Kuhusu bajeti ya uchanguzi mdogo wa ubunge jimbo la Arumeru Mashariki, Mnyika alisema chama kimeamua kuwa kampeni za uchaguzi huo ziendeshwe kwa nguvu ya umma bila kutegemea ruzuku za chama.
Alisema chama kimejipanga kupata misaada kutoka kwa wananchi wa Arumeru na wananchi wengine nchini katika kuhakikisha hakitumii ruzuku ya chama kwenye uchaguzi huo.
"Kampeni za Arumeru zitaendeshwa kwa nguvu ya umma ikiwa ni pamoja na kupata fedha za wananchi kote nchini na si kutegemea ruzuku za chama bali za wananchi kwa ujumla na hasa Arumeru,"alisema Mnyika.
Alisema chama kimeteua watu kadhaa wa kuangalia jinsi gani ya kupata fedha hizo za nguvu ya umma na kile kiasi ambacho kitahitajika kuongezeka chama kitatangaza kiasi gani kitatumika.
SOURCE:MWANANCHI.
Alisema chama kimejipanga kupata misaada kutoka kwa wananchi wa Arumeru na wananchi wengine nchini katika kuhakikisha hakitumii ruzuku ya chama kwenye uchaguzi huo.
"Kampeni za Arumeru zitaendeshwa kwa nguvu ya umma ikiwa ni pamoja na kupata fedha za wananchi kote nchini na si kutegemea ruzuku za chama bali za wananchi kwa ujumla na hasa Arumeru,"alisema Mnyika.
Alisema chama kimeteua watu kadhaa wa kuangalia jinsi gani ya kupata fedha hizo za nguvu ya umma na kile kiasi ambacho kitahitajika kuongezeka chama kitatangaza kiasi gani kitatumika.
SOURCE:MWANANCHI.