CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu

CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
24,148
Reaction score
56,422
Kuna watu wanaifananisha Chadema na NCCR Mageuzi, wanaifananisha Chadema na CUF wengine wamefikia kuifananisha Chadema na ACT Wazalendo, hawako sahihi hawajui historia yake.

Chadema haikufika pale ilipo kwa kubebwa na vyombo vya dola imepambana kwa jasho la damu, haijafika hapo kwa kupata wanachama wa mkupuo wanachama wa mafuriko kama ilivyopata NCCR 1995 wakati Mrema alipohama CCM au kama ACT Wazalendo inavyopata wanachama wengi (Zanzibar) baada ya Maalimu Seif kuhama CUF. Chadema imewajenga wanachama na viongozi wake kutoka mashinani, wengi wa viongozi wake imewa groom yenyewe, Mnyika, Zitto, Mbowe, Mdee, Heche, Kafulila, Katambi nk.

Waliosahau historia ya Chadema naomba niwakumbushe kidogo. Mwaka 1994 Chadema ilikuwa na Madiwani 13 tu Tanzania nzima haikuwa na Halmashauri hata moja. Mwaka 1995 ilikuwa na Wabunge wanne (4). Mwaka 2000 ilipata Madiwani 45 tu nchi nzima. Kwa hiyo safari ya Chadema siyo ya kuangalia leo, yanayo wakuta ndugu zake ACT Wazalendo wao yaliwakuta zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Chadema ina wanachama wenye imani na damu ya demokrasia, wanaharakati, wanachama wake wengi siyo wanaofuata mtu, ina wanachama na wapenzi waliojitoa.

Kuwa mwanachama wa Chadema lazima u-risk kazi yako ref. Prof. Baregu, u-risk maisha yako ref. Tundu Lissu, u-risk biashara zako ref. Mbowe. Kama huna moyo wa kiuana mapinduzi, una tamaa ya utajiri, tamaa ya kazi serikalini, tamaa ya tenda Chadema siyo sehemu yako. Alikuwepo Dr. Slaa kaondoka mwenyewe, alikuja Lowassa na watu wake kaondoka na watu wake kaiacha Chadema na watu wake wasioyumba.

Chadema inajengwa na mfumo ambao unafika hadi vijijini kwenye mashina si rahisi kuuvunja, Chadema ya leo haina tofauti na Chama cha Mapinduzi CCM, imejengeka ki taasisi zaidi, CCM hata aondoke Magufuli itabaki kuwa CCM, vivyo hivyo Chadema hata aondoke Mbowe itabaki kuwa Chadema, si rahisi kuilinganisha na vyama vingine, vitakuja vitapata umaarufu na kama havitasimamia misingi vitaondoka na kuiacha Chadema.

Mchambuzi huru mwana JF Quinine.
 
Ata mwenyewe jiwe anajua siku akirudi kwao chattle na kuanza lima kwa bustani ya dada yake Moni na kufuga mbuzi hapo ndipo atakapoelewa nini
FB_IMG_1552336612225.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila Chadema inatakiwa kuondokana na mamluki kama ilivyo kwa Sumaye .

Chadema haiwezi kuchukua dola kwa kuendelea kuwategemea CCM.


Tunataka chadema mpya yenye watu wenye ushawishi ma uthubutu kama ilivyo kwa Lissu, Heche,Lema na Sugu ..

Watu Mbogo hawahitajiki Chadema kama mnataka kuchukua Dola..
 
Mkuu mimi nina maoni mawili tu hapa:

Mosi, kitu kimoja kikubwa CHADEMA haina, ambacho nadhani ni muhimu kwa siasa za Afrika ni kuwa na wanachama watiifu ambao ni watu kutoka vyombo vya dola kama TISS, JWTZ, POLISI na Mahakama.

Hili ndilo linawabeba CCM na kuwapa kiburi cha kufanya watakavyo hapa nchini bila hata kuzingatia miiko ya kisheria.

