CHADEMA mna mpango gani na majimbo haya ya Kigoma?

CHADEMA mna mpango gani na majimbo haya ya Kigoma?

oneblood

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2011
Posts
244
Reaction score
51
Kimsingi sielewi tatizo ni nini ama Waha tumeikosea nini Tanzania na CHADEMA, wote tunatambua juhudi kubwa za wanakigoma katika kuyapokea mageuzi ya kisiasa hapa nchini kwani tangu vyama vingi vianzishwe mkoa wa Kigoma ulikuwa wa kwanza kutoa mbunge wa upinzani nchini,na kwa sasa mkoa mzima CCM wanamajimbo 3 kati ya majimbo 7 ya uchaguzi.

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba mkoa mzima hasa katika majimbo ya Muhambwe, Kakonko, Kasulu mjini na Kigoma mjini kote huko wananchi wanaipenda,kuikubali na kuiamini CHADEMA,na hata wabunge waliopo sasa Machali, Mkosamali, Mama Buyogela, Chiza na Serukamba walishinda either kwa kuiba kura (Chiza Kakonko na Serukamba Kigoma mjini )hawa waliiba kura na baadhi yao ninaushahidi wa kuaminika.

Kwa majimbo yaliyobaki NCCR MAGEUZI walishinda si kwa kuwa wanakubalika kama chama bali ni wananchi kukosa mgombe mbadala toka CHADEMA, Kwa mfano jimbo la Muhambwe na manyovu,japokuwa yapo madai ya watu wa CHADEMA kununuliwa na wale wa CCM,Majimbo yale yanayomilikiwa na vyama tofauti na CHADEMA wabunge wao wanakazi ya ziada kuweza kushinda isipokuwa kwa Kafulila tu ambaye nae kunatarifa zisizo Rasmi kutafta namna ya kurudi CHADEMA yeye na Nakaya na mpango huo unaratibiwa na mmoja wa viongozi wa CHADEMA.

Wakuu pamoja na hayo yote nasikitika kusema ni kama viongozi wa CDM kitaifa wametutelekeza wakazi wa Kigoma na mkoa kwa ujumla,naweza nikasema kwa uhakika makao makuu inahusika katika hili,kwani tangu uchaguzi mkuu wa 2010 hakuna kiongozi yoyote wa chama makao makuu aliewahi kufika hukokwa ajili ya kuimalisha chama yofauti na Zitto ambaye anaenda kama mbunge jimboni kwake

Kwa mfano watu wa huku wanampenda na kumkubali dk Slaa kuliko hata Zitto lakini hakuna harakati zozote za kuukomboa mkoa wa kigoma kutoka kwenye makucha ya CCM,viongozi wa makao wapo bize na kaskazini tu hasa Arusha inauma kwa kweli,tuseme sasa Arusha inatosha twende kigoma jamani,Viongozi wa sasa wa CDM waliopo Kigoma japokuwa wamekitoa mbali chama lakini kwa sasa wamechoka kifikra na kukata tamaa ni rahisi kununulika mfano katibu wa CDM mkoa na Mwenykiti wa CDM wilaya Kibondo mwalimu Ndidyicha huyu amebaki na kazi ya kujipendekeza kwa mkuu wa wilaya hiyo bwana Mwamoto wakati CDM wilaya nzima haina hata ofisi hai ya kupanga wala wanayoimiliki.

Zitto kabwe nae hana msaada wa kisiasa katika mkoa,kwani kwa jina lake na nguvu alizokuwa nazo kisiasa ilikuwa ni jambo la ajabu sana mkoa mzima akashinda yeye tu tena kwa mbinde na ni baada ya dk Slaa kurudi jimboni mwake kupiga kampeni upya,kama haitoshi mpaka sasa hajafanya hata ziara moja ya kuimalisha majimbo mkoani humo hii ni aibu kwani Charity begins@home,wito kwa mwenykiti wetu mbowe akumbuke jimbo la muhambwe la mkosamali alilipoteza baada ya Kumnyima fedha za kampeni dogo mkosamali wakati akijua wazi kuwa bado mwanafunzi wa SAUT ,dk Slaa nakuamini fanyia kazi hili
 
  • Thanks
Reactions: MC
Viongozi wa CHADEMA msikilizeni mwanaCHADEMA mwenzenu nendeni Mkoa wa Kigoma mkoa ulioonyesha mfano wa kupenda mageuzi munataka wananchi watoe machozi ya damu ndio muende nilienda kasulu mjini Kikazi,hata mimi nilisikia vijana wananiambia wanapenda sana kumuona Mnyika kwenye kihoteli nilichofikia nadhani wakati umefika sasa viongozi kuzungukia maeneo ambayo wananchi wanawahitaji
 
Viongozi wa CHADEMA msikilizeni mwanaCHADEMA mwenzenu nendeni Mkoa wa Kigoma mkoa ulioonyesha mfano wa kupenda mageuzi munataka wananchi watoe machozi ya damu ndio muende nilienda kasulu mjini Kikazi,hata mimi nilisikia vijana wananiambia wanapenda sana kumuona Mnyika kwenye kihoteli nilichofikia nadhani wakati umefika sasa viongozi kuzungukia maeneo ambayo wananchi wanawahitaji

kweli mkuu mkoa mzima wanaipenda na kuikubali CDM tatizo uongozi wa mkoa na kitaifa makao makuu hawataki kpeleka harakati za kisiasa kule.
 
