Mganga wa Jadi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2008
- 280
- 51
Ni kweli hawakushinda lakini inaonesha matumaini ya siku za usoni. Chadema sasa inakubalika visiwani ni vizuri kuendeleza mapambano mpaka upande huo wa nchi yetu.
Chadema,
Siku zote tunaamini kushindwa na kushinda vyote ni sawa kwa anaeshindana. Na kama mtaaluma kutoa tathini yenu ya kushindwa kwenu katika jimbo hili la Uzini ambalo kila wakti tuliaminishwa hapa barzani kuwa mambo ni mazuri sana na kampeni zinaendelea vizuri sana na mna uhakika wa kulichukua jimbo la Uzini.
matokeo yametoka na kuonyesha kuwa mmepata asilimia nne (4%). Tukumbuke kuna viongozi wakuu walikuwa kule na kuweka kambi kuhakikisha ushindi na walikuwa wanachukua posho kila siku. Je hawakuliona hilo kuwa wanamwelekeo mkubwa wa kushindwa? na kupunguza nguvu kubwa.
Tunaomba tathini yenu ya uchaguzi wa huko Uzini Znz ili kuona wapi mlijikwaa na hatua gani zitumike next time msijikwae tena ikiwa pamoja na kuwachukulia hatua wale wote waliohujumu iwe kwa kutoa taarifa au kwa vitendo na kupelekea kupata 4%.
Mwita,Hapo kwenye chama cha st.maalim seif ndipo ulitakiwa kuhoji imekuwaje kimeporomoka kiasi hicho?
Kujaribu kukimbia aibu yenu ccm B kwa kuizungumzia Chadema ni zaidi ya uvuvuzela.
Unatakiwa ukamuambie st.maalim seif na justa ladhu watoe tathmini ya kushindwa kwenu vibaya jimbo la uzini.
Kwa chadema hiyo 4% bado ni mafanikio makubwa na hiyo ni kengere ya hatari kwa ccm B.
Ni dhahiri kwamba wewe si wa gerezani kama ulivyokjuwa unatuaminisha.
Neno la kawaida sana kama hilo lisingekushinda, umeishia kubananga na huyo muarabu naye kabananga.
Kumbuka mtu makini. hata akifeli anajitathimini kwanini amefeli.
Sasa Chadema wanashindwa nini kuonyesha makosa ao hapa.
Kumbuka Ritz, Mtendaji mkuu aliweka kambi kule Uzini na akina Mbowe na wengine walitia timu nzito sana kule pasi na kusahau hapa barzani kila siku tulikuwa tunapewa update kuwa mambo mazuri uzini na ushindi ni dhwahir.
Sasa nashangaa iweje wapate 4%.
pasi na shaka kuna matatizo makubwa katika uongozi wao hususan katika kutoa tathmini.
naona leo hautatembe uchi kutoka Post mpaka Bunyokwa.
Kilichofanyika Zanzibar ni uharamia wala siyo uchaguzi. Huwezi kuuita uchaguzi huru na wa haki huku wanaoenda kupiga kura ukiwatisha, unaandikisha majina na kuwafuatilia. CDM, hawakushtuka mapema kwa nini maggamba walikuwa hawaongei sana kwenye huo uchaguzi!!
Dr. Barubaru,
Sasa tatembeaje wakati Chadema wamepata kura 281(4%) halafu wanasema wamejihidi.
Chadema ni chama cha kulalama kila wakti kinaonewa.
Hivi hata mkipewa kura za wale wote wasiopiga mngeweza kushinda?
Jipange na sio kuleta hoja za kuonewa.
Kumbuka mchawi wenu ni kauli zenu majukwaani na bungeni kuhusu waZnz na Znz kijumla.
Tumpe pole Padre Slaa kwa kuweka kambi na kuambulia 4%
Mwita,
Siasa za Znz ni zaidi ya unavyyozijua. Ndio maana hukumuona Jussa, maalim Seif hata mtatiro na Mh Juma Duni kuweka kambi kule. Kwani lile jimbo kwa vyovyote vile ni mali ya CCM.
