CHADEMA kuondokewa na mgombea urais Lowassa na mgombea mwenza wake Juma Duni Haji kunaashiria nini?

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,907
Wakuu chadema Mgombea uraisi na mgombea mwenza wao 2015 wote wameondoka chadema. Alianza Juma Duni Haji mgombea Mwenza sasa mgombea uraisi kamalizia. Wataalamu wa political science mtusaidie hili ni nini? wenyewe chadema wanasema hakuna kitu kuondoka kwao si kitu
 
Hawajawahi kujipanga kugombea Urais ndio maana waliwatafuta Mamuluki/wapiganaji wa kuazima ili kuwasaidia, mamuluki wamerudi kwao.
 
Yehodaya. Pamoja na kuifanyia Cdm umafia wa kutumia rasilimali za serikali.
Na vyombo vya Dola na vya maamuzi bado hamridhiki ?!

Lowassa kapata mwaliko, na kafanya ziara Ikulu mwenyewe , bila kushirikisha chama na wananchi walioumizwa kwa ajili yake. Kosa la Cdm ni nini hapo ?!.
Vyama hivi visivyo na dola huwezi kumshurutisha mtu kubaki.

Na hata huko CCM hajaenda kwa utashi wake. Bali kuna mengi yamepita chini ya Capet ili kudhoofisha upinzani na kulinda maslahi yake. Kama ulimsikia bosi aliuliza "kwanini umeteseka huko muda wote huo ?!"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona hivyo ujue wamechoka kuokoteza makapi kutoka mtaa wa Lumumba. Uchaguzi wa mwakani mkae mkao wa kula maana yule mnadhimu wao kama kweli atagombea, huenda akawavuruga sana.

Nimeona tu mlivyochanganyikiwa siku chache zilizopita baada ya yeye tu kufanya mikutano michache na mahojiano na vyombo vya habari vya kimataifa. Mlipoteana hadi mlikua mnatia huruma. Mlijitahidi kujibizana nae lakini kiukweli mlishindwa.
 
Hayo mengi hebu taja japo matatu aliyofanyiwa hadi kaamua kurudi CCM?

Je ninyi hamjiangalii mmemkosea nini hadi kaamua kuondoka? Acheni ujinga tamaa ya madaraka na ufisadi wa ruzuku, na upendeleo itawamaliza.

Angalia viti maalimu wengi wenu wachaga na ndugu za viongozi wa chadema. Si ni ulofa huu. Hata mke wa Lowassa mlimteua viti maalum japo alikataa
 

Wamemaliza Kazi waliyotumwa,unadhani angesimama Dr slaa 2015 Leo ungepata hata hio buku saba,
 
Ushajiuliza itakuwaje endapo upinzani halisi ukiacha kusimamisha mgombea?
Je kama wakimkaribisha Mh. Zitto Kabwe agombee akisindikizana na Sumaye?
Hizi siasa bwana..watakaa wajipange sis tunasubiria Sera..alafu kupiga kura
 
Kwanza kabisa cha kufahamu ni kuwa ule ulikuwa ni mkakati wa ukawa wa kupambana na CCM, ENL hajawahi kuwa mpinzani na Duni hajawahi kuwa Chadema. Kuondoka kwa ENL kunaipa Chadema na upinzani fursa ya kujipanga vema zaidi. Zinagtia: 1 Yohana 2:19.
 
Mahaba huficha madhaifu,, hili ni jambo la msingi sana ambalo Ukawa wanatakiw wajiulize lakini hawatofanya hivyo... na utatukanwa sana kuleta huu uzi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tundu Lissu TOSHA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…