuwanunua wapinzani.
Nataka nikwambie jambo moja ambalo ni endapo Upinzani nao wangekuwa na Fedha ama vyeo vya kuwagawia wanachama wake walahi CCM isingewapata mpinzani anayehamia kwao!
HATARI KUBWA ILIYOPO KWA CCM NI HII!
Ipo siku fedha zitaisha kwani fedha hazioti kama majani. Mtapataje wanachama?
Ipo siku hao mnaowachukua watachoka kwani roho zao hazipo nanyi wamekuja huko kimwili.
Ipo siku mtashindwa kuhudumia wananchi kwani hela za kodi mmefanyia manunuzi, watawang’oa kwa mapanga na marungu.
Ipo siku mtachukua mashushushu na watawadhalilisha kama hamuamini ulizeni kule ARUMERU.
USHAURI WANGU KWENU CCM
Pambaneni na maisha na hali za watanzania hiyo ndio dawa ya kuuua upinzani! Japo hauwezi kufa kabisa kwani hata ulaya pamoja na maendeleo makubwa waliyo nayo bado upinzani una nguvu.
Tambueni kuwa watanzania wasasa wana uelewa mkubwa mno, hawana imani kabisa na jinsi mnavyochukua wapinzani, wengi wanaamini ni mchezo mchafu mnacheza kwani hawaoni sababu ya nyinyi kupendwa kiasi hicho.
MWISHO KABISA
WAPINZANI msirudi nyuma kwani hizi ni dalili kuwa mnawaumiza kiasi cha kutosha kuwafanya wasichague jema wala baya, hapa ndio pa kukazia uzi hata kama msikie viongozi wengi kiasi gani wanafika bei! CHADEMA na UPINZANI ni itikadi ambayo kamwe haitoondoka kwenye mioyo ya watanzania katika wakati ambao CCM BADO IKO MADARAKANI!
BADO WENGINE WATAHAMA!