CHADEMA: Kabla ya Mwaka 2015 Rais Kikwete anasafiri sana, baada ya mwaka 2015 kwanini Rais Magufuli hasafiri nje ya nchi?

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

Kipindi cha utawala wa Rais Kikwete,CADEMA walisema yafuatayo kuhusu ziara za nje ya nchi; Safari za Rais zimeifilisi nchi. Rais anaenda nchi za nje kutalii, Rais anapaswa kubaki nchini ashughulikie kero za wananchi badala ya kusafiri, Ziara za Rais Kikwete ni za kuombaomba hazina mkakati wowote nk.

Katika kipindi hiki cha utawala wa Rais Magufuli vinywa vya CHADEMA vinanena haya: Rais Magufuli ni mshamba hataki kujichanganya na Marais wenzie. Rais Magufuli asafiri nje ya nchi majukumu ya ndani awaachie wasaidizi wake. Kutosafiri nje ya nchi kunaikosesha nchi misaada. Rais Magufuli aende nje kujifunza kutoka mataifa mengine nk.

Kabla ya kuhitimisha niwakumbushe kuwa pamoja na Kenyatta kwenda China kwa mbwembwe lakini hao China wamemnyima mkopo ujenzi wa reli.

Kuna mengi mnaweza kuongezea kwenye hoja hii nawatakia siku njema.
 
Kuna mbwekaji moja juzi alikuwa analalamika Kwanini Magufuli hajaenda Urus!

Huyo Huyo jana kaanza kulalamika mkutano wa Urus unafaida gani kwa Africa?

Unaweza kuona jinsi gani hawawatu wasivyo kua na haya wala heshima
 
Ndugu zangu,

Kipindi cha utawala wa Rais Kikwete,CADEMA walisema yafuatayo kuhusu ziara za nje ya nchi; Safari za Rais zimeifilisi nchi. Rais anaenda nchi za nje kutalii, Rais anapaswa kubaki nchini ashughulikie kero za wananchi badala ya kusafiri, Ziara za Rais Kikwete ni za kuombaomba hazina mkakati wowote nk.

Katika kipindi hiki cha utawala wa Rais Magufuli vinywa vya CHADEMA vinanena haya: Rais Magufuli ni mshamba hataki kujichanganya na Marais wenzie. Rais Magufuli asafiri nje ya nchi majukumu ya ndani awaachie wasaidizi wake. Kutosafiri nje ya nchi kunaikosesha nchi misaada. Rais Magufuli aende nje kujifunza kutoka mataifa mengine nk.

Kabla ya kuhitimisha niwakumbushe kuwa pamoja na Kenyatta kwenda China kwa mbwembwe lakini hao China wamemnyima mkopo ujenzi wa reli.

Kuna mengi mnaweza kuongezea kwenye hoja hii nawatakia siku njema.
Wapuuzi hao.
Rais kikwete ni DHAIFU, NI LEGELEGE. Tunataka rais imara, rais mkali. Kaja rais imara na mkali, ooooh...rais huyu ni dikteta.
 
Kama Engineer wa Chama kwenye uropokaji enzi za Kikwete ni huyu huyu (Mbowe)wa awamu hii ya Magufuli unategemea vipi chama kiwe na sera mpya za kupambana na huu utawala
Tatzo kubwa kwa hawa Chadema ni wao kujiona wapo very UNIQUE lakini ukiwafatilia wao na matendo yao ndio balaa kabsa Mikakati ya Mauaji wapo,Wizi wapo,Kusaliti wa Nchi yetu wapo
 
Kuna mbwekaji moja juzi alikuwa analalamika Kwanini Magufuli hajaenda Urus!

Huyo Huyo jana kaanza kulalamika mkutano wa Urus unafaida gani kwa Africa?

Unaweza kuona jinsi gani hawawatu wasivyo kua na haya wala heshima

Kwa niaba ya muanzisha mada na ww mpotoshaji mwenzake, malalamiko ilikuwa kusafiri sana hadi safari zisizo na tija na sio kusafiri, hapa zingatia neno kusafiri sana. Magufuli hasafiri kabisa, hapa zingatia kusafiri sana mbadala wake sio kutokusafiri kabisa. Hivi mtu akiambiwa amezaa watoto wengi sana, jibu ni mdogo wake kutokupata mtoto kabisa?
 
