CHADEMA isitafute mchawi, ni Mbowe

CHADEMA isitafute mchawi, ni Mbowe

Hivi Ruta...,
huko ccm huwa mnapewa ukada kwa kutegemea kiwango cha umbumbumbu ulio nao..?!

CCM ina Raisi, Polisisiem, Tissisiem .., Takukurusisiem.., Tume ya Unyanganyi wa Kura.., Wakuu wa Mikoa na Wilaya , Mahakamasisiem.., Jeshi la Wana sisiem.., halafu bado wewe na VILAZA wenzio mnakuja huku mitandaoni kulialia kuhusu Mbowe kama vile hamna nguvu...?!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mmeitana kutoka huko mafichoni ili mje ajazike kwenye huu upuuzi wenu
Kujibu hoja nzito kwa majibu mafupifupi ya matusi ni kuzomea.
Kuzomea mtu ama kuzomea kiongozi hakufanywi kwa utashi wa hekima ama busara za mzomeaji kwa muktadha wa kuguswa na hisia fulani, bali kuna msukumo bila ridhaa ya mzomeaji toka kwa 'mastermind', ni utovu wa heshima.
Zomeazomea huwa ni malipo ya hongo ya vitu vidogo vidogo mfano wa 'sheli' la pombe za kienyeji, sahani ya pilau ama ukabila na ukanda.
Wakishamaliza kuzomea, huwa tayari wamelipia walichokula ama kulipwa na kuendelea na shughili zao.
Sasa humu kwa great thinkers nani analipia wazomeaji wa namna hii?
 
Ngoja nione Leo timu Ufipa watajibu hoja kwa hoja au ndo yaleyale ya Lumumba hoja kwa matusi na kejeli nataka nione utofauti wao.
 
Kazi yenu, kukenua, wakati mnaumia, aliyewaita nyumbu hakukosea.
 
Una kiwango cha chini sana cha uelewa au unatumika kipropaganda. Fedha zote za chama zinaidhinishwa kwa mfumo rasmi na pia zinakaguliwa kila mwaka na CAG na kutoa ripoti. Jee hayo unayosema ya matumizi mabaya umeyatoa kwenye ripoti ya CAG au katika vibaraza vya Lumumba?
Hizo story zenu mbona zimeshachacha?
Ni lini CDM wamepata hati safi kutoka kwa CAG, tangu CAG aanze kukagua matumizi ya vyama vya siasa CDM imepata hati chafu kwa miaka yote.
 
Ni lini CDM wamepata hati safi kutoka kwa CAG, tangu CAG aanze kukagua matumizi ya vyama vya siasa CDM imepata hati chafu kwa miaka yote.
Ni lini Chadema wamepata hati chafu? tofautisha hati chafu na hati yenye mashaka. Kama hujui hilo tafata Mhasibu anayejua nini maana yake atakuambia.
Na hakuna chama chochote kikubwa kimewahi kupata hati safi toka vianzishwe
 
Hauna hoja, pesa za ruzuku kwani waga wanagawiwa madiwani ili kuwazuia wasinunuliwe na ccm?

Mbona usihoji pesa za ruzuku za ccm zinaenda wapi wala ukiukwaji wa haki za binadamu ambao hadi wazungu ughaibuni wanaona. You're definitely out of touch with reality.
 
Kujibu hoja nzito kwa majibu mafupifupi ya matusi ni kuzomea.
Kuzomea mtu ama kuzomea kiongozi hakufanywi kwa utashi wa hekima ama busara za mzomeaji kwa muktadha wa kuguswa na hisia fulani, bali kuna msukumo bila ridhaa ya mzomeaji toka kwa 'mastermind', ni utovu wa heshima.
Zomeazomea huwa ni malipo ya hongo ya vitu vidogo vidogo mfano wa 'sheli' la pombe za kienyeji, sahani ya pilau ama ukabila na ukanda.
Wakishamaliza kuzomea, huwa tayari wamelipia walichokula ama kulipwa na kuendelea na shughili zao.
Sasa humu kwa great thinkers nani analipia wazomeaji wa namna hii?
Mbona unataja tabia za ccm vijijini kk ndio michezo yenu kununua pombe za kienyeji na vitenge kuwarubuni maskini ccm should stop that habit
 
