CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu


Mkuu nashukuru sana kwa kunitendea haki. Ukijaribu kuangalia michango yangu kwa cdm haina shaka kwamba naikubali cdm na pia naitaka mema cdm kama chama. Hata msimamo wangu kuhusu Lowassa uko wazi na wala sikuyumba mpaka majuzi anaondoka cdm.

Tuje kwenye hili la Mbowe, ukweli ni kuwa Mbowe ni jabali hasa na mhimili halisi wa cdm, lakini hili suala la kwamba sio muda muafaka Mbowe kuachia madaraka silipendi sana kwani hata wakati wa JK ilisemwa hivyo hivyo. Wasiwasi wangu Mbowe anaweza kuendelea kuwa mwenyekiti kwa sababu hizi hizi za kwamba muda sio sahihi. Hivi ni kweli ndani ya cdm taasisi ni Mbowe tu ndio jasiri na wengine wote ni wadhaifu? Angalia post yangu namba 31 hasa post paragraph ya pili utapata ni kipi nasimamia.

Huenda Mbowe anaweza akachaguliwa tena na wanachama hilo sina shida nalo kwani ndio demokrasia, lakini wangalau akijadiliwa kutapatikana mabadiliko ya dhati. Kwa mfano huyo katibu mkuu kuna haja ya kuendelea kuwa na mtu wa hivyo wakati huu? Huoni kama tungekuwa na katibu mkuu imara Mbowe naye angezidi kuwa imara. Tuje kwenye mfano halisi mfano masahibu yaliyompata Lisu yangempata Mbowe na hata kufa Cdm ndio ingekufa? Tujue cdm ndio maisha yetu na ndio silaha yetu, iwapo leo tutashindwa hata kuhoji nafasi ya mwenyekiti wetu tutapata wapi nguvu ya kuhoji nguvu ya rais? Nashukuru sana Kalamu1 umejitosa kwenye hili, tusione aibu kuhoji uwajibikaji wa yoyote.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
 
Kama kumbukumbu yangu hainiangushi, nakuomba urejee wakati ule wa kampeni iliyokuwa inapangwa ya "UKUTA." Angalia watu waliokuwa wanapigia kelele nyingi sana UKUTA ifanyike bila kujali dalili za matokeo yake.
Sijui wakati huu tungekuwa tunasemaje!
Fafanua zaidi.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
Vuta pumzi, nadhani sasa unapost tu bila ya kuwaza unachopost!
Maneno haya niliyo'quote' hukuyapa fikra ya kutosha.
 
Vuta pumzi, nadhani sasa unapost tu bila ya kuwaza unachopost!
Maneno haya niliyo'quote' hukuyapa fikra ya kutosha.
Nimeyaelewa ndiyo maana nikajibu hivyo, gari inapoharibika huwezi kukimbilia kubadili injini.
 

Quinine katika watu ninaowaheshimu hapa jukwaani ww ni mmojawapo. Hii post yako inaisifu cdm kama taasisi imara, sasa taasisi imara isiyoweza kupata mwenyekiti zaidi ya Mbowe, tena humo ndani kuna wasomi kibao hapo unamaanisha nini boss?. Hivi Mbowe akifa hii leo ndio cdm haitakaa iwe na mwenyekiti!? Hapo cdm ikiitwa ni genge utakataa?
 
Tuje kwenye hili la Mbowe, ukweli ni kuwa Mbowe ni jabali hasa na mhimili halisi wa cdm, lakini hili suala la kwamba sio muda muafaka Mbowe kuachia madaraka silipendi sana kwani hata wakati wa JK ilisemwa hivyo hivyo
Sikujua kuwa kuna aliyesema muda haukuwa mwafaka kwa JK kuachia madaraka! Nilikuwa nimechoka sana na kusubiri aondoke.

Siyo sahihi kulinganisha kutoka kwa JK na Mbowe kwa aina zote unazoweza kuzilinganisha.

Mimi ninakubaliana na wewe juu ya Mbowe na viongozi wenzake ndani ya chama, wakati utakaporuhusu; yaani baada ya uchaguzi mkuu wa 2020; CHADEMA waitishe uchaguzi wawapate viongozi wao.

Hili hawawezi wakalifanya wakati huu bila ya kuhatarisha usalama wa chama chao. CCM wana nyenzo zote wanazohitaji kuwavuruga na wasiweze hata kushiriki uchaguzi mwaka huu na mwakani.

Itashangaza sana kwa kiongozi yeyote kutoka CHADEMA kupigia kelele uchaguzi ndani ya chama wakati huu.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.

Quinine naona ni bora upumzike hii mada imekuwa nzito kwako, post ya mwenyekiti wa cdm ni post sensitive kuliko post ya urais!? Kama mtu alikuja akiwa na wiki 2 alipewa post ya kugombea urais itakuwa hiyo ya uenyekiti wa cdm? Kuna post sensitive nchi hii kuliko ya urais. Sikuwahi kujua kama ww ni mwepesi kiasi hiki, na ndio maana unaamini kwamba Mbowe tu ndio anaweza kuwa mwenyekiti cdm. Kama ni Mbowe tu ndio anaweza kuwa mwenyekiti ndani ya cdm basi hapo hamna chama boss.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
"Post ya Mkti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere"?

