sixgates
JF-Expert Member
- Mar 19, 2011
- 3,979
- 1,662
Siku za karibuni tumeshuhudia ushindani, kuchachafiana katika hatua ya kura za maoni katika ngazi ya Ubunge na Udiwani kupitia CCM. Tanzania nzima imekuwa ikifuatilia mchakato huu kupitia vyombo vya habari na mitandaoni hadi sasa “Wajumbe” wamejizolea umaarufu kutokana na mchakato mzima. Binafsi nimegundua mapungufu kadhaa katika mchakato wa kura za maoni kwa CCM, lakini ni details ndogo na zina nafasi ya kurekebishwa kwa sababu bado mchakato unaendelea.
Kwa upande wa CHADEMA, hata tukiuliza hapa hivi kuna aliejua mchakato ulivyoenda, haki tutapata wale ambao ni wanachadema ambao nao walikuwa na interest, ila kura za maoni za CCM hadi mtoto mdogo anajua kwa sababu kwanza umekuwa wa wazi sana, pili kupitia ofisi ya mwenezi wamewazidi maarifa Chadema kwa kutengeneza umaarufu na momentum kwa zoezi lao na kwa hakika wamejinadi hata kabla ya octoba wakati chadema wanajifungia hawaoni umuhimu wa kuwekeza kwenye (publicity). Wanatumia muda mwingi kutengeneza matukio ili kupata free public stunt.
CHADEMA mmekubali kujifungia na kuzuia haki ya watanzania kuona namna mchakato wa kura za maoni katika nafasi za ubunge na udiwani ndani ya Chadema zinaendaje.. hakuna uwazi na ni hatari, mmepanda upepo mtavuna tufani. Ujanja ujanja uliotokea kwa Meya Boniface Jacob kuwa mgombea ubunge hapo Ubungo, Chadema imepasuka, hatashinda. Viongozi wa chadema wekeni miguu chini, sikilizeni wanachama. Haiwezekani chama kichanga kama cha ACT wazalendo kimefanikiwa kutengeneza mchakato wa kura za maoni katika chama chao ziwe wazi nyie wenye miongo zaidi ya miwili mnaogopa kuuweka mchakato wazi. Ni ushauri, mwenye masikio na asikie.
Kwa upande wa CHADEMA, hata tukiuliza hapa hivi kuna aliejua mchakato ulivyoenda, haki tutapata wale ambao ni wanachadema ambao nao walikuwa na interest, ila kura za maoni za CCM hadi mtoto mdogo anajua kwa sababu kwanza umekuwa wa wazi sana, pili kupitia ofisi ya mwenezi wamewazidi maarifa Chadema kwa kutengeneza umaarufu na momentum kwa zoezi lao na kwa hakika wamejinadi hata kabla ya octoba wakati chadema wanajifungia hawaoni umuhimu wa kuwekeza kwenye (publicity). Wanatumia muda mwingi kutengeneza matukio ili kupata free public stunt.
CHADEMA mmekubali kujifungia na kuzuia haki ya watanzania kuona namna mchakato wa kura za maoni katika nafasi za ubunge na udiwani ndani ya Chadema zinaendaje.. hakuna uwazi na ni hatari, mmepanda upepo mtavuna tufani. Ujanja ujanja uliotokea kwa Meya Boniface Jacob kuwa mgombea ubunge hapo Ubungo, Chadema imepasuka, hatashinda. Viongozi wa chadema wekeni miguu chini, sikilizeni wanachama. Haiwezekani chama kichanga kama cha ACT wazalendo kimefanikiwa kutengeneza mchakato wa kura za maoni katika chama chao ziwe wazi nyie wenye miongo zaidi ya miwili mnaogopa kuuweka mchakato wazi. Ni ushauri, mwenye masikio na asikie.