Makamanda wetu pliz sikilizeni hiki kilio. Huu sio muda wakupoteza. We need these guys to go. Dr slaa sasa hv utakua umepunguziwa majukumu nenda kaweke kambi
 
mleta mada unataka umaa ukuamini wakati unadanganya.majimbo ya kigoma ni manane na si saba kama ulivyodai.majimbo hayo ni kigoma mjini(serukamba)kigoma kaskazini(zitto)kigoma kusini(kafulila)kasulu njini(machali)kasulu vijijini(buyogera) kasulu manyovu(obama)kibondo mjini(mkosamali) kakonko(chiza).pia kuhusu kukubalika kwa zitto sijui we unatokea kigoma sehem gani ?zitto ni Rais wa kgm na nchi nzima kwa ujumla.kuhusu zitto kuikomboa kigoma kila mwanakigoma anakili kuwa zitto ndio kaupigania kigoma.na kakijenga chama maeneo yote.mfano miezi kadhaa iliyopita zitto kafanya mikutano wilaya ya kasulu,uvinza,Buhigwe,kigoma kaskazini na kafanya mara nyingi kigoma mjini.lkn tambua kuwa Zitto anamajukumu mwengi ya kitaifa.kwanza ni Naibu katibu mkuu wa chama chake,mbunge wa kigoma kaskazini,naibu kipngozi wa kambi ya upinzani,mwenyekiti wa hesabu za serikali,mwandishi wa makala mbalimbali magazetini,pia anafanya Phd.yake.mwogope mandela wa Tanzania mzalendo aliejitolea maisha yake kutupigania watanzania.
 
mleta mada unataka umaa ukuamini wakati unadanganya.majimbo ya kigoma ni manane na si saba kama ulivyodai.majimbo hayo ni kigoma mjini(serukamba)kigoma kaskazini(zitto)kigoma kusini(kafulila)kasulu njini(machali)kasulu vijijini(buyogera) kasulu manyovu(obama)kibondo mjini(mkosamali) kakonko(chiza).pia kuhusu kukubalika kwa zitto sijui we unatokea kigoma sehem gani ?zitto ni Rais wa kgm na nchi nzima kwa ujumla.kuhusu zitto kuikomboa kigoma kila mwanakigoma anakili kuwa zitto ndio kaupigania kigoma.na kakijenga chama maeneo yote.mfano miezi kadhaa iliyopita zitto kafanya mikutano wilaya ya kasulu,uvinza,Buhigwe,kigoma kaskazini na kafanya mara nyingi kigoma mjini.lkn tambua kuwa Zitto anamajukumu mwengi ya kitaifa.kwanza ni Naibu katibu mkuu wa chama chake,mbunge wa kigoma kaskazini,naibu kipngozi wa kambi ya upinzani,mwenyekiti wa hesabu za serikali,mwandishi wa makala mbalimbali magazetini,pia anafanya Phd.yake.mwogope mandela wa Tanzania mzalendo aliejitolea maisha yake kutupigania watanzania.

Naona unachanganya mada mkuu Zitto hapa nimemhusisha katika suala la kutoimalisha chama mkoa huku nikifanya political reference na nguvu alizokuwa nazo mwaka 2010na bado tukapoteza viti vingi kimkoa na pamoja ya nguvu alyonayo ambayo wewe unataka kutuamisha kwamba ni mkoa mzima,chukua hii Zitto anakubalika zaidi kitaifa zaidi ya kimkoa,na anakubalika kitaifa zaidi kwa watu ambao sio wanaCDM na wote wanaomkubali ukichunguza zaidi utagundua mawili either wanatoka CUF ama CCM.
Suala la idadi ya majimbo kuwa 8 na si 7 hiyo ni kweli na ni makosa ya kibinadamu na kiuandishi,asante kwa masahihisho,sijaelewa unaposema ameuletea mkoa wote wa kigoma nitakupinga,Nenda manyovu,Kibondo,kakonko na kasulu ukajiionee japo amefanikiwa kwa kiasi chake upande wa makao makuu ya mkoa,kuhusu ujenzi wa chama hakihesabu kuimalika kutokana na idadi ya mikutano bali majimbo waliyoshinda ama wanayoyatalajia kuyachukua na mikutano uisemayo aliifanya kutokana na vikao vya ndani kujadili uanzishwaji wa kanda,uchaguzi wa ndani na walivifanyia Kasulu na si ziala rasmi mkuu
 
