CHADEMA mnampuuza Mbowe!

CHADEMA mnampuuza Mbowe!

Nape Nnauye

MP Mtama
Joined
Dec 26, 2012
Posts
99
Reaction score
408
Mhe. Mbowe akiwa Mbeya alikiri wazi kuwa CHADEMA kwa miaka yote tangu kuanzishwa kwake kimekuwa ni chama cha HARAKATI... Lakini nilifurahi kusikia akiwaomba wenzake kuwa sasa ni wakati wa kukibadili Chama chao kutoka chama cha harakati na kuwa sasa chama cha SIASA.

Sasa ni karibu miezi mitano tangu atangaze na kuwasilisha ombi hili kwa wenzake lakini kwa masikitiko makubwa wenzake mmempuuza mwenyekiti wenu, badala ya kukibadilisha chama sasa mnakifanya cha harakati zaidi mpaka sasa mnapanga na kutekeleza kudhuru watu hasa wasiowaunga mkono.

Kumpuuza Mbowe kwenye wito wake huo ni kifo chenu na hivyo kuathirika kwa demokrasia nchini. Uwepo wenu umeleta joto zuri kwenye siasa na demokrasia nchini ukiachilia mbali vibweka vya baadhi ya viongozi wenu. Lakini nadhani sio tatizo la chama bali la viongozi wachache waliofanya CHADEMA kichaka cha kufichia rangi zao halisi.

MTAKAO CHANGIA PUNGUZENI MAPOVU NA MATUSI MJENGE HOJA.
 
Unafikiri wewe unaweza ukawa msemaji wa Mbowe leo baada ya jana kuongoza timu ya kumtukana sana Igunga ikiongozwa na wewe na Mwampamba?

Unafikiri kuwa ukiandika hivyo ndio unafuta yale matusi ya jana? Nafikiri unafiki ndio sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa CCM ndio maana baada ya matusi jana leo unakuja hapa kumsifia Mbowe, ndugu yangu punguza huo unafiki kwani ni jambo baya sana ...

Ni ushauri wangu tu kwako, maana nimejikuta nakusikitikia sana .
 
Hayo ni unayoyasema mbele za watu, lakini Moyoni Mwako unakiri kwa dhati kuwa CCM ina Hali mbaya na kwamba 2015 kazi ipo

Katika kila ulifanyalo kumbuka mwisho wa siku 'Wananchi ndio watakao piga kura' na ukweli uko wazi kwamba wananchi wanaoiunga Mkono Chadema wanaongezeka kwa speed kali, Yaani kimahesabu "Exponential Function"
 
Wewe nawe kituko, kutoka kwa watu kama Lissu wenye historia ya kifafa unategemea siasa? Haya majitu yaacheni hivyo hivyo ili vichaa nao wapate vyama vya kuongoza.
 
Unadhihirisha udhaifu zaidi katka ccm na serikali yenu. Maana ya ccm yamekuwa magumu kuyatatua hvy unakimbilia kuibua hoja za kitoto dhidi ya mbowe. Umepotea kwa hilo.
 
Naunga mkono hoja, chadema badilikeni muwe watetezi wa haki
 
Nape,ninajua wazi kuwa moyoni mwako na pia ukiwa uvunguni,unakiri fika kuwa kwa mwendo wa CCM mbele ni giza nene.Japo hadharani huwezi sema.
Pole sana,kwani hapa Igunga mmevuna aibu,shahidi ni mmi mwenyewe.
 
Nape, matatizo ya Tanzania ni umaskini uliokithiri unaotokana na uvivu wa kufikiri wa ninyi mnaoiongoza nchi hii kupitia chama chenu CCM. Badala ya kubuni na kupanga mikakati ya kutumia raslimali za nchi kuwaletea maendeleo wewe na wenzako mnawaza namna ya kuiba kura, kurubuni wapiga kura kwa wali, kofia na kanga! mbaya zaidi ni kwamba sasa Nape unatumia nguvu kubwa na hila kuhujumu vyama vya upinzani hasa CHADEMA badala ya kupanga mikakati ya kutimiza na kutekeleza ilani ya chama chenu! Kama kijana kama wewe ambaye unategemea kuchukua nchi kutoka kwa akina Kikwete unakuwa na mtazamo wa kuku kuona usawa wa mdomo wake, tutegemee maendeleo kweli? Akili yako imekwama kwenye kuandaa njama za uchaguzi na sio maendeleo ya watanzania!Laana ya umaskini wa watanzania iangukie kichwani mwako na uishie kuwa katibu muongo wa CCM wala usipande zaidi ya hapo!
 