Wanabodi


Barua ya msajiri kwa CDM, haina uzito wowote wala uhalari wa kisheria. Lengo mahususi ni kuhamisha watu kwenye reli.
Anayeiua Chadema ni Mbowe na ufisadi wake. Hela ya ruzuku anaitafuna kwa visingizio kebekebe. Utasikia alikopesha chama mabilioni wakati wa uchaguzi sasa anakidai chama mrejesho.

Swali ni vikao vipi viliidhinisha mikopo hiyo? Pili, mwenzetu ni benki? Tatu, hizo fedha alizitoa wapi kwa shughuli ipi? Nne, kwa matumizi yapi kwani sheria za uchaguzi zimeweka ukomo wa matumizi ya chaguzi.

Sasa kwa huu ufisadi Chadema imeshindwa kupeleka fedha mashinani na matokeo yake ukata umechangia baadhi ya madiwani kurubuniwa na ccm. CCM imegundua huu udhaifu wa Mbowe na wameugeuza kivuno.

Sasa wa kulaumiwa ni nani?

Pili, ujio wa Lowassa na kumkabidhi ugombea Urais aligeuza ni dili yake binafsi na kauli zake zinamtia hatiani. Alidai yeye ni nani amkatae Lowassa ambaye alikuja na wafuasi wengi.

Maswali yafuatayo hayana majibu..

Kwanza Mbowe wewe ni nani hadi uone suala la kugombea Urais ni lake binafsi? Kiongozi anayejiheshimu angesema tuwaulize wanachama kwa kura yao kupitia primaries ya mikutano ya wilaya nchi nzima waamue na kila anayetaka kugombea achukue fomu na wanachama waamue.

Pili, nafasi mbalimbali za uongozi kamati kuu ya cdm hutapika majina lakini wanachama hawaulizwi sasa ni demokrasia ipi mwenzetu anaitafuta wakati nafasi hii ndogo Mwenyezi Mungu aliyompa kashindwa kuonyesha wasifu wake wa demokrasia?

Tatu, hivi mwenzetu ulijuaje Lowassa kaja na wafuasi wengi kama siyo hisia zako binafsi? Labda utuelimishe kabla Lowassa kujiunga na cdm mlikuwa na wanachama wangapi na baada ya kujiunga mkawa na wanachama wangapi. Kwa taarifa yako, kwa takwimu nilizonazo idadi ya wanachama haikuongezeka eti kwa sababu Lowassa alijiunga na cdm. Hizi takwimu hukuziongelea kwa sababu uliona zingelikuumbua.

Maandiko yako wazi kama huaminiki kwa madogo nani atakuamini kwa makubwa hata yawe ni yako?

CCM ina matatizo yake na ingepaswa kuwajibishwa lakini kwa uongozi huu dhaifu wa Mbowe ambao sanasana ni mkao wa kula ni kheri kabisa ccm wakaendelea kutesa hadi pale wanachama wa Chadema watakapofanya kweli na kumtimua huyu fisadi mkubwa na wakajipanga upya.

Vinginevyo mtabakia kulalama badala ya kujilaumu wenyewe.

N.B:-

Dola ina jukumu kubwa la kulinda ruzuku zinazopewa vyama vyote vya siasa na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa na hii siyo siasa ila ni utawala bora.
Ukitaka kujua mleta hoja ni CCM haihitaji kutumia nguvu kubwa.

Chadema Hakuna Mashininani, Chadema tuna Misingi.
 
Anayeiua Chadema ni Mbowe na ufisadi wake. Hela ya ruzuku anaitafuna kwa visingizio kebekebe. Utasikia alikopesha chama mabilioni wakati wa uchaguzi sasa anakidai chama mrejesho.