makamanda wangu ntawatuma ucjali kamanda kunakwenda kuitawala nchi
 
Kimsingi sielewi tatizo ni nini ama Waha tumeikosea nini Tanzania na CHADEMA, wote tunatambua juhudi kubwa za wanakigoma katika kuyapokea mageuzi ya kisiasa hapa nchini kwani tangu vyama vingi vianzishwe mkoa wa Kigoma ulikuwa wa kwanza kutoa mbunge wa upinzani nchini,na kwa sasa mkoa mzima CCM wanamajimbo 3 kati ya majimbo 7 ya uchaguzi.

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba mkoa mzima hasa katika majimbo ya Muhambwe, Kakonko, Kasulu mjini na Kigoma mjini kote huko wananchi wanaipenda,kuikubali na kuiamini CHADEMA,na hata wabunge waliopo sasa Machali, Mkosamali, Mama Buyogela, Chiza na Serukamba walishinda either kwa kuiba kura (Chiza Kakonko na Serukamba Kigoma mjini )hawa waliiba kura na baadhi yao ninaushahidi wa kuaminika.

Kwa majimbo yaliyobaki NCCR MAGEUZI walishinda si kwa kuwa wanakubalika kama chama bali ni wananchi kukosa mgombe mbadala toka CHADEMA, Kwa mfano jimbo la Muhambwe na manyovu,japokuwa yapo madai ya watu wa CHADEMA kununuliwa na wale wa CCM,Majimbo yale yanayomilikiwa na vyama tofauti na CHADEMA wabunge wao wanakazi ya ziada kuweza kushinda isipokuwa kwa Kafulila tu ambaye nae kunatarifa zisizo Rasmi kutafta namna ya kurudi CHADEMA yeye na Nakaya na mpango huo unaratibiwa na mmoja wa viongozi wa CHADEMA.

Wakuu pamoja na hayo yote nasikitika kusema ni kama viongozi wa CDM kitaifa wametutelekeza wakazi wa Kigoma na mkoa kwa ujumla,naweza nikasema kwa uhakika makao makuu inahusika katika hili,kwani tangu uchaguzi mkuu wa 2010 hakuna kiongozi yoyote wa chama makao makuu aliewahi kufika hukokwa ajili ya kuimalisha chama yofauti na Zitto ambaye anaenda kama mbunge jimboni kwake

Kwa mfano watu wa huku wanampenda na kumkubali dk Slaa kuliko hata Zitto lakini hakuna harakati zozote za kuukomboa mkoa wa kigoma kutoka kwenye makucha ya CCM,viongozi wa makao wapo bize na kaskazini tu hasa Arusha inauma kwa kweli,tuseme sasa Arusha inatosha twende kigoma jamani,Viongozi wa sasa wa CDM waliopo Kigoma japokuwa wamekitoa mbali chama lakini kwa sasa wamechoka kifikra na kukata tamaa ni rahisi kununulika mfano katibu wa CDM mkoa na Mwenykiti wa CDM wilaya Kibondo mwalimu Ndidyicha huyu amebaki na kazi ya kujipendekeza kwa mkuu wa wilaya hiyo bwana Mwamoto wakati CDM wilaya nzima haina hata ofisi hai ya kupanga wala wanayoimiliki.

Zitto kabwe nae hana msaada wa kisiasa katika mkoa,kwani kwa jina lake na nguvu alizokuwa nazo kisiasa ilikuwa ni jambo la ajabu sana mkoa mzima akashinda yeye tu tena kwa mbinde na ni baada ya dk Slaa kurudi jimboni mwake kupiga kampeni upya,kama haitoshi mpaka sasa hajafanya hata ziara moja ya kuimalisha majimbo mkoani humo hii ni aibu kwani Charity begins@home,wito kwa mwenykiti wetu mbowe akumbuke jimbo la muhambwe la mkosamali alilipoteza baada ya Kumnyima fedha za kampeni dogo mkosamali wakati akijua wazi kuwa bado mwanafunzi wa SAUT ,dk Slaa nakuamini fanyia kazi hili
Mkosamali na Machali walihama CDM mapema tu kweda NCCR kumfuata kafulila ambaye ndiye walikuwa naye bega kwa bega toka mwanzo....
 
Mkosamali na Machali walihama CDM mapema tu kweda NCCR kumfuata kafulila ambaye ndiye walikuwa naye bega kwa bega toka mwanzo....

