CHADEMA isitafute mchawi, ni Mbowe

CHADEMA isitafute mchawi, ni Mbowe

Mkuu @Rutasubanyuma hili ni andiko zito sana kutoka kwa mshabiki au mwanachama wa Chadema ndani na pengine nje ya JF.
Nafahamu ulivyokuwa mtetezi mkuu wa Chadema hapa jamvini na of course kwenye field huko kwenye chimbuko la harakati kali za Siasa za upinzani kupitia Chadema.

Nakumbuka tuliwahi kuingia kwenye mikwaruzano mikali ya hoja katika threads na posts mbalimbali hapa jamvini.

Nilikuwa nashangaa sana kukuona ukiitetea Chadema iliyobadili gia angani na nikawaza hivi huyu great thinker na wengine unaofanania nao wanahitaji nini haswa kwa Taifa hili?
Yaani kuna kipindi mlikuwa mnaupinga ufisadi na magumashi ya CCM katika hali zote sasa ikawaje mkabadilika na kumuunga mkono mwanaccm aliyeichafua CCM?ikawaje mkambadilikia Slaa na kumuona ni wa hovyo kabisa?

Jibu langu likawa mtakuwa na maslahi muhimu ndani ya Chadema na hamtaki yavurugwe hata kama gharama yake ni kuusaliti ule umma uliokuwa unapinga ufisadi.

Leo hii ninapoona hii post ninashangazwa sana na kutoamini...au account yako imekuwa hacked?

Au kwa mara ya kwanza umeweza kupata fursa ya kumjua mbowe na inner cycle ya Chadema?

Kwa ufupi nakubaliana na wewe kuwa Ni heri ya ZIMWI LIKUJUALO...yaani CCM na changamoto zake ni bora sana mara 10000 kuliko Chadema iliyokaa kimaslahi zaidi.

The good thing about CCM wana machinery za kuwawajibisha mafisadi ,wezi na wahuni waliomo chamani na hivyo kuwa na uwezo wa kudhibiti Chama kuwa mateka wa watu wabaya.

Again...IAM PERPLEXED!!

Cc: BAK Crashwise Pascal Mayalla @TumainMakene wilbrod slaa Tundu Lissu
Yericko Nyerere Mchambuzi @mzeemwanakijiji
mtaishia kuoana tu kama shaka s.shaka alivyoolewa na salehe mpelembwe huko tanga hakuna lolote hapo.kama chadema imekufa mbona mnaua wanafunzi lwa risasi.za moto mkozuia maandamano? kama imekufa mbona viongozi karibu wote wapo mahakamani kwa kesi za kipuuzi. iv ni nani anaiua chadema kati ya yule anayewanunua viongozi na wanachama wake na yule anayetafutwa ili auwawe.
jinga lao una upeo mdogo sana kichwani nadhani ni kule kuiba mitihani
 
mtaishia kuoana tu kama shaka s.shaka alivyoolewa na salehe mpelembwe huko tanga hakuna lolote hapo.kama chadema imekufa mbona mnaua wanafunzi lwa risasi.za moto mkozuia maandamano? kama imekufa mbona viongozi karibu wote wapo mahakamani kwa kesi za kipuuzi. iv ni nani anaiua chadema kati ya yule anayewanunua viongozi na wanachama wake na yule anayetafutwa ili auwawe.
jinga lao una upeo mdogo sana kichwani nadhani ni kule kuiba mitihani
povu haliondoi ukweli wa kifo cha chadema!
Elewa hoja ya mleta thread ambaye ni mwenzenu.
 
Ccm kila wakilala wakiamka ni mbowe.Kama anaiuwa chadema si mfurahi sasa?mbona mnalalama tena?
 
Siamini na simtki kuamini kabisa kwamba chama kilichoasisi mapinduzi Tanzania kama kinavyojinasibu leo hii kinaambulia kununua watanzania maskini kabisa ; hata kwenye vitabu vya dini hii ni dhambi isiyo na msamaha - kununua haki; yaani chama kinanunua haki kweli kweli
 
Una kiwango cha chini sana cha uelewa au unatumika kipropaganda. Fedha zote za chama zinaidhinishwa kwa mfumo rasmi na pia zinakaguliwa kila mwaka na CAG na kutoa ripoti. Jee hayo unayosema ya matumizi mabaya umeyatoa kwenye ripoti ya CAG au katika vibaraza vya Lumumba?
Hizo story zenu mbona zimeshachacha?

CAG ameshawahi kuipa CHADEMA hati safi?

Kwanini kwa miaka zaidi 20 tangu iundwe hawajawahi kupata hati safi wakikaguliwa hesabu zao?
 
Unajua hata tuichukie CCM kwa kiwango gani lakini kwa upinzani huu chini ya Mbowe mtabaki na maumivu tu. CCM imezoea kuua sisimizi kwa nyundo ndio maana hata wakati huu CDM ikiwa dhaifu na ungwaji mkono mdogo kuliko wakati wowote lakini bado CCM wanatumia hila hadi aibu!

Watu wanajitenga na siasa ....vijana wenye jasho lao CDM kama Mnyika ni kama wanaomba ifike 2020 waangalie mambo mengine ....gia za angani za Mbowe zilivuruga watu wengi na ameshindwa kujirekebisha ili walau abaki na heshima yake kutokana na mchango wake.

Chama hakina uelekeo kwasasa zaidi ya kupandia madhaifu yanaibuka awamu hii kuliko mikakati ya kueleweka! Bila matukio huwezi kuisikia CDM! Imagine nyimbo ya Roma kufungiwa Bavicha wanaibuka!!! Wengine wanaridhika na kelele za baadhi ya jumuiya dhidi ya serikali wakifikiri chama ndio kinapigwa jeki!!

