CHADEMA inafuata mkondo wa Muslim Brotherhood? Je watarudia makosa yao?

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Kwa watu wanaonijua vyema, nina karama na uwezo wa kusoma siasa za nchi fulani na kutabiri mabadiliko ambayo wengi wanakuwa bado hawajayaona. Haya si majisifu, nasema tu ukweli.

Nilifanya hivyo kwa Obama kabla hajawa maarufu sana, nilifanya hivyo kwa Uhuru Kenyatta wakati huo anashika nafasi za chini katika chaguzi kuu, nilifanya kwa Trump wakati wengine bado walikuwa wanamuona msindikizaji, nilifanya hivyo kwa Muslim Brotherhood kule Misri kabla hata vuguvugu la Arab Spring halijatokea na nilifanya hivyