WanaJF!
Dhana hii ya kuwajibika na kuwajibishwa imekuwa ikielekezwa upande mmoja tu, nako ni CCM na serikali yake. Tena mara kwa mara mashinikizo yamekuwa yakitokea CHADEMA, kuwa serikali iwawajibishe viongozi wenye kasoro.
Lakini kama ilivyo ada, CHADEMA imesahau kwa makusudi kabisa katika kuwawajibisha viongozi wake hasa wale wenye muelekeo wa kukichafua chama.
Kwa mfululizo wa matukio haya yaliyo muandama Dr Slaa, kama CHADEMA kingekuwa chama makini basi kingemchukulia hatua Dr Slaa za kinidhamu kwa lengo la kulinda hadhi ya chama.
Mfululizo wa matukio yenyewe ni kama ifuatavyo;
1. TUHUMA YA KUKWAPUA MKE WA MTU. Hii tuhuma sio tu kwamba imemchafua Dr Slaa na Josephine, bali imechafua CHADEMA kwa kiasi kikubwa sana mbele ya jamii ya watu wenye heshima na wastaarabu.
2. TUHUMA YA KUMPA JOSEPHINE MAMLAKA NDANI YA CHADEMA. Hii pia imeshusha heshima ya CHADEMA kwani watanzania kwa sasa wanaona CHADEMA ni kama chama cha familia.
Haiwezekani mchumba wa katibu mkuu kupewa fedha za chama kwa ajili ya ziara za mikoani. Josephine ni nani mpaka akakague uhai wa chama mikoani?
3. TUHUMA YA KUJIKOPESHA FEDHA YA CHAMA. Hii tuhuma tangu imetolewa haijawahi kupatiwa maelezo, zaidi ya kupiga piga chenga. Hali iliyo pelekea CHADEMA kuonekana kama sio chama cha siasa bali ni 'saccoss' ya watu wachache.
Kwa tuhuma hizo na nyingine nyingi dhidi ya Dr Slaa kama katibu mkuu wa CHADEMA, ingekuwa ni vyema kama chama kingechukua hatua za kinidhamu dhidi yake, hata kwa kumuondoa kwenye nafasi hiyo ili chama kiweze kurejesha hadhi yake kwenye jamii, ambayo kimsingi kwa sasa hadhi ya CHADEMA imeshuka sana kutokana na matukio haya ya aibu.
Dhana hii ya kuwajibika na kuwajibishwa imekuwa ikielekezwa upande mmoja tu, nako ni CCM na serikali yake. Tena mara kwa mara mashinikizo yamekuwa yakitokea CHADEMA, kuwa serikali iwawajibishe viongozi wenye kasoro.
Lakini kama ilivyo ada, CHADEMA imesahau kwa makusudi kabisa katika kuwawajibisha viongozi wake hasa wale wenye muelekeo wa kukichafua chama.
Kwa mfululizo wa matukio haya yaliyo muandama Dr Slaa, kama CHADEMA kingekuwa chama makini basi kingemchukulia hatua Dr Slaa za kinidhamu kwa lengo la kulinda hadhi ya chama.
Mfululizo wa matukio yenyewe ni kama ifuatavyo;
1. TUHUMA YA KUKWAPUA MKE WA MTU. Hii tuhuma sio tu kwamba imemchafua Dr Slaa na Josephine, bali imechafua CHADEMA kwa kiasi kikubwa sana mbele ya jamii ya watu wenye heshima na wastaarabu.
2. TUHUMA YA KUMPA JOSEPHINE MAMLAKA NDANI YA CHADEMA. Hii pia imeshusha heshima ya CHADEMA kwani watanzania kwa sasa wanaona CHADEMA ni kama chama cha familia.
Haiwezekani mchumba wa katibu mkuu kupewa fedha za chama kwa ajili ya ziara za mikoani. Josephine ni nani mpaka akakague uhai wa chama mikoani?
3. TUHUMA YA KUJIKOPESHA FEDHA YA CHAMA. Hii tuhuma tangu imetolewa haijawahi kupatiwa maelezo, zaidi ya kupiga piga chenga. Hali iliyo pelekea CHADEMA kuonekana kama sio chama cha siasa bali ni 'saccoss' ya watu wachache.
Kwa tuhuma hizo na nyingine nyingi dhidi ya Dr Slaa kama katibu mkuu wa CHADEMA, ingekuwa ni vyema kama chama kingechukua hatua za kinidhamu dhidi yake, hata kwa kumuondoa kwenye nafasi hiyo ili chama kiweze kurejesha hadhi yake kwenye jamii, ambayo kimsingi kwa sasa hadhi ya CHADEMA imeshuka sana kutokana na matukio haya ya aibu.