Jumuiya zipo na zitapiga kelele kila inapobidi na zipo hadi nchi zilizoendelea lakini hapa kwetu wapinzani wakisikia kelele zao wanafikiri ni wenzao ....wanawasemea ....hawana mikakati ya kueleweka ....
 
Huku JF kuna watu wanadukua a/c za watu?
Hivi ni kweli hili bandiko amelitoa mtoa mada? sitaki kuamini. Mleta mada ni CDM blood blood. Mods angalieni isije ikawa akaunti yake imehakiwa
 
Anayeiua Chadema ni Mbowe na ufisadi wake. Hela ya ruzuku anaitafuna kwa visingizio kebekebe. Utasikia alikopesha chama mabilioni wakati wa uchaguzi sasa anakidai chama mrejesho.

Swali ni vikao vipi viliidhinisha mikopo hiyo? Pili, mwenzetu ni benki? Tatu, hizo fedha alizitoa wapi kwa shughuli ipi? Nne, kwa matumizi yapi kwani sheria za uchaguzi zimeweka ukomo wa matumizi ya chaguzi.

Sasa kwa huu ufisadi Chadema imeshindwa kupeleka fedha mashinani na matokeo yake ukata umechangia baadhi ya madiwani kurubuniwa na ccm. CCM imegundua huu udhaifu wa Mbowe na wameugeuza kivuno.

Sasa wa kulaumiwa ni nani?

Pili, ujio wa Lowassa na kumkabidhi ugombea Urais aligeuza ni dili yake binafsi na kauli zake zinamtia hatiani. Alidai yeye ni nani amkatae Lowassa ambaye alikuja na wafuasi wengi.

Maswali yafuatayo hayana majibu..

Kwanza Mbowe wewe ni nani hadi uone suala la kugombea Urais ni lake binafsi? Kiongozi anayejiheshimu angesema tuwaulize wanachama kwa kura yao kupitia primaries ya mikutano ya wilaya nchi nzima waamue na kila anayetaka kugombea achukue fomu na wanachama waamue.

Pili, nafasi mbalimbali za uongozi kamati kuu ya cdm hutapika majina lakini wanachama hawaulizwi sasa ni demokrasia ipi mwenzetu anaitafuta wakati nafasi hii ndogo Mwenyezi Mungu aliyompa kashindwa kuonyesha wasifu wake wa demokrasia?

Tatu, hivi mwenzetu ulijuaje Lowassa kaja na wafuasi wengi kama siyo hisia zako binafsi? Labda utuelimishe kabla Lowassa kujiunga na cdm mlikuwa na wanachama wangapi na baada ya kujiunga mkawa na wanachama wangapi. Kwa taarifa yako, kwa takwimu nilizonazo idadi ya wanachama haikuongezeka eti kwa sababu Lowassa alijiunga na cdm. Hizi takwimu hukuziongelea kwa sababu uliona zingelikuumbua.

Maandiko yako wazi kama huaminiki kwa madogo nani atakuamini kwa makubwa hata yawe ni yako?

CCM ina matatizo yake na ingepaswa kuwajibishwa lakini kwa uongozi huu dhaifu wa Mbowe ambao sanasana ni mkao wa kula ni kheri kabisa ccm wakaendelea kutesa hadi pale wanachama wa Chadema watakapofanya kweli na kumtimua huyu fisadi mkubwa na wakajipanga upya.

Vinginevyo mtabakia kulalama badala ya kujilaumu wenyewe.

N.B:-

Dola ina jukumu kubwa la kulinda ruzuku zinazopewa vyama vyote vya siasa na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa na hii siyo siasa ila ni utawala bora.
Label some one with an ugly image so that there is 'justification' for elimination
 
Rutta Chadema inamjua sana mchawi wake. Ni kile Chama kinachoogopa mikutano, maandamano n.k
 
Anayeiua Chadema ni Mbowe, au ni wale wanaonunua madiwani?.
 
Swali ni moja vyama vipo porini, jungle war hakuna sheria za kuzisimamia. Ama inabid uchutame.
 
Hizo pesa za walipakodi nani ana jukumu la kuzikagua? Tumuamini na kwa mengine iwapo hili kalinyamazia mnalalamika kwenye keyboard?, au mnawafanya watu hamnazo?
Kila unapotaka kuligusia hili la fedha na ruzuku ndani ya Chadema lazima parazuka drama ya kulipotezea
 
Wanajukwaa mtakumbuka tangu Mbowe alipobadili gia angani Julai 2015 CHADEMA kumeingia ganzi kwa kushindwa kujigamba mbele za watu tena kwamba ni chama kinachopiga vita ufisadi na ni chama cha wanyonge.

Sasa CHADEMA kimebaki kusubiri kudandia hoja badala ya kufanya siasa kisayansi kama alivyowahi kuwaasa balozi Wilbrod Slaa hapo nyuma.

Je kubadili gia angani kulikuwa ni asset au liability kwa CHADEMA?

Vijana wa Ufipa leteni majibu tafadhali, mchezo huu hauhitaji hasira jamani.

Chilonwa.
 
Wanajukwaa mtakumbuka tangu Mbowe alipobadili gia angani Julai 2015 CHADEMA kumeingia ganzi kwa kushindwa kujigamba mbele za watu tena kwamba ni chama kinachopiga vita ufisadi na ni chama cha wanyonge.

Sasa CHADEMA kimebaki kusubiri kudandia hoja badala ya kufanya siasa kisayansi kama alivyowahi kuwaasa balozi Wilbrod Slaa hapo nyuma.

Je kubadili gia angani kulikuwa ni asset au liability kwa CHADEMA?

Vijana wa Ufipa leteni majibu tafadhali, mchezo huu hauhitaji hasira jamani.

Chilonwa.
Mavi.
 
Back
Top Bottom