Inasikitisha kuaona kiongoza wa chama kilichopo madarakani kama wewe unakuwa hauna busara kiasi hiki.Hii inaonesha ni jinsi gani mara nyingi haushirikishi ubongo ambao umepewa bure kabisa.inasikitisha na kutia shaka kama uwezo wako wa kufikiri uko sawa pale unapoamua kusema watu wasitokwe na POVU kama unajua ni watu wana mapovu pindi waongeapo.jitahidi kusimama kama kiongozi wa taifa kwan vijana kama sisi wenye chini ya miaka 24 tunajifunza kutoka kwa watu makini.
 
Chadema si chama cha harakati bali ni chama cha siasa za kweli na kina cho aminika na ndio maana kila leo huwezi kuongea bila kukitaja, kama kingekuwa cha harakati tuu wala kisinge kukosesha usingizi namna hii

hivi jk alipo sema mmuache kutegemea polisi mbona hamkuacha hadi mkawatumia kufungua case ya kigaidi hadi mka mdharirisha DPP?

Hivi filikunjombe alipo sema kuwa wenzio waache kufanya kazi zako mbona hawajaacha hadi sasa kiasi kwamba una kosa cha kusema?

Pia mangula aliposema atapambana na mafisadi hadi leo yapo na wewe ulisema pia.
 
Nakushauri achana na Chadema kabisa.Kila dakika unahangaika na Chadema kana kwamba wewe ni Katibu Mwenezi wa Chadema.

Umemporomoshea matusi ya nguoni Mbowe jana kule Igunga unadhani Chadema haijui.

The best thing for you to do now ni kujiandaa kisaikolojia kuipisha Chadema Ikulu 2015
 
Tangu lini katibu wa itikadi na unezi wa ccm kawa msemaji wa Chadema, ama ndio mdogomdogo unaomba ajira upande wa pili baada ya kugundua kwako kunazama.

Ila tu kwa sasa labda ccm ndio chama ambacho kinapoteza/kimepoteza hadhi ya kuwa chama cha siasa hapa Tanzania, lakini vingine kikiwemo Chadema kama ulivyokitaja ni chama cha siasa na kinafanya siasa na umma unajua hivyo, ila hiyo ccm yako mmhh, sijui kama kuna tone la siasa ndani yenu kwa sasa.

Kama ccm inafanya siasa basi ni siasa chafu, ambazo huwezi kuziweka hazarani ama mbele ya umma.
 
Mhe. Mbowe akiwa Mbeya alikiri wazi kuwa CHADEMA kwa miaka yote tangu kuanzishwa kwake kimekuwa ni chama cha HARAKATI... Lakini nilifurahi kusikia akiwaomba wenzake kuwa sasa ni wakati wa kukibadili Chama chao kutoka chama cha harakati na kuwa sasa chama cha SIASA.

Sasa ni karibu miezi mitano tangu atangaze na kuwasilisha ombi hili kwa wenzake lakini kwa masikitiko makubwa wenzake mmempuuza mwenyekiti wenu, badala ya kukibadilisha chama sasa mnakifanya cha harakati zaidi mpaka sasa mnapanga na kutekeleza kudhuru watu hasa wasiowaunga mkono.

Kumpuuza Mbowe kwenye wito wake huo ni kifo chenu na hivyo kuathirika kwa demokrasia nchini. Uwepo wenu umeleta joto zuri kwenye siasa na demokrasia nchini ukiachilia mbali vibweka vya baadhi ya viongozi wenu. Lakini nadhani sio tatizo la chama bali la viongozi wachache waliofanya CHADEMA kichaka cha kufichia rangi zao halisi.

MTAKAO CHANGIA PUNGUZENI MAPOVU NA MATUSI MJENGE HOJA.

-Una audacity ipi ya kutoa ushauri kwa CHADEMA wewe?

-Kama CHADEMA kitaathirika kwa namna yoyote kwa mujibu wa mtazamo ulioueleza si ndiyo utafurahi zaidi?Next time ukiandika hapa uwe unafanya hivyo kama msomi.

-Political state ya CHADEMA kama chama cha siasa unaweza vipi kuitofautisha na political activism?Unaweza vipi kui-distinguish kwa kutumia ITIKADI ya chama hiki?

-Next time usiwe unatutia aibu vijana wenzako kwa kuandika andika tu ilimradi uonekane active.

-Hizo siasa za kudhuru watu ni zipi.Ni jambo la ajabu kabisa badala ya kunadi itikadi na sera za chama chako wewe unanadi udaku na majungu.Ndiyo siasa mpya zilizoletwa na vijana huko kwenye chama chako?Usiharibu Taswira ya vijana wa taifa hili kwa uzembe na udhaifu unaouonyesha katika kuitumikia dhamana uliyopewa na chama chako

-Umeachana na mradi wa kuzunguka kumtukana yule waziri mkuu aliyejiuzulu sasa unajaribu kutafuta umaarufu wa bei rahisi kupitia CHADEMA.Najua mfumo wa majimbo ni kitanzi kwenu,mna kazi ngumu sana sana.Get prepared!
 
Back
Top Bottom