Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 4,367
- 2,404
Si siri kuwa CHADEMA inauhusiano wa karibu au ni mwanachama wa Christian Democratic Parties duniani. Kuhudhuria kwa mwenyekiti wa BAVICHA katika mkutano wa CDU kule Ujerumani ni moja ya uthibitisho wa ukaribu huo. Lakini si kuhudhuria tu bali hata wanachama wa CHADEMA wakati huo waliandika hapa JF kuthibitisha ushirikiano na uhusiano wa CHADEMA na Christian Democratic Union cha Ujerumani. Wanachama hawakutueleza kinaga ubaga hasa ni nini idiolojia ya Christian Democratic Parties. Niliahidi kuandika mada kuhusu hili, na hii ni sehemu ya kwanza katika mfululizo wa sehemu 4.
Christian Democratic Parties DunianiChristian Democracy ni idiolojia ya kisiasa yenye lengo la kutumia misingi ya Kikristo katika tawala za jamii. Muundo huu ulizaliwa katika karne ya 19 huko Ulaya kwa ushawishi wa mafundisho ya Kikatoliki ya kijamaa pamoja na wale wenye mlengo wa kulia (Conservatism).
Kifupi, Christian democracy imekuwa na siasa kali zaidi katika maswala ya Tamaduni, jamii na moral issues pia inazingatia social markets economy katika upande wa uchumi.
Tukimnukuu Geoffrey K Robert na Patricia Hogwood wameandika " Christian Democracy has incorporated many of the views held by Liberals, conservatives and socialists within the wider framework of moral and Christian Principles". Aidha baadhi wanaenda mbali zaidi pale wanapoandika kuwa Vyama hivi vinaamini kuwa Serikali inaunda Mamlaka yake toka kwa Mungu na sio toka kwa watu.
Nguvu ya vyama vya kidemokrasia vya Kikristo Ulaya
Mtazamo wa kisiasa wa vyama vya Kidemokrasia vya Kikristo umetofautiana katika makali yake (conservatism) kutoka nchi moja hadi nyingine kutokana na umaarufu au uzito wa kanisa katika nchi husika.Kwa mfano vile vya Ulaya vina siasa za kati (moderate conservative), lakini nchi za Ujerumani, Uhispania na Belgium vyama hivi vina nguvu sana na ni conservative zaidi.Katika kipindi cha hivi karibuni (2000-2012) Vyama vingi vya kidemokrasia vya kikristo vimesota sana katika chaguzi kuu. Vingi vikiishia kupata 4-9% katika chaguzi kuu, vingine vikiishia kupata chini ya 3% na kushindwa kuingia Bungeni. Nchi ambazo vyama hivi vina nguvu na kushika madaraka katika miaka ya hivi karibuni ni Ujerumani (Christian Democratic Union- Bi Angela Merkel, kabla yake, Konrad Adenauer, Helmut Kohl), Italia- (Giulio Andreotti-PM, Giorgio La Pira, Aldo Moro-PM, Adone Zoli-PM.), Uhispania (Mariano Rajoy-PM).
Nafasi ya CHADEMA
Maswali mengi, watanzania tunapaswa kujiuliza, hivi CHADEMA inapokwwenda katika mikutano kama hiyo inakuwa na ajenda gani na inajifunza nini? Je ni idiolojia ya principles za kikristo ndio tuzitarajie itapochukua madaraka? Hivi ni makosa kukiita chama hicho kuwa ni cha kidini.
Waswahili wanasema niambie rafiki zako ni akina nani, nitakueleza wewe ni nani? Marafiki wa CHADEMA ndio hao nafikiri si vigumu kwa watanzania kukielezea kinaga ubaga kuwa hiki ni chama cha aina gani.
Sehemu ya pili itaelezea Historia ya chimbuko la vyama vya Kikristo.
Christian Democratic Parties DunianiChristian Democracy ni idiolojia ya kisiasa yenye lengo la kutumia misingi ya Kikristo katika tawala za jamii. Muundo huu ulizaliwa katika karne ya 19 huko Ulaya kwa ushawishi wa mafundisho ya Kikatoliki ya kijamaa pamoja na wale wenye mlengo wa kulia (Conservatism).
Kifupi, Christian democracy imekuwa na siasa kali zaidi katika maswala ya Tamaduni, jamii na moral issues pia inazingatia social markets economy katika upande wa uchumi.
Tukimnukuu Geoffrey K Robert na Patricia Hogwood wameandika " Christian Democracy has incorporated many of the views held by Liberals, conservatives and socialists within the wider framework of moral and Christian Principles". Aidha baadhi wanaenda mbali zaidi pale wanapoandika kuwa Vyama hivi vinaamini kuwa Serikali inaunda Mamlaka yake toka kwa Mungu na sio toka kwa watu.
Nguvu ya vyama vya kidemokrasia vya Kikristo Ulaya
Mtazamo wa kisiasa wa vyama vya Kidemokrasia vya Kikristo umetofautiana katika makali yake (conservatism) kutoka nchi moja hadi nyingine kutokana na umaarufu au uzito wa kanisa katika nchi husika.Kwa mfano vile vya Ulaya vina siasa za kati (moderate conservative), lakini nchi za Ujerumani, Uhispania na Belgium vyama hivi vina nguvu sana na ni conservative zaidi.Katika kipindi cha hivi karibuni (2000-2012) Vyama vingi vya kidemokrasia vya kikristo vimesota sana katika chaguzi kuu. Vingi vikiishia kupata 4-9% katika chaguzi kuu, vingine vikiishia kupata chini ya 3% na kushindwa kuingia Bungeni. Nchi ambazo vyama hivi vina nguvu na kushika madaraka katika miaka ya hivi karibuni ni Ujerumani (Christian Democratic Union- Bi Angela Merkel, kabla yake, Konrad Adenauer, Helmut Kohl), Italia- (Giulio Andreotti-PM, Giorgio La Pira, Aldo Moro-PM, Adone Zoli-PM.), Uhispania (Mariano Rajoy-PM).
Nafasi ya CHADEMA
Maswali mengi, watanzania tunapaswa kujiuliza, hivi CHADEMA inapokwwenda katika mikutano kama hiyo inakuwa na ajenda gani na inajifunza nini? Je ni idiolojia ya principles za kikristo ndio tuzitarajie itapochukua madaraka? Hivi ni makosa kukiita chama hicho kuwa ni cha kidini.
Waswahili wanasema niambie rafiki zako ni akina nani, nitakueleza wewe ni nani? Marafiki wa CHADEMA ndio hao nafikiri si vigumu kwa watanzania kukielezea kinaga ubaga kuwa hiki ni chama cha aina gani.
Sehemu ya pili itaelezea Historia ya chimbuko la vyama vya Kikristo.