CHADEMA kimejitahidi sana kufika vijijini kuliko vyama vingine vya upinzani. Lakini bahati mbaya sana ni kwamba chaguzi za Afrika hazifanikishwi kwa boski la kura peke yake, lazima mkono wa dola utumike tu.

Pili, kitu kingine kikubwa zaidi na muhimu ambacho CUF inacho ambacho vyama vingine vya upinzani havina ni kwamba CUF imewahi kufanikiwa kushika dola kule Zanzibar kwa nguvu zao wenyewe kabla hata ya UKAWA kuzaliwa.

Walifanikiwa kuunda Serikali ya Umoja ya Zanzibar na kutoa Makamu wa Raisi: Hivyo nadhani kwenye suala zima la uzoefu wa kiuongozi CUF watakuwa wako mbele kidogo ya CHADEMA. Pia mtandao wao kule visiwani ni mkubwa sana kuliko chama chochote cha upinzani hapa Tanzania.
 
Mleta uzi uko sahihi sana kuhusu cdm. Ila cdm 2015 ilituangusha sana kwa tamaa ya viongozi wachache kukubali kuchukua asali ya Lowassa na kumpa nafasi adhimu mzee toka ccm aliyetaka urais tu bila kujali chama. Lile ni kosa la wazi na kubwa sana kufanywa na taasisi. Sikutegemea taasisi kubwa kama cdm ingeweza kufanya maamuzi mazito kwa kuchukua mgombea ambaye hata Mimi nisiyejua siasa nilijua kabisa ni kosa la dhahiri. Kwa kosa lile ni dhahiri Mbowe anapaswa kuachana na uenyekiti na kumuachia mtu mwingine ili tuanze upya.

Halafu cheo muhimu cha katibu mkuu ndani ya cdm kimepwaya mno kiasi kwamba kuendelea kuwa na katibu mkuu kama huyo ni kosa kubwa. Kwa sasa tunapaswa kuwa na katibu mkuu mtu kama Heche au Marcos Albanie. Huyo katibu mkuu wa sasa kachangia kuifubaza sana cdm.
 
tindo,
Nakubaliana na wewe Mbowe kwa wadhifa wake alifanya kosa lkn haliwezi kufifisha juhudi anazofanya, kusema aachie uenyekiti humtendei haki kwa sababu uamuzi ulifanywa na kamati nzima.

kuhusu katibu Mkuu ni kweli kaifanya Chadema nzima ipoe nilishawahi kushauri kitu kama hicho,

Kuna haja ya CHADEMA kubadilika kuendana na hali halisi
 
Nakubaliana na wewe Mbowe kwa wadhifa wake alifanya kosa lkn haliwezi kufifisha juhudi anazofanya, kusema aachie uenyekiti humtendei haki kwa sababu uamuzi ulifanywa na safari nzima.

kuhusu katibu Mkuu ni kweli kaifanya Chadema nzima ipoe.

Mimi sisemi Mbowe apumzike uenyekiti kisa hilo kosa la Lowassa tu, bali ameshakaa madarakani kwenye nafasi ya uenyekiti zaidi ya miaka 15, hapo ndio dhana ya taasisi ingepata maana kwa kuchagua mwenyekiti mwingine. Jaribu kuangalia kiongozi mzuri ni ndani ya miaka kumi tu kwenye nafasi moja, lakini akizidi miaka kumi huanza kuongoza kwa mizengwe na maamuzi kama hayo ya kumpokea Lowassa. Hili wala halihitaji ubishani kwani ndio uhalisia. Mwisho kabisa wa ubora wa Mbowe ilikuwa ni 2015 hata kama cdm ingetoa rais, ukweli uwezo wake kwa sasa umefikia ukingoni.
 
Kuna watu wanaifananisha Chadema na NCCR Mageuzi, wanaifananisha Chadema na CUF wengine wamefikia kuifananisha Chadema na ACT Wazalendo, hawako sahihi hawajui historia yake.

