CHADEMA 'mnazingua'

huyu ni lawyer? aiseeeeeeeeeeeeeeeee.

 
Asante Mkuu kwa mchango wako mujarabu.
 
Petro E. Mselewa: Hoja yako ni nzuri, ila nawaza huko kujijenga kwenye vijiji na kata kutawezekana? Maana wameambiwa siasa ni mpaka 2020. Sioni dalili ya dola kuwaruhusu Chadema kulifanyia kazi wazo lako.
 
Pole sana Wakili, Chadema mbona walianza kuzingua toka kubadili gia ya hewani kwa sasa ni wazinguaji sugu. Sijui kama ulijiandaa kuogeshwa matusi na wazinguaji maana ndicho walichobakiza
 
Countrywide: Watanzania wengi hawana nyenzo za kuwawezesha kuwa twitter, facebook, n.k. wote ambao wako huko mnakosema tayari wanaziona hoja za Chadema na upinzani kwa ujumla. Waliobaki ndo hao wa katani na vijijini ambako mwenye nchi kawakataza. Ila mbona naona kama watanzania na hata wasomi hawaoni kinachoendelea kwenye siasa za nchi yetu? Inasikitisha sana!
 
Ukila na kipofu usimshike mkono...
Hii staili ya CDM ya kuwaacha "watawala uchwara" wajiendee wanavyopenda ni bora kuliko..!!
 
Mwanasheria uchwara katika ubora wake. Hivi wewe hujui kama uchaguzi hauko uhuru na wala si wa haki!? Unadhani ni kwanini Serikali dhalimu haitaki katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi?

Hoja zipi wewe ambazo huziamini? Wapi ungejua kwamba zero brain kachota trillions hazina bila idhini ya Bunge? Wapi ungejua kwamba ndege imeshikwa kutokana na deni la $38.7 million? Kama siyo kupitia Chadema?

Huku kukamatwa kamatwa kwa Wabunge wa Chadema na sasa kuwindwa maisha yao kwa mtutu wa bunduki.

Uanasheria wako unatia shaka kwa kuandika pumba bila kutilia hali halisi ya kisiasa nchini pamoja na hayo bado Chadema inaibua issues mbali mbali za kifisadi ndani ya Serikali hii dhalimu

 
Tony antony: Kwa hiyo huyo baba unataka kutwambia hajui kwamba anakosea hadi aambiwe na mahakama? Hivi kuna mahakama TZ ya kumwambia huyu baba kwamba amekosea? Labda mahakama za wenzetu Kenya.
 

Huyo jamaa Petro E. Mselewa SIO Lawyer, ,,labda bushlawyer tena ni mbeba mafaili tu,

humu labda anaefaa kujiita Lawler ni barafu , ,japo yeye ni zao la Wazee wa kaunda suti, l
 
Sidhani kama anapata wateja huyu!
 

CHADEMA ilipotea mwaka 2015 kwa sababu tunazozijua ni FACT.

Hata hivyo wafia CHADEMA hawaikubali hii FACT.
 
KAMA 2015 ILIKUWA NDIO ANGUKO LAO, MBONA MNATAKA KUWAPUNGUZA KWA RISASI HUKU MKIWA MMEWAZUIA KUONGEA NA WANANCHI
 

eti ndio mwanasheria huyo,,,labda Lawler Wa walevi wa mnazi na gongo
 
Kwani mtu kuwa lawyer anapaswa aweje?

Anapaswa awe na mawazo na mitazamo kama yenu kwa asilimia 100?

Watu wa ajabu sana nyie.
 
Kama kuvaa T-shirt tu yenye jina la kiongozi wa chama cha upinzani unakamatwa itakuwaje kwa yule atakayepita mitaani kutangaza mkutano wa hadhara wa chama cha upinzani? Tuwalaumu kwa mengine na siyo hili. Halafu binafsi huwa najiuliza, je, ina maana hata wasomi kama Mselewa huwa wana mawazo kwamba upinzani upo kwa faida ya wapinzani wenyewe? mimi najua upinzani ni afya kwa Taifa zima. Hivyo kwa vile ni kwa faida yetu sote basi iwe ni wajibu wa sisi wote kulilia uwepo wa watu wenye mawazo mbadala (wapinzani)
 
Kwani mtu kuwa lawyer anapaswa aweje?

Anapaswa awe na mawazo na mitazamo kama yenu kwa asilimia 100?

Watu wa ajabu sana nyie.
One expects a highly reasoned argument from a lawyer since a lawyer is a philosopher!
 
Petro, utakosa wateja, nina mashaka na uwakili wako! Training yako etc...... take time to read and think before posting!
Wateja wa nini? Sema sitakuwa na marafiki walio tayari kusikia ukweli. Hatuna muda wa kupindisha mambo,CHADEMA inazingua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…