Bila shaka kwa nguvu na Muumba tu wazima na harakati za kujenga maisha yetu pamoja na taifa kwa ujumla.
Leo nikiwa kama Mwalimu kitaaluma, naomba nizungumzie madai, lawama na kuhusishwa kwa kundi hili adhimu na siasa za nchi yetu.
Kwa kuanza naomba mtambue, Walimu sio watumishi kada mali ya wanasaisa, walimu hatuhusiki na umiliki wa chama chochote cha siasa nchini, so far. Kumekuwa na lawama, chuki na maneno ya kejeri kutoka kwa makada wa vyama vya siasa hasa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenda kwa Walimu haswa linapokuja suala la uchaguzi mkuu hapa kwetu.
Ipo hivi; imeonekana mara nyingi walimu wakipewa nafasi za kusimamia uchaguzi mkuu, naomba mtofautishe, mamlaka pekee nchini zenye kusimamia hili zoezi ni NEC, POLISI na Wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla, sio CWT wala chama chochote cha Walimu. Walimu sio wasimamizi, ni waendesha zoezi la kupiga kura, mwisho wa siku wao hufanya vile wanavyoelekezwa.
Vijana wa CHADEMA wamekuwa na kawaida ya kulaumu Walimu kuwa wanahusika na wizi wa kura ama kuisaidia CCM kuingia madarakani, jambo ambalo linashangaza, na linasikitisha ukizingatia CDM ndio chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, na mnajua ilivyo hadhi kubwa kuwa chama kikuu cha upinzani, hii ni sawa na kusema “chama mbadala wa chama tawala” kina kuja na hoja hii kwa kweli.
Walimu tunapata nafasi nyingi za kusimamia zoezi kulingana na wingi wetu katika kada, vile vile uzoefu wa kuratibu shughuli zinazohusisha watu wengi, uandishi na uzoefu katika kutoa maelekezo, mambo ambayo zoezi la upigaji kura linataka. Suala la kutumika na CCM halihusishi waalimu kaa sababu hakuna semina ya walimu kama walimu peke yake ya namna gani kura ziibiwe kituoni, ama waraka rasmi kwa Walimu kuhusu wizi wa kura. Na endapo itatokea mwalimu kama msimamizi wa kituo akafanya hivyo asihusishwe kama mwalimu kwa sababu hakutumwa kama Mwalimu, ualimu unahusiana vipi na wizi wa kura? Ni mtaala? Miiko ya kazi? Ama ni kitu gani.
NIONAVYO MIMI
CHADEMA huitumia hii hoja kwa namna mbili
1.SABABU YA KUPATA MTAJI WATU KISIASA Kwa kuwa Walimu ni kundi kubwa, wataka wawa “provoke” kwamba wao ndio sababu ya matatizo yote nchini pamoja na matatizo yao wenyewe lengo likiwa ni kuwafanya wawe subjects wao ambapo kwa madai haya maana yake Walimu kuyakataa itabidi wafanye matakwa ya CDM, kwa neno la kimombo wanaita “Blackmailing” yaani jitihada za kuwa prove wrong watu, Walimu wawape favor CDM.
Ndugu zangu CDM, kama kweli mnataka kuwa chama tawala nchi hii, acheni siasa za namna hii, changamoto katika utawala zipo kila kona duniani, fanyeni siasa yenu kama wanasiasa mnao jielewa, kumbukeni kundi mnalojaribu ku mess up nalo ni kubwa mno, lawama zikiwa nyingi zinakuwa sehemu ya maisha yetu, tukiwazoea hamtakuwa na mtaji wa watu huenda kama mnavyojaribu kutafuta kupitia sisi, dare not comrades!
2. KISINGIZIO BAADA YA KUSHINDWA UCHAGUZI
“Hata wakishinda wao, CCM itaunda serikali” nadhani mnamfahamu aliyesema hii kauli, kwa hiyo jueni kwamba mpo kwenye chi ambayo watu wana haki ya kupiga kura ila sio kuchagua viongozi, msilalamike lalamike hovyo kuwalaumu walimu as if sisi ndo tunaunda serikali, wapo walimu wengi tu makada wa vyama vya siasa ikiwemo chama chenu, amini usiamini kwa lawama hizi! (Sina neno)
”CCM itatumia dola kubaki madaraki” vile vile mnajua aliyesema hii kauli, hakusema CCM Itatumia Walimu kubaki madaraki, mkishindwa kuelewa na hapo basi hamjaamua tu na mnachuki na sisi za bure tu.
Mwisho kabisa naomba niwasihi muweke hadharani sera zenu kwa mtindo wa kuzidisha kutoa elimu zaidi hasa maeneo ya vijijini ambapo kuna ngoma kubwa sana ya chama tawala. Msiishie kutukana walimu, mbaya zaidi hamtulipi

mnazidisha hasira tu.
Nawasilisha.