Chadema haikufika pale ilipo kwa kubebwa na vyombo vya dola imepambana kwa jasho la damu, haijafika hapo kwa kupata wanachama wa mkupuo wanachama wa mafuriko kama ilivyopata NCCR 1995 wakati Mrema alipohama CCM au kama ACT Wazalendo inavyopata wanachama wengi baada ya Maalimu Seif kuhama CUF. Chadema imewajenga wanachama na viongozi wake kutoka mashinani, wengi wa viongozi wake imewa groom yenyewe, Mnyika, Zitto, Mbowe, Heche, Kafulila, Katambi nk.

Waliosahau historia ya Chadema naomba niwakumbushe kidogo. Mwaka 1994 Chadema ilikuwa na Madiwani 13 tu Tanzania nzima haikuwa na Halmashauri hata moja. Mwaka 1995 ilikuwa na Wabunge wanne (4). Mwaka 2000 ilipata Madiwani 45 tu nchi nzima. Kwa hiyo safari ya Chadema siyo ya kuangalia leo, yanayo wakuta ndugu zake ACT Wazalendo wao yaliwakuta zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Chadema ina wanachama wenye imani na damu ya demokrasia, wanaharakati, wanachama wake wengi siyo wanaofuata mtu, ina wanachama na wapenzi waliojitoa.

Kuwa mwanachama wa Chadema lazima u-risk kazi yako ref. Prof. Baregu, u-risk maisha yako ref. Tundu Lissu, u-risk biashara zako ref. Mbowe. Kama huna moyo wa kiuana mapinduzi, una tamaa ya utajiri, tamaa ya kazi serikalini, tamaa ya tenda Chadema siyo sehemu yako. Alikuwepo Dr. Slaa kaondoka mwenyewe, alikuja Lowassa na watu wake kaondoka na watu wake kaiacha Chadema na watu wake wasioyumba.

Chadema inajengwa na mfumo ambao unafika hadi vijijini kwenye mashina si rahisi kuuvunja, Chadema ya leo haina tofauti na Chama cha Mapinduzi CCM, imejengeka ki taasisi zaidi, CCM hata aondoke Magufuli itabaki kuwa CCM, vivyo hivyo Chadema hata aondoke Mbowe itabaki kuwa Chadema, si rahisi kuilinganisha na vyama vingine.

Mchambuzi huru mwana JF Quinine.
Shughuli za chama zinaendelea kila kona ya nchi..jpg
[AT
 
Mleta uzi uko sahihi sana kuhusu cdm. Ila cdm 2015 ilituangusha sana kwa tamaa ya viongozi wachache kukubali kuchukua asali ya Lowassa na kumpa nafasi adhimu mzee toka ccm aliyetaka urais tu bila kujali chama. Lile ni kosa la wazi na kubwa sana kufanywa na taasisi. Sikutegemea taasisi kubwa kama cdm ingeweza kufanya maamuzi mazito kwa kuchukua mgombea ambaye hata Mimi nisiyejua siasa nilijua kabisa ni kosa la dhahiri. Kwa kosa lile ni dhahiri Mbowe anapaswa kuachana na uenyekiti na kumuachia mtu mwingine ili tuanze upya.

Halafu cheo muhimu cha katibu mkuu ndani ya cdm kimepwaya mno kiasi kwamba kuendelea kuwa na katibu mkuu kama huyo ni kosa kubwa. Kwa sasa tunapaswa kuwa na katibu mkuu mtu kama Heche au Marcos Albanie. Huyo katibu mkuu wa sasa kachangia kuifubaza sana cdm.
Mingu ni mwema kuruhusu hilo kosa kuliko wangendelea kushirikiana na lipumba..kozi lipumba angendelea kuwepo ukawa..
 
