Najua shilingi ina pande mbili,wapo watakaokubaliana na mimi, pia wapo watakaopingana na mimi juu ya CHADEMA.Lakini daima ukweli utasimama tu,kuna watu watapinga kwa nje lakini kimoyomoyo watakubaliana na ukweli huu.
Awali ya yote napenda kutoa pongezi za dhati kwa uongozi mzima wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) akiwemo Kamanda F.Mbowe,makamu m/kiti Arf Said,Katibu mkuu Dr.W.Slaa,Naibu k/mkuu zitto Kabwe na wanasheria wote wa CHADEMA.
Napenda kutumia nafasi kwa kuwa,hakuna chama cha siasa kilichowahi kupitia magumu kama CHADEMA.Kwani mambo mengi magumu na makubwa,mengine yanatia aibu kuyataja.Mambo hayo yapo yanayozungumzia maisha binafsi ya viongozi wa chama ambayo sio sehemu ya siasa na kwa ujumla wake hayana tija.Lakini pamoja na hayo nawashukuru viongozi kwa kuwa na umoja,mshikamano wa kutoyumbishwa na propaganda zote za watu/vyama vingine vya siasa hususani chama tawala.
Ni viongozi wa CHADEMA na wanachama pekee wamekuwa vinara wa kuwa na kesi nyingi kuliko kawaida.Najua huu ni ukandamizaji a demokrasia nchini.
Pamoja na magumu yote haya,CHADEMA inazidi kung'ara kwenye anga za siasa nchini.Hili ni jambo jema.Zaidi ya yote,magumu haya ndio yanaimarisha umoja wa chama kupitia viongozi wake.
Cha mwisho napenda kutoa wito kwa wanachama wote kuwa tusikate tamaa hakuna mafanikio yasiyo na changamoto,matatizo,majaribu na vikwazo.Au hakuna safari ndefu isiyo na changamoto zake.Tusikate tamaa kila tunaposikia propaganda za vyama vingine vya siasa,tuwe wazalendo kwa chama chetu.Tujiepushe na rushwa,ufisadi,lugha chafu na propaganda zinazoweza kutugawa kama chama na taifa zima kwa ujumla.Tuhimize upendo,umoja,uadilifu,umoja,amani na mshikamano.
Nawapongeza sana.