Wakati wa Kikwete walisema Serikali haina ubavu wa kumkamata Seth na Ruge, baada ya kuingia JPM imekuwa sasa Mzee Ruge na umri wake wa zaid ya miaka 70 anaonewa

Acha upotoshaji, watu walisema Seth na Ruge wakamatwe pamoja na kundi lote aliloshirikiana nalo huko serikalini. Kinyume na hapo ni uonevu kama uonevu mwingine. Kinacholalamikiwa hapa ni double standard katika zoezi hilo. Kama unadhani mtaleta huu Utetezi dhaifu na mtarajie kutoboa mtapata tabu sana.
 
Ndugu zangu,

Kipindi cha utawala wa Rais Kikwete,CADEMA walisema yafuatayo kuhusu ziara za nje ya nchi; Safari za Rais zimeifilisi nchi. Rais anaenda nchi za nje kutalii, Rais anapaswa kubaki nchini ashughulikie kero za wananchi badala ya kusafiri, Ziara za Rais Kikwete ni za kuombaomba hazina mkakati wowote nk.

Katika kipindi hiki cha utawala wa Rais Magufuli vinywa vya CHADEMA vinanena haya: Rais Magufuli ni mshamba hataki kujichanganya na Marais wenzie. Rais Magufuli asafiri nje ya nchi majukumu ya ndani awaachie wasaidizi wake. Kutosafiri nje ya nchi kunaikosesha nchi misaada. Rais Magufuli aende nje kujifunza kutoka mataifa mengine nk.

Kabla ya kuhitimisha niwakumbushe kuwa pamoja na Kenyatta kwenda China kwa mbwembwe lakini hao China wamemnyima mkopo ujenzi wa reli.

Kuna mengi mnaweza kuongezea kwenye hoja hii nawatakia siku njema.
Too much of everything is harmful, ukila chakula kingi ni shida usipo Kula kabisa nayo ni shida,ila kwa mwanaccm kuelewa jambo hili dogo ni ngumu mno
 
Wapuuzi hao.
Rais kikwete ni DHAIFU, NI LEGELEGE. Tunataka rais imara, rais mkali. Kaja rais imara na mkali, ooooh...rais huyu ni dikteta.

Mjinga hutumia nguvu kuzifanya hoja zake zionekane bora. Kikwete alikuwa dhaifu maana hakuchukua hatua stahiki kwa wenye makosa kwa mujibu wa sheria ndio tukataka rais mkali. Rais huyu sio mkali bali ana jazba, tenganisha ukali na jazba. Wangalau mfano wa ukali ni wa Nyerere. Huyu ni dictator maana kajigeuza yeye ndio sheria, ndio mifumo ndio kila kitu. Kwa maneno marahisi Magufuli ni rais mwenye mtindo tofauti na JK, lakini sio aina ya rais tuliyemtaka.
 
Ndugu zangu,

Kipindi cha utawala wa Rais Kikwete,CADEMA walisema yafuatayo kuhusu ziara za nje ya nchi; Safari za Rais zimeifilisi nchi. Rais anaenda nchi za nje kutalii, Rais anapaswa kubaki nchini ashughulikie kero za wananchi badala ya kusafiri, Ziara za Rais Kikwete ni za kuombaomba hazina mkakati wowote nk.

Katika kipindi hiki cha utawala wa Rais Magufuli vinywa vya CHADEMA vinanena haya: Rais Magufuli ni mshamba hataki kujichanganya na Marais wenzie. Rais Magufuli asafiri nje ya nchi majukumu ya ndani awaachie wasaidizi wake. Kutosafiri nje ya nchi kunaikosesha nchi misaada. Rais Magufuli aende nje kujifunza kutoka mataifa mengine nk.

Kabla ya kuhitimisha niwakumbushe kuwa pamoja na Kenyatta kwenda China kwa mbwembwe lakini hao China wamemnyima mkopo ujenzi wa reli.

Kuna mengi mnaweza kuongezea kwenye hoja hii nawatakia siku njema.
Huujui msemo usemao VIRTUE STANDS IN THE MIDDLE?? Too high or too low both are harmful. They should strike the balance!!
 
Mjinga hutumia nguvu kuzifanya hoja zake zionekane bora. Kikwete alikuwa dhaifu maana hakuchukua hatua stahiki kwa wenye makosa kwa mijini wa sheria ndio tukataka rais mkali. Rais huyu sio mkali bali ana jazba, tenganisha ukali na jazba. Wangalau mfano wa ukali ni wa Nyerere. Huyu ni dictator maana kajigeuza yeye ndio sheria, ndio mifumo ndio kila kitu. Kwa maneno marahisi Magufuli ni rais mwenye mtindo tofauti na JK, lakini sio aina ya rais tuliyemtaka.
Ndio chaguo letu pendwa WATANZANIA WENGI. subirini 2035 mnaweza chagua mumtakaye, tatizo mko wachache.
 
