4 7mbatizaji
JF-Expert Member
- Dec 8, 2019
- 5,979
- 6,782
Sina
Kwa tathmini ya harakaharaka inaonesha uchaguzi mwaka huu ni mgumu sana kwa CCM. Siyo kwasababu CCM haijafanya kitu , la , ila ni kwasababu raia wa nchi hii wameichoka kabisa. Ndiyo maana wamejaribu kuonesha na kutangaza miradi mingi iliyofanywa na Serikali yao lakini raia hawaelewi.
Kwa sababu hiyo CCM wanajaribu kutumia njia zingine ili wapate ushindi. Ndiyo maana nawatahadharisha chadema waangalie mambo yafuatayo ambayo nimeyashuhudia mimi mwenyewe hapa mwanza jimbo la nyamagana.
1. CCM wanazunguka shule za sekondari za boarding na kuwashawishi wanafunzi kuwapigia kura lakini pia kuwatumia kuingiza kura hewa.
2. Wasimamizi wa uchaguzi na makarani waongozaji kwenye vituo vyote vya kupigia kura ni makada wa CCM. Safari hii hata walimu wamepigwa chini wakisema kuwa hawajapewa stahiki zao kwahiyo wanahofu wataangusha.
Wote walioomba hiyo kazi walikuwa wanaulizwa maswali yafuatayo:
-Kama ni mwanachama wa CCM
- Kama yuko tayari kupokea maelekezo tofauti na kanuni za uchaguzi Kama kuingiza majina hewa au kuhakikisha mgombea wa CCM anashinda. Ukikataa utaambiwa asante kwa kushiriki.
Kwahiyo wanafunzi ndiyo wanaandaliwa kupelekwa kwenye vituo na kuingiza kura ambazo tayari zimeshapigwa.
Mbali na wanafunzi wafungwa na vyombo vya usalama wanaweza kutumika pia.
CHADEMA fuatilieni hayo na muwe na msimamo thabiti.
Sina Shaka na uchaguzi huu pamoja na yote hayo mungu wangu kaisha nitoa hofu ,kwa kweli sikufunga siku kumi nne bure ,Asante Sana jf mungu awabariki jukwaa murua Sana, mnanifanya kuwa na raha mda woteKwa tathmini ya harakaharaka inaonesha uchaguzi mwaka huu ni mgumu sana kwa CCM. Siyo kwasababu CCM haijafanya kitu , la , ila ni kwasababu raia wa nchi hii wameichoka kabisa. Ndiyo maana wamejaribu kuonesha na kutangaza miradi mingi iliyofanywa na Serikali yao lakini raia hawaelewi.
Kwa sababu hiyo CCM wanajaribu kutumia njia zingine ili wapate ushindi. Ndiyo maana nawatahadharisha chadema waangalie mambo yafuatayo ambayo nimeyashuhudia mimi mwenyewe hapa mwanza jimbo la nyamagana.
1. CCM wanazunguka shule za sekondari za boarding na kuwashawishi wanafunzi kuwapigia kura lakini pia kuwatumia kuingiza kura hewa.
2. Wasimamizi wa uchaguzi na makarani waongozaji kwenye vituo vyote vya kupigia kura ni makada wa CCM. Safari hii hata walimu wamepigwa chini wakisema kuwa hawajapewa stahiki zao kwahiyo wanahofu wataangusha.
Wote walioomba hiyo kazi walikuwa wanaulizwa maswali yafuatayo:
-Kama ni mwanachama wa CCM
- Kama yuko tayari kupokea maelekezo tofauti na kanuni za uchaguzi Kama kuingiza majina hewa au kuhakikisha mgombea wa CCM anashinda. Ukikataa utaambiwa asante kwa kushiriki.
Kwahiyo wanafunzi ndiyo wanaandaliwa kupelekwa kwenye vituo na kuingiza kura ambazo tayari zimeshapigwa.
Mbali na wanafunzi wafungwa na vyombo vya usalama wanaweza kutumika pia.
CHADEMA fuatilieni hayo na muwe na msimamo thabiti.