Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mara kimewasilisha ripoti maalum kwa Kanisa Katoliki, ikielezea matukio ya watu waliouawa au kupotea katika mkoa huo. Sambamba na hilo, chama hicho kimetumia nafasi hiyo kueleza msimamo wake wa No Reform No Election, ukimaanisha kwamba kitazuia uchaguzi wowote iwapo mabadiliko ya sheria na mfumo wa uchaguzi hayatatekelezwa.
Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Chacha Heche, amesema wamechukua hatua hiyo kwa sababu wamedanganywa mara nyingi kuhusu maridhiano ya kisiasa, huku wakihisi kuwa mfumo wa uchaguzi bado hauna usawa. Heche amewataka viongozi wa dini kuunga mkono juhudi za kupigania haki za wananchi, hususan katika kuimarisha demokrasia.
Diwani wa Kata ya Mbogi, Jimbo la Tarime Vijijini, Steven Nyahiri, ameainisha changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2024, akisema uchaguzi huo ulikumbwa na mapungufu makubwa. Ameeleza kuwa viongozi wa dini wana nafasi muhimu katika kupaza sauti na kusaidia kuleta mabadiliko ya kweli ya kisiasa na kijamii.
Kwa upande wake, Veronica Sando, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) Mkoa wa Mara, amesema kuwa licha ya mkoa huo kuwa na rasilimali nyingi kama mbuga za wanyama, badala ya kuwa baraka kwa wananchi, rasilimali hizo zimekuwa chanzo cha madhila, huku baadhi ya watu wakijeruhiwa au hata kuuawa.
Katibu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma, Cleophas Sabure, amethibitisha kupokea ripoti hiyo na kuahidi kuiwasilisha kwa Askofu wa Jimbo. Amesema baada ya Askofu kupitia ripoti hiyo, CHADEMA itaitwa kwa majadiliano zaidi ili kufanyia kazi malalamiko yao.
Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Chacha Heche, amesema wamechukua hatua hiyo kwa sababu wamedanganywa mara nyingi kuhusu maridhiano ya kisiasa, huku wakihisi kuwa mfumo wa uchaguzi bado hauna usawa. Heche amewataka viongozi wa dini kuunga mkono juhudi za kupigania haki za wananchi, hususan katika kuimarisha demokrasia.
Diwani wa Kata ya Mbogi, Jimbo la Tarime Vijijini, Steven Nyahiri, ameainisha changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2024, akisema uchaguzi huo ulikumbwa na mapungufu makubwa. Ameeleza kuwa viongozi wa dini wana nafasi muhimu katika kupaza sauti na kusaidia kuleta mabadiliko ya kweli ya kisiasa na kijamii.
Kwa upande wake, Veronica Sando, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) Mkoa wa Mara, amesema kuwa licha ya mkoa huo kuwa na rasilimali nyingi kama mbuga za wanyama, badala ya kuwa baraka kwa wananchi, rasilimali hizo zimekuwa chanzo cha madhila, huku baadhi ya watu wakijeruhiwa au hata kuuawa.
Katibu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma, Cleophas Sabure, amethibitisha kupokea ripoti hiyo na kuahidi kuiwasilisha kwa Askofu wa Jimbo. Amesema baada ya Askofu kupitia ripoti hiyo, CHADEMA itaitwa kwa majadiliano zaidi ili kufanyia kazi malalamiko yao.