Swali ni vikao vipi viliidhinisha mikopo hiyo? Pili, mwenzetu ni benki? Tatu, hizo fedha alizitoa wapi kwa shughuli ipi? Nne, kwa matumizi yapi kwani sheria za uchaguzi zimeweka ukomo wa matumizi ya chaguzi.

Sasa kwa huu ufisadi Chadema imeshindwa kupeleka fedha mashinani na matokeo yake ukata umechangia baadhi ya madiwani kurubuniwa na ccm. CCM imegundua huu udhaifu wa Mbowe na wameugeuza kivuno.

Sasa wa kulaumiwa ni nani?

Pili, ujio wa Lowassa na kumkabidhi ugombea Urais aligeuza ni dili yake binafsi na kauli zake zinamtia hatiani. Alidai yeye ni nani amkatae Lowassa ambaye alikuja na wafuasi wengi.

Maswali yafuatayo hayana majibu..

Kwanza Mbowe wewe ni nani hadi uone suala la kugombea Urais ni lake binafsi? Kiongozi anayejiheshimu angesema tuwaulize wanachama kwa kura yao kupitia primaries ya mikutano ya wilaya nchi nzima waamue na kila anayetaka kugombea achukue fomu na wanachama waamue.

Pili, nafasi mbalimbali za uongozi kamati kuu ya cdm hutapika majina lakini wanachama hawaulizwi sasa ni demokrasia ipi mwenzetu anaitafuta wakati nafasi hii ndogo Mwenyezi Mungu aliyompa kashindwa kuonyesha wasifu wake wa demokrasia?

Tatu, hivi mwenzetu ulijuaje Lowassa kaja na wafuasi wengi kama siyo hisia zako binafsi? Labda utuelimishe kabla Lowassa kujiunga na cdm mlikuwa na wanachama wangapi na baada ya kujiunga mkawa na wanachama wangapi. Kwa taarifa yako, kwa takwimu nilizonazo idadi ya wanachama haikuongezeka eti kwa sababu Lowassa alijiunga na cdm. Hizi takwimu hukuziongelea kwa sababu uliona zingelikuumbua.

Maandiko yako wazi kama huaminiki kwa madogo nani atakuamini kwa makubwa hata yawe ni yako?

CCM ina matatizo yake na ingepaswa kuwajibishwa lakini kwa uongozi huu dhaifu wa Mbowe ambao sanasana ni mkao wa kula ni kheri kabisa ccm wakaendelea kutesa hadi pale wanachama wa Chadema watakapofanya kweli na kumtimua huyu fisadi mkubwa na wakajipanga upya.

Vinginevyo mtabakia kulalama badala ya kujilaumu wenyewe.

N.B:-

Dola ina jukumu kubwa la kulinda ruzuku zinazopewa vyama vyote vya siasa na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa na hii siyo siasa ila ni utawala bora.
Mbowe ni shujaa
 
Una kiwango cha chini sana cha uelewa au unatumika kipropaganda. Fedha zote za chama zinaidhinishwa kwa mfumo rasmi na pia zinakaguliwa kila mwaka na CAG na kutoa ripoti. Jee hayo unayosema ya matumizi mabaya umeyatoa kwenye ripoti ya CAG au katika vibaraza vya Lumumba?
Hizo story zenu mbona zimeshachacha?
Nani asiyejua kuwa kila mwaka CHADEMA imekuwa ikiambulia hati chafu kutoka kwa CAG?

Acha kujitoa ufahamu. Kuna tatizo kubwa sana la matumizi ya fedha za umma huko CHADEMA.

Sasa sijui mkiipata Hazina kuu itakuwaje
 
Anayeiua Chadema ni Mbowe na ufisadi wake. Hela ya ruzuku anaitafuna kwa visingizio kebekebe. Utasikia alikopesha chama mabilioni wakati wa uchaguzi sasa anakidai chama mrejesho.

Swali ni vikao vipi viliidhinisha mikopo hiyo? Pili, mwenzetu ni benki? Tatu, hizo fedha alizitoa wapi kwa shughuli ipi? Nne, kwa matumizi yapi kwani sheria za uchaguzi zimeweka ukomo wa matumizi ya chaguzi.