Nikubainishie kidogo hata kama CCM wangeamua kuweka mgombea wake awe Jiwe au Pake na nyie wengine wekeni Bin'Adam basi juwa yule wa CCM laazima ashinde. Ndio maana CUF na vyama vingine hawakutumia nguvu kubwa kutafuta kiti hicho.
Chadema nafikiri utakubaliana na mimi kuwa Dr Padre Slaa aliweka kambi huko akiwemo na yule ndugu yetu Waitara na Heche na vijana wenziwe kwa takriban siku zote za uchaguzi ndio wameangukia pabaya zaidi ya ule uchaguzi wa 2010. Kwani 2010 walipata 7% na leo wamepata 4%.
Sasa nafikiri Chadema wajiulize je wamekuwa au ndio wamedebweda?
Huko ni kufaulu au kufeli ukilinganisha na nguvu walizotumia?
Nafikiri siku nyingine lazima wasome alama za nyakati kabla kukurupuka.
Dhambi ya ukabila na ukanda inasambaratisha Taifa na kuleta chuki kubwa miongoni mwa jamii na fitna kubwa kwa kizazi na kizazi. Mfano wake ni mauaji ya Kimbari kati ya wahutu na watusi.
Na vipi kuhusu dhambi ya Ukabila na ukanda?
Naungana na wewe mkuu wangu.Ukabila, Ukanda na Udini ni dhambi mbaya sana.Tukiungana pamoja tutatokomeza washenzi wa aina hii.Umeandika pointi nzuri sana mkuu.Hongera kwa kuliona hili mkuu wangu
Sasa kwa kuliona hilo naomba utambue hakuna udini wala chochote kuwa ni sababu ya Chadema kushindwa uzini Znz.
Bali mchawi wenu ni kauli zenu mlizokuwa mnazitoa majukwaani na bungeni kuhusu Znz na wazanzibar ndio zinawahukumu.
Hiyo ndio sababu kwa Znz zaidi ya 99% ya raia wake ni waislam.
funguka macho uone.
Kumbuka sitetei chama chochote hapa.Mimi nalaani matendo ya kishenzi ya kibaguzi kwa mtu au chama chochote.Nikuulize swali Vile vikaratasi vilivyobandikwa vya kubagua vyama kidini huko Uzini mpaka magazeti yakaripoti wewe unaona ni sawa?
Hizo ni mbinu tu za kisiasa. Mtu au chama chochote kinaweza kuweka na kuvisambaza kisiri ili kitengeneze njia ya ushindi wake au hata kupata sababu ya kushindwa kwake.
Kwa mantiki hiyo inawezekana hata Chadema walivisambaza kwa kuwa waliona kabisa wameshatangaza jimbo la uzini ni lazima washinde na kuwaarifu wanachama wao kupitia mitandaoni na magazetini wakti hali halisi ilikuwa lazima washindwe. sasa kutengeneza sababu za kushindwa kwao labda wanasambaza vikaratasi hivyo na kupata sehemu ya kutokea.
Kumbuka Chadema wametuamia zaidi ya milioni 70 pesa za kitanzania wakati CCM na vyama vingine havichamaliza hata milioni 10.
Ndio zinaitwa mbinu za kisiasa hizo.
Barubaru. Katika hali ya kawaida kufanya kampeni kubwa na kuishia kupata kura kiduchu ni kwamba mgombea hauziki. Lakini huko kwenu Zanzibar ni kinyume,ubora wa mgombea na sera siyo vigezo vya kuchaguliwa. Ushabiki na ubaguzi wenu kati ya CCM na CUF siyo tu umedumaza siasa za ushindani wa vyama bali kwa nyakati tofauti wagombea wazuri wamenyimwa kura na kuikosesha Zanzibar watu ambao wangeiletea maendeleo. Jiulize swali dogo, leo hii Dr. Shein ama Salim Hamed Salim wakigombea ubunge/uwakilishi huko kwao Pemba kupitia CCM wanaweza kupata kura ngapi?