EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Kwenye uchaguzi huu Chadema kimeamua kuhakiki wapigakura wake katika vijiji vyote vya Jimbo la Arumeru Mashariki mbinu ambayo ilitumiwa na CCM kwenye uchaguzi uliopita wa Igunga. Jimbo hilo lina kata 17 na vijiji 86. Akizungumzia mkakati wa ushindi wa chama hicho, Katibu Mkuu Dr. W. Slaa amesema viongozi 10 wa Chadema katika kila kijiji watapewa fomu za kuwajua wapiga kura na kuhakikisha kuwa wanakipigia kura chama hicho.
"Mtapewa fomu leo na kila kiongozi ataorodhesha watu wake tayari kwa mkakati wa kampeni na hili sio kosa kwani tunataka kuhakikisha kuwa tunajua mapema kuwa ushindi wetu ni wa kura ngapi,"alisema Dk Slaa.
Alisema utaratibu huo pia utawezesha kuanza kwa kampeni za nyumba kwa nyumba kwa kila kiongozi na kwamba katika eneo ambalo kura zitakuwa chache kiongozi anayehusika atatoa maelezo.
Katika hatua nyingine Katibu Mkuu huyo ameagiza kukamata magari ya viongozi wa CCM watakaopita katika maeneo yao, kwa lengo la kununua shahada za kupigia kura na kutoa rushwa.
"Kukamata wahalifu si kazi ya polisi pekee yao, nawaagiza kuwa kuanzia sasa muwe makini na CCM maana tayari magari yao yameanza kuonekana vijijini wakiwarubuni wananchi, mkiwaona wakamateni,"alisema Dk Slaa.
Katibu huyo, alisema baada ya kukamata magari na wanachama wa CCM watakaotoa rushwa, hatua zichukuliwe kuwafikisha katika vituo vya polisi na kama wakisumbua wawasiliane na viongozi wa kitaifa wa Chadema waliopiga kambi katika jimbo hilo.
"Kamateni hao wanaokiuka sheria msidanganyike kuwa kazi hiyo ni ya polisi, wakiwasumbua tupigieni simu na hili msiwe na hofu yoyote makamanda wangu," alisema Dk Slaa.
Mwananchi.
"Mtapewa fomu leo na kila kiongozi ataorodhesha watu wake tayari kwa mkakati wa kampeni na hili sio kosa kwani tunataka kuhakikisha kuwa tunajua mapema kuwa ushindi wetu ni wa kura ngapi,"alisema Dk Slaa.
Alisema utaratibu huo pia utawezesha kuanza kwa kampeni za nyumba kwa nyumba kwa kila kiongozi na kwamba katika eneo ambalo kura zitakuwa chache kiongozi anayehusika atatoa maelezo.
Katika hatua nyingine Katibu Mkuu huyo ameagiza kukamata magari ya viongozi wa CCM watakaopita katika maeneo yao, kwa lengo la kununua shahada za kupigia kura na kutoa rushwa.
"Kukamata wahalifu si kazi ya polisi pekee yao, nawaagiza kuwa kuanzia sasa muwe makini na CCM maana tayari magari yao yameanza kuonekana vijijini wakiwarubuni wananchi, mkiwaona wakamateni,"alisema Dk Slaa.
Katibu huyo, alisema baada ya kukamata magari na wanachama wa CCM watakaotoa rushwa, hatua zichukuliwe kuwafikisha katika vituo vya polisi na kama wakisumbua wawasiliane na viongozi wa kitaifa wa Chadema waliopiga kambi katika jimbo hilo.
"Kamateni hao wanaokiuka sheria msidanganyike kuwa kazi hiyo ni ya polisi, wakiwasumbua tupigieni simu na hili msiwe na hofu yoyote makamanda wangu," alisema Dk Slaa.
Mwananchi.