Sasa kwa huu ufisadi Chadema imeshindwa kupeleka fedha mashinani na matokeo yake ukata umechangia baadhi ya madiwani kurubuniwa na ccm. CCM imegundua huu udhaifu wa Mbowe na wameugeuza kivuno.

Sasa wa kulaumiwa ni nani?

Pili, ujio wa Lowassa na kumkabidhi ugombea Urais aligeuza ni dili yake binafsi na kauli zake zinamtia hatiani. Alidai yeye ni nani amkatae Lowassa ambaye alikuja na wafuasi wengi.

Maswali yafuatayo hayana majibu..

Kwanza Mbowe wewe ni nani hadi uone suala la kugombea Urais ni lake binafsi? Kiongozi anayejiheshimu angesema tuwaulize wanachama kwa kura yao kupitia primaries ya mikutano ya wilaya nchi nzima waamue na kila anayetaka kugombea achukue fomu na wanachama waamue.

Pili, nafasi mbalimbali za uongozi kamati kuu ya cdm hutapika majina lakini wanachama hawaulizwi sasa ni demokrasia ipi mwenzetu anaitafuta wakati nafasi hii ndogo Mwenyezi Mungu aliyompa kashindwa kuonyesha wasifu wake wa demokrasia?

Tatu, hivi mwenzetu ulijuaje Lowassa kaja na wafuasi wengi kama siyo hisia zako binafsi? Labda utuelimishe kabla Lowassa kujiunga na cdm mlikuwa na wanachama wangapi na baada ya kujiunga mkawa na wanachama wangapi. Kwa taarifa yako, kwa takwimu nilizonazo idadi ya wanachama haikuongezeka eti kwa sababu Lowassa alijiunga na cdm. Hizi takwimu hukuziongelea kwa sababu uliona zingelikuumbua.

Maandiko yako wazi kama huaminiki kwa madogo nani atakuamini kwa makubwa hata yawe ni yako?

CCM ina matatizo yake na ingepaswa kuwajibishwa lakini kwa uongozi huu dhaifu wa Mbowe ambao sanasana ni mkao wa kula ni kheri kabisa ccm wakaendelea kutesa hadi pale wanachama wa Chadema watakapofanya kweli na kumtimua huyu fisadi mkubwa na wakajipanga upya.

Vinginevyo mtabakia kulalama badala ya kujilaumu wenyewe.

N.B:-

Dola ina jukumu kubwa la kulinda ruzuku zinazopewa vyama vyote vya siasa na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa na hii siyo siasa ila ni utawala bora.


Mbona vyote ulivyotoa ni innuendoes bila data,dates,places,na wahusika?

Cha msingi ungetoa tarehe,wahusika,maeneo,etc?Real data,sio innuendos!
 
Mbowe alkuwa kiongoz mzur lkn tokea amkarbishe lowasa amekiharbia sifa Chama Sasa hv amepoteza mwelekeo
 
Anayeiua Chadema ni Mbowe na ufisadi wake. Hela ya ruzuku anaitafuna kwa visingizio kebekebe. Utasikia alikopesha chama mabilioni wakati wa uchaguzi sasa anakidai chama mrejesho.

Swali ni vikao vipi viliidhinisha mikopo hiyo? Pili, mwenzetu ni benki? Tatu, hizo fedha alizitoa wapi kwa shughuli ipi? Nne, kwa matumizi yapi kwani sheria za uchaguzi zimeweka ukomo wa matumizi ya chaguzi.

Sasa kwa huu ufisadi Chadema imeshindwa kupeleka fedha mashinani na matokeo yake ukata umechangia baadhi ya madiwani kurubuniwa na ccm. CCM imegundua huu udhaifu wa Mbowe na wameugeuza kivuno.

Sasa wa kulaumiwa ni nani?

Pili, ujio wa Lowassa na kumkabidhi ugombea Urais aligeuza ni dili yake binafsi na kauli zake zinamtia hatiani. Alidai yeye ni nani amkatae Lowassa ambaye alikuja na wafuasi wengi.