Mkuu Mpau kama ulikuwa hujui,chukua hii ,dogo Mkosamali alisafirisha hadi daresalama kwa gari ya Kafulila na kulipiwa kila kitu ili aende makao makuu kumwona mwenyekiti mbowe na amwulize jimbo la muhambwe limetengewa shilingi ngapi?hii inafuatia na ushawishi wa Zitto,Mma Buyogela a.k.a mama Balu na kafulila walikaa nae kwa zaidi ya masaa 3 katika Upendo Guest house kumshawishi huku Kafulila akimsisitizia Mkosamali kwamba makao makuu hawajalipa kupaumbele jimbo la Muhambwe na majimbo mengine mkoani humo iktajwa kuwa mwaka wa 2000 na 2005 CDM makao makuu walitoa fedha za kutosha bt zikaliwa na wajanja wachache na CDM ikapoteza jimbo,na kuonana na mwenyekiti Mbowe ilishindikana ndipo bwana Kafulila akamkutanisha na Johni Mnyika wakati huo akiwa ofisa habari wa chama makao mkuu na Mnyika akamwakikishia kwamba ni kweli kwa Jimbo la muhambwe chama hakijalipa kipaumbele jimbo hilo bt hawezi kukosa milioni 1 na nusu,huyohuyo Kafulila akampeleka dogo kwa mwenyekiti wa NCCR Mageuzi bwana Mbatia na mbatia akamwakikishia kumpatia milioni 5 kwa ajili ya kampeni kama atahamia NCCR ,na dogo Mkosamali akasaini deal na kuhamia huko yeye na mshauri wake mkuu ambaye kwa wakati huo alikuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya CDM kutokea mkoa wa Kigoma ndugu Balela na wakaenda redio Kwizela kutangaza kujitoa CDM na kuhamia NCCR,kumbukumbu zangu zinaniambia dogo alishiliki kwenye kampeni za marudio ya ubunge Busanda akitokea chuo cha SAUT,Tatzo kubwa la dogo Mkosamali ni njaa ya pesa na madarka bt bora alivyohama mapema coz alikuwa anatumiwa na Zitto na kwa sasa ni janga jimboni mwake hakubaliki tena na amebakia kugombana na mkuu wa wilaya hiyo na mwenyekiti aliefukuzwa huku akishinda kwa waganga Burundi,data ninazo

:angry:
 
Well said mkuu.....

Kigoma ni raslimali ya wanamageuzi isiyopewa attention stahiki

ZZK amepambana sana na ni mtu muhimu sana kwenye mageuzi TZ, ... ni vizuri kufahamu kuwa ni mtata at some point,
 
Mkuu oneblood,

Nasikia kwa mbali kidogo mataganzo ya mkutano wa CDM viwanja vya mikutano Kasulu Mjini, kesho saa 9. Make sure you are there pls
 
Mkuu oneblood,

Nasikia kwa mbali kidogo mataganzo ya mkutano wa CDM viwanja vya mikutano Kasulu Mjini, kesho saa 9. Make sure you are there pls
Point taken I will be there mkuu Muakyamirwa,M4C every where
 
Wewe unataka waje huko kufanya nini nawakati huko kunakirusi?
 
Mkuu oneblood,

Nasikia kwa mbali kidogo mataganzo ya mkutano wa CDM viwanja vya mikutano Kasulu Mjini, kesho saa 9. Make sure you are there pls

Hata mie nimesikia niko kasulu kikazi but kesho nageuza zangu Geita nikaungane na makamanda kwenye kampeni za udiwani kule kata ya Nyampulukano Sengerema
 
Wewe unataka waje huko kufanya nini nawakati huko kunakirusi?

Magamba mtateseka,mtahangaika na matapata maumivu ya kisaikolojia kama mwanamke aliyepitiliza miezi ya zaidi ya 4 ya kujifungua na wala hana uchungu wala dalili za kujifungua kwa kweli huwa inamuuma,CHADEMA forever

😛ray2:
 
Hakika wito huu wa mhimu. Fikeni pia kata ya Muhinda mkawatulize wale makamanda ambao bado wana hasira kali baada wa watu waliowaamini wawakilishe katika baraza la katiba wilaya kuenguliwa na diwani gamba,kilaza na mfisadi wa kata hiyo akishirikiana na wala rushwa wenyeviti katka kata hiyo iliyo katika wilaya mpya ya Buhigwe tarafa ya Manyovu.
 
Kwa asilimia kubwa naweza kukuamini mleta 'uzi' jinsi ulinyoweza kwa umakini kuileta na kuitetea hoja ya yako. Nadha HQ wakisikivu watalifanyia kazi hili
 
Back
Top Bottom