Nimeyaelewa ndiyo maana nikajibu hivyo, gari inapoharibika huwezi kukimbilia kubadili injini.

Viongozi na wanachama waliomo CHADEMA ni "watu wowote from nowhere?"

Basi sawa!
 
Mkuu ndiyo maana nikasema tujaribu kuwa specific tuanze kujadili nani anaweza kuvaa viatu vya Mbowe siyo dhambi kuwajua kwa majina, mbona wenye uwezo wa kuwa makatibu wakuu makatibu wenezi wanaoweza wanatajwa kuwa Marcos Albanie, Heche, Msigwa, Malisa kwanini post ya Mkiti hatutaji?
 

Kalamu1 usiwe mwepesi, ccm kama ni kuivuruga cdm imeshaivuruga na wala hawamuogopi Mbowe. Kama Mbowe kakaa ndani miezi minne itakuwa kuogopa huo uenyekiti wake? Cdm si inaporwa ushindi wake kwenye chaguzi kimachomacho na Mbowe akiwa mwenyekiti amefanyaje? Mali ngapi za Mbowe zimevurugwa na hana lolote alilofanya? Ukiniambia viongozi wa cdm hakuna anayetaka kugombea uwenyekiti nitakuelewa lakini sio kwamba Mbowe ndio mwenye uwezo kulingana na wakati wa sasa. Kama cdm ni taasisi basi utetezi wa kwamba Mbowe ndio anayefaa tu kwenye uenyekiti ni utani wa mchana kweupe.
 
Niliyeanzisha mada ni mimi naijua uzito wake inawezekana wewe hujui hata lengo lake, hii mada ni pana nyie mmedandia sehemu ndogo sana ya mada husika 'uenyekiti wa Mbowe' na mimi naenda na nyie, akitokea mwingine tutajadili mafanikio ya Chadema nk, usichanganye mada kusema sensitive nalinganisha na posts ndani ya chama siyo nje ya chama, kwenye chama Mkiti ndiye kichwa cha chama.
 
Kwani katiba inasemaje, si ni mwaka huu ndio wanapashwa kufanya uchaguzi, nafikiri uchaguzi wa mwisho wamefanya 2014 kama sikosei.

Na kwa hizi sheria za sasa zinazomfanya msajili kuwa Mungu mtu nahisi atawashinikiza wafanye kwa amri kutoka juu.
 

Anayeweza kuwa katibu mkuu anaweza kuwa mwenyekiti pia. Labda kama uniambie cdm haiendeshwi kama taasisi bali kama kampuni ya watu fulani ambayo vyanzo vyake vya mapato vinategemea mifuko ya hao matajiri. Hapa ninachokiona ni kwamba unapima upepo uone ni nani anatajwa kwenye nafasi hiyo. Kama Mbowe analeta pesa zake za mfukoni kuendesha chama una haki ya kusema hakuna anayeweza kuwa mwenyekiti kwani akiwa mwenyekiti inabidi aje na hela zake. Sasa kama cdm kinaendeshwa kwa fedha za mwenyekiti hapo ujue hamna chama kuna kundi la wajanja.
 

Nikurahisishie kama hii mada ni nzito na ww tu ndio unaujua uzito wake basi huku jukwaani ulipoileta sio sehemu sahihi. Hapa umeleta mada ya ofisi jukwaani ambapo huku tuko huru hatujali mipaka ya huko ofisini kwenu. Siku nyingine mada ya huko ofisini bakini nayo ikija hapa tunaichambua bila woga wala mipaka. Unasema mada ni pana lakini wakati huohuo unaiwekea mipaka!! Mkuu kubali tu leo umejichanganya, kajipange upya sio wote ni wepesi kwa kiwango unachodhani.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
QUININE hapa umepotoka sana, na kwa hoja unapaswa kuwaomba radhi wanachadema wote humu Jamvini.

Hivi Lowassa na JUMA Duni walikuwa wanachadema from somewhere ila wanachadema wengine ni from nowhere to deserve uenyekiti wa chama ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Angalau sasa tunaanza kujuana rangi it was just a matter of time,
Tangu uanze kujadili point yako kuu ni Mbowe, huendi zaidi ya kuongelea Mbowe kakaa muda mrefu, umeshaeleweka ni muda wa kuwaachia wenye mawazo tofauti na Mbowe kuachia madaraka. Kwa heri if you don't mind.
 
Ni mawazo yangu niombe radhi kutoa maoni yangu,

Lowassa na Duni waligombea wenyekiti?
 
Kwahiyo kama tumedandia mada ulitaka uanzishe mada uchangie peke yako tu ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…