Maswali yafuatayo hayana majibu..

Kwanza Mbowe wewe ni nani hadi uone suala la kugombea Urais ni lake binafsi? Kiongozi anayejiheshimu angesema tuwaulize wanachama kwa kura yao kupitia primaries ya mikutano ya wilaya nchi nzima waamue na kila anayetaka kugombea achukue fomu na wanachama waamue.

Pili, nafasi mbalimbali za uongozi kamati kuu ya cdm hutapika majina lakini wanachama hawaulizwi sasa ni demokrasia ipi mwenzetu anaitafuta wakati nafasi hii ndogo Mwenyezi Mungu aliyompa kashindwa kuonyesha wasifu wake wa demokrasia?

Tatu, hivi mwenzetu ulijuaje Lowassa kaja na wafuasi wengi kama siyo hisia zako binafsi? Labda utuelimishe kabla Lowassa kujiunga na cdm mlikuwa na wanachama wangapi na baada ya kujiunga mkawa na wanachama wangapi. Kwa taarifa yako, kwa takwimu nilizonazo idadi ya wanachama haikuongezeka eti kwa sababu Lowassa alijiunga na cdm. Hizi takwimu hukuziongelea kwa sababu uliona zingelikuumbua.

Maandiko yako wazi kama huaminiki kwa madogo nani atakuamini kwa makubwa hata yawe ni yako?

CCM ina matatizo yake na ingepaswa kuwajibishwa lakini kwa uongozi huu dhaifu wa Mbowe ambao sanasana ni mkao wa kula ni kheri kabisa ccm wakaendelea kutesa hadi pale wanachama wa Chadema watakapofanya kweli na kumtimua huyu fisadi mkubwa na wakajipanga upya.

Vinginevyo mtabakia kulalama badala ya kujilaumu wenyewe.

N.B:-

Dola ina jukumu kubwa la kulinda ruzuku zinazopewa vyama vyote vya siasa na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa na hii siyo siasa ila ni utawala bora.
Ngoja wavuke mto ndio utawajua,unamsema mungu wao Mbowe ambaye hakosei,jitayarishe na mvua ya mitusi,kejeli na ujinga kibao.Tatizo Chadema hawapendi kuangalia mbaya wao waliyenae wao kila ubaya ni kutokana CCM ,na Mbowe ndivyo anavyotaka hivyo ili ale vizuri .Mwenyekiti gani anakuwa mwenyekiti wa maisha kwenye chama cha demokrasia ,si ajabu hata Babu Seya anashangaa kumkuta bado Mbowe ni mwenyekiti-Mbowe na Wenger wa Arsenal hawana tofauti
 
mbowe ni mfanyabiashara wa siasa,hilo halina ubishi
japo ni ukweli mchungu
Pia ni Mjasiriasiasa,kwa nchi za kiafrika mtu yeyote ambaye ni mfanyabiashara tapeli kuwa mwanasiasa na kumpa uongozi ni kutaka kukifilisi chama,hivi mnadhani Mbowe mjinga kuwa mwenyekiti wa maisha?ukitaka kumjua Mbowe gombea au tangaza nia ya kugombea uenyekiti Chadema,Chadema ni mali ya Mbowe na mwe wake mzee Mtei,wengine wote ni vibarua tu
 
Pia ni Mjasiriasiasa,kwa nchi za kiafrika mtu yeyote ambaye ni mfanyabiashara tapeli kuwa mwanasiasa na kumpa uongozi ni kutaka kukifilisi chama,hivi mnadhani Mbowe mjinga kuwa mwenyekiti wa maisha?ukitaka kumjua Mbowe gombea au tangaza nia ya kugombea uenyekiti Chadema,Chadema ni mali ya Mbowe na mwe wake mzee Mtei,wengine wote ni vibarua tu
Watu wanapokosa cha kusema huishia kuokoteza ili kupata bk7. Pole sana.
 
Back
Top Bottom