Kuna mbwekaji moja juzi alikuwa analalamika Kwanini Magufuli hajaenda Urus!

Huyo Huyo jana kaanza kulalamika mkutano wa Urus unafaida gani kwa Africa?

Unaweza kuona jinsi gani hawawatu wasivyo kua na haya wala heshima
Wasivyo kuwa na haya wala heshima kama bwana yule anayetukana watu hadharani utadhani kawa kibaka.
 
Ndugu zangu,

Kipindi cha utawala wa Rais Kikwete,CADEMA walisema yafuatayo kuhusu ziara za nje ya nchi; Safari za Rais zimeifilisi nchi. Rais anaenda nchi za nje kutalii, Rais anapaswa kubaki nchini ashughulikie kero za wananchi badala ya kusafiri, Ziara za Rais Kikwete ni za kuombaomba hazina mkakati wowote nk.

Katika kipindi hiki cha utawala wa Rais Magufuli vinywa vya CHADEMA vinanena haya: Rais Magufuli ni mshamba hataki kujichanganya na Marais wenzie. Rais Magufuli asafiri nje ya nchi majukumu ya ndani awaachie wasaidizi wake. Kutosafiri nje ya nchi kunaikosesha nchi misaada. Rais Magufuli aende nje kujifunza kutoka mataifa mengine nk.

Kabla ya kuhitimisha niwakumbushe kuwa pamoja na Kenyatta kwenda China kwa mbwembwe lakini hao China wamemnyima mkopo ujenzi wa reli.

Kuna mengi mnaweza kuongezea kwenye hoja hii nawatakia siku njema.
Inawezekana rais mmoja akawa anasafiri sana, mwingine akawa hasafiri kabisa, na inavyotakiwa ni rais anayesafiri kwa kiasi.
 
Ndio chaguo letu pendwa WATANZANIA WENGI. subirini 2035 mnaweza chagua mumtakaye, tatizo mko wachache.

Ukweli hauendani na usemacho. Juzi wakati wa kuandikisha wapiga kura SM ilikuwa ni kipimo halisi, usemacho kinakataana na ukweli. Hivi tunavyozungumza boss wa Twaweza kuporwa passport, kwa kuweka ukweli wa kukubalika kwa mungu wa Tanzania.
 
Wakati wa Kikwete walisema Serikali haina ubavu wa kumkamata Seth na Ruge, baada ya kuingia JPM imekuwa sasa Mzee Ruge na umri wake wa zaid ya miaka 70 anaonewa

..wakati wa JK mlisema Babu Seya na Papii ni walawiti watoto wanastahili adhabu kali.

..Jpm alipowafungulia mkashangilia mkidai ana mamlaka ya kusamehe yeyote. Na mkashangilia zaidi walipoalikwa Ikulu.

..wakati huohuo mnadai mnapiga ushoga, lakini mnashangilia shoga anayeharibu watoto wa shule kurudishwa mtaani.
 
Nakumbuka wakati wa JK kulikuwa na kelele kwamba hatuna ndege hata moja hadi tunazidiwa na vinchi kama Rwanda!

Tukaambiwa enzi za Nyerere ATC ilikuwa na ndege sijui ngapi tena Boeing na blah blah kibao!

Tukaambiwa ilani yao imeweka wazi kufufua shirika la ndege!

Awamu hii ikaanza na "bomba Dear",wakazikashifu kwamba heri kupanda Superfeo au Saratoga hivyo vipangaboi siyo ndege,seat kama school bus!!

Mara tulipoambiwa zinakuja Dreamliner wimbo ukabadilika ikawa zitakuwa "Terrible teen" mara " zitamsaidiaje bibi yangu kule kijijini?"

Sasa hivi tunaambiwa siyo kipaumbele kwa sababu hakuna Kijiji chochote kwenye ziara za viongozi waliwahi kuambiwa kero yao ni ndege!

Kwani serikali ipo kwa ajili ya kutatua kero za wanavijiji tu?

Ni wanavijiji wa wapi waliwahi kusema kero yao katiba mpya au idadi ya serikali za muungano au tume ya uchaguzi?

Ilani yenu ilitaka kufufua shirika la ndege gani ambazo ni kero kwa wanakijiji? Kware au bata mzinga?


Njia rahisi ya ku-deal na wapumbavu design hii ni kuwa-ignore!

Magu akitoka mtakuja tena kujibaraguza humu kwamba alikuwa the best tatizo ni MFUMO.
 
Back
Top Bottom