Chadema msimwache kijana huyu

invito

New Member
May 18, 2012
3
1
Kati ya Vijana SHUJAA,MAHIRI na MAKINI katika mambo ya SIASA tulioweza kuwashuhudia katika uchaguzi wa Urais,Ubunge na Madiwani mwaka 2010 nchini Tanzania Amani Mwaipaja ni mmoja wapo. Kijana huyu aligombea Ubunge Jimbo la MOrogoro Mjini kwa Tiketi ya CHADEMA na kushika nafasi ya pili akimwacha Mgombea wa CUF Abeid Mlapakolo katika nafasi ya Tatu.

Nimejaribu kufuatilia historia yake ingawa haifahamiki kwa wengi lakini Amani Mwaipaja ana digrii ya sheria ya chuo kikuu Mzumbe, mratibu wa miradi mbalimbali ya Kijamii na ni mwanaharakati wa haki za Binadamu.

Kwa wananchi wa Morogoro wengi walikuwa hawamfahamu mpaka pale alipogombea Ubunge na kuonesha kiwango kikubwa sana alipokuwa jukwaani kipindi cha Kampeni, kusema ukweli, kwa siasa sa Morogoro Kijana huyu aliionesha ushindani mkubwa sana ingawa inawezekana hakupata sapoti kubwa kutokana na kuwa mgeni machoni pa wengi au kushindwa kufika maeneo mengi wakati wa kampeni kutokana na changamaoto ya fedha lakini ni potential sana huyu kijana

Nimekuwa pia nikufuatilia makala zake kwenye magazeti ya mwanahalisi na magazeti mbalimbali na kugundua kuwa ana uwezo mkubwa katika kufikiri isipokuwa hatumiki sawasawa kwa mfano, Amani Mwaipaja amekuwa akiendesha semina mbalimbali kwa jamii na vyuo na hata anaposhiriki katika mikutano ya Hadhara bado naonesha umahiri mkubwa sana wa kushawishi watu isipokuwa hatumiki sawasawa

Nakumbuka lile sakata la maaskari wanaoshirikiana na majambazi mkoani Morogoro huyu ndiye aliyekuwa mstari wa mbele katika kuandaa nyaraka mbalimbali akimsaidia askari jeshi aliyeamua kuweka uozo wa jeshi la Polisi Morogoro Hadharani ajulikanaye kwa jina la Dunga au afande Donald.

Sakata la afande Donald ndilo lililopekea akina SABA SITA NA WENZAKE kuhamishwa Morogoro (Source:Waraka uliosambazwa na Afande Donald kwa wananchi-Morogoro). Hiyo ni kazi ya Amani Mwaipaja ambaye hakuogopa vitisho vya akina Sabasita,alisimama kidete na tunaambiwa hata IGP Mwema alipounda Tume ya kuchunguza madai ya askari huyo alisindikizwa na Amani Mwaipaja akiwa kama mwanasheria mshauri.

Juzijuzi Amani Mwaipaja ametajwa tena na Afande Sele alipokuwa akihojiwa na Clouds Radio kuwa ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumsaidia mwanzo mpaka mwisho pale Afande Sele na Twenty Percent walipokuwa Rumande,watanzania wote walisikia.

Amani Mwaipaja huyu wiki chache zilizopita ameonekana kwenye Runinga mbalimbali ikiwemo ITV na TBC akitoa maoni kuhusu mabadiliko ya Baraza la Mawaziri.

USHAURI wangu kwa CHADEMA Ni kwamba:

Iandae utaratibu wa namna ya kuwapangia majukumu hawa vijana wanaoonekana kuwa potential katika Chama badala ya kuwatumia wale tu ambao tayari ni wabunge au wana nafasi fulani makao makuu,

Kwa mkoa kama wa Morogoro ambao unahitaji nguvu ya ziada katika kuhamasisha na kujenga chama ISIACHE kuwatumia vijana kama hawa

Mzalendo: Chuo Kikuu Sokoine-Morogoro
 
Unapozungumzia CHADEMA hao wakina Mwaipaja ndio CHADEMA au kuna CHADEMA nyingine nisiyoijua mimi?
 
Hapo Umenena Invito, Amani Mwaipaja ni moja kati ya potential kubwa sana ya Chadema kwa upande wa Morogoro Mjini isipokuwa wana Morogoro bado hawajajua,labda wanasubiri operesheni sangara ije iwafumbue macho...napita tu
 
Chadema ipo hiyohiyo moja,isipokuwa CAHDEMA Kama chama kinapaswa kuwatengeneza hawa vijana badala ya kuwaacha na kuendekeza majungu hasa kwa upande wa Chadema jimbo la Morogoro Mjini,viongozi waliopo hawaendani na kasi ya CHADEMA Tunayoijua, wengi wamekalia majungu na kuwavunja mioyo watu wanaoonekana wanaweza,sijui wanatumwa na CCM?:israel:
 
Leo nilikuwa napita morogoro nimesikia nyimbo za CDM, sijui kuna nini. nafuatilia. inaonekana Moro inabadilika kwa kasi fulani.
 
I do support this idea of using youth to bring changes we Tanzanians badly need.
 
ushauri huo ni mzuri sana hasa kwa maendeleo ya chama na faida ya taifa kwa ujumla.nina imani 2015 kila kitu kitakuwa sawa sawa.pia ni rai yangu kwa vijana wote waliofunguka kuwa watumike kwa ukombozi wa pili wa nchi yetu baada ya ule wa kwanza wa 1961
 
I appreciate Amani's efforts, and of coz am wishing him best success. Invito and Amani, take this:
1) One must learn to grab an opportunity
2) Luck favors the brave. So be courageous to go those extra miles
 
amani z.jpg
Kijana Amani Mwaipaja akiwa na Doctor Slaa jukwaani,
 
ni wazo zuri kwa maendeleo ya na mabadiliko ya moro. Vichwa km hivi lazima tuvitumie na imani ya jf hili litachukuliwa na wahusika.
 
amani j.jpg
Moja ya picha Amani Mwaipaja akiwa na Dokta wa Ukweli,hapa ilikuwa wakati wa ziara ya Dr. mikoani kuomba kura za udhamini kama mnakumbuka
 
Kila mwenye nia njema, na mwenye dhamira ya kweli ya kuikomboa Tanzania tunayoitaka lazima ataipenda CHADEMA.
 
Usemayo Mungi ni kweli tupu, uzuri wa huyu jamaa ni kwamba ni mtu wa kujishusha sana na ana heshimu watu wote,kama ni kujifagilia basi wana morogoro walipaswa kujifagilia
 
Back
Top Bottom