Chadema kuelekea 2015

Nimewahi kusema huko nyuma kwamba watanzania wanakila kitu isipokuwa Viongozi.

Nakubaliana na wewe kwa hoja ya pili kwamba kuna madhira yanatusibu kwa vile tu viongozi wanapenda kufikiri kwa niaba yetu badala ya kutushirikisha. Yapo matatizo ktk jamii tunamoishi yanahitaji ushirikishwaji wa watu tu. Kwa mfano:
- Usafi wa mtaa
- kuziba/kufukia mazalia ya mbu
- ukarabati mdogo wa barabara za mtaa (za vumbi)
- Usafi kwenye maeneo ya wazi ili watoto wacheze mahali safi n.k

Tunahitaji kusikilizwa na kutoa maoni juu ya maendeleo yetu wenyewe.
Kama CDM watafanya hivi, ntakuwa wa kwanza kuomba kadi ya uanachama na itakuwa mara yangu ya kwanza kuwa mwanachama wa chama cha siasa.

hivi haswa ndio vitu vya msingi vya kuanzia itasaidia sana kuwaweka viongozi wetu sawa, na kujua majukumu yao kwa jamii maana wanachokifanya sas hivi hakieleweki kabisaaaaaaaaa(e.g unakuta mwenyekiti wa kitongoji hajui hata taka za home kwake zinatupwa wapi anachojua ni kudai posho za vikao)
 
Naunga mkono hoja.

Kila mwanachadema ahakikishe ana kadi ya uanachama na pia awe mjumbe katika shina na tawi katika eneo analoishi na kuhudhuria vikao vya chama bila kukosa.
Mimi binafsi jumamosi 29/01/2011 nitahudhuri kikao chama cha kata katika jimbo la Temeke-DSM. Ajenda kuu ya mkutano ni kufungua matawi mengi ya wakereketwa wa CDM.

Wakubalance, CDM sio chama cha wachaga kama ambavyo wewe unaeneza. Tunajua unalipwa fedha nyingi na sisiemu kwa kazi hiyo. Napenda kukujulisha kuwa umechelewa sana kwani asilimia kubwa ya watanzania wa sasa wanafahamu kwamba CDM ndio chama makini chenye watu makini na sera za ukweli. Ndani ya sisiemu watu makini ni wawili tu mzee 6 na mwakimango waliobaki wote ni vilaza including you!
 
Yafanyieni kazi hayo maono, yataboresha maisha ya watz. Hakuna taifa duniani limewahi kuwa na maendeleo kwa kupiga porojo labda la misukule. Hivyo tunahitaji kuchapa kazi kama tutaishi milele, tukifanya hivyo na kudhibiti wabaka uchumi (mafisadi) lazima ndege yetu ipae. Taifa likikosa viongozi wenye maono limepotea kabisa, tuombe Mungu tusifike huko.
 
Back
Top Bottom