Hebu niambieni tofauti ya chadema na ccm kwa sasa ni nini?
Tunataka kitu brand new! Hivi kutoafauti gani ya uwepo wa Chenge ccm na uwepo Nyalandu chadema?
Hivi unawezaje kusema tuwakatae watu waliotufikisha hapa huku umemkumbatia Sumaye, Lowasa na Nyalandu?
Utasikia wana chadema wakisema eti hoo mbona hamuwashiki kuwapeleka mahakamani, serious? Kwahiyo kwavile mwenzio anakojoa ndani na wewe unakojoa ndani?
Ndio maana watu kama kina Kafulila wakiamua kujiondoa wanaonekana wanatafuta vyeo! Hivi Kafulila si alikuwa anajua kwamba chadema hakuna vyeo au?
Siyo kwamba watu hajaichoka ccm, ila wanajiuliza mbadala wa ccm ni nani? Hakuna!