Vipofu wanaongozana na kufarijiana eti Chadema itadumu, mwenye akili timamu anatambua kuwa wali wa kushiba huonekana kwenye Sahani hivyo 2020 Chadema +Cuf+ACT=NLD ya leo, time will tell

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila katibu mkuu yupo pale ilu kuondoa habari mzima ya ukabila

Sent using Jamii Forums mobile app

Hiyo ni dhana ya kipuuzi sana, kabla yake katibu mkuu alikuwa Slaa na dhana ya uchaga/ukaskazini ikiwa imepamba moto lakini cdm kilikubalika nchi nzima. Leo hiyo dhana haipo kisa hakuna mtu anayefanya kazi yake sawasawa. Huwezi kuchagua mtu mwenye uwezo hafifu kisa adui yako anakutuhumu kwa dhana za kijinga.
 
Mkuu usiwe loyal kwa chama chochote, kuwa loyal kwa UPINZANI
Tunahitaji Chadema na vyama vingine vya upinzani viunganishe nguvu ili kuing'oa CCM fullstop!.

Kinachotokea leo ACT, ni mkondo wa umeme tu kutoka CUF ya zamani kutafuta waya mwingine wa kupita na hivyo kupitia ACT lakini upinzani ni ule ule.

leo hii hata kama ACT itafanyiwa figisu, mkondo uleule utakwenda kupitia kwa CHAUMA ya Hashim Rungwe!.
 
Kuna watu wanaifananisha Chadema na NCCR Mageuzi, wanaifananisha Chadema na CUF wengine wamefikia kuifananisha Chadema na ACT Wazalendo, hawako sahihi hawajui historia yake.

Chadema haikufika pale ilipo kwa kubebwa na vyombo vya dola imepambana kwa jasho la damu, haijafika hapo kwa kupata wanachama wa mkupuo wanachama wa mafuriko kama ilivyopata NCCR 1995 wakati Mrema alipohama CCM au kama ACT Wazalendo inavyopata wanachama wengi baada ya Maalimu Seif kuhama CUF. Chadema imewajenga wanachama na viongozi wake kutoka mashinani, wengi wa viongozi wake imewa groom yenyewe, Mnyika, Zitto, Mbowe, Heche, Kafulila, Katambi nk.

Waliosahau historia ya Chadema naomba niwakumbushe kidogo. Mwaka 1994 Chadema ilikuwa na Madiwani 13 tu Tanzania nzima haikuwa na Halmashauri hata moja. Mwaka 1995 ilikuwa na Wabunge wanne (4). Mwaka 2000 ilipata Madiwani 45 tu nchi nzima. Kwa hiyo safari ya Chadema siyo ya kuangalia leo, yanayo wakuta ndugu zake ACT Wazalendo wao yaliwakuta zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Chadema ina wanachama wenye imani na damu ya demokrasia, wanaharakati, wanachama wake wengi siyo wanaofuata mtu, ina wanachama na wapenzi waliojitoa.

Kuwa mwanachama wa Chadema lazima u-risk kazi yako ref. Prof. Baregu, u-risk maisha yako ref. Tundu Lissu, u-risk biashara zako ref. Mbowe. Kama huna moyo wa kiuana mapinduzi, una tamaa ya utajiri, tamaa ya kazi serikalini, tamaa ya tenda Chadema siyo sehemu yako. Alikuwepo Dr. Slaa kaondoka mwenyewe, alikuja Lowassa na watu wake kaondoka na watu wake kaiacha Chadema na watu wake wasioyumba.

Chadema inajengwa na mfumo ambao unafika hadi vijijini kwenye mashina si rahisi kuuvunja, Chadema ya leo haina tofauti na Chama cha Mapinduzi CCM, imejengeka ki taasisi zaidi, CCM hata aondoke Magufuli itabaki kuwa CCM, vivyo hivyo Chadema hata aondoke Mbowe itabaki kuwa Chadema, si rahisi kuilinganisha na vyama vingine.

Mchambuzi huru mwana JF Quinine.
Wewe nadhani utakuwa unaumwa ugonjwa wa kulewa uongo uongo wa wapinzani, yaani hicho chama kwanza hakipo kabisa, kimepotea kabisa kabisa, yaani kilichobaki ni kakikundi ka watu fulani wenye kuendesha majungu majungu. CCM ni CCM wala huwezi kufananisha na hicho kikundi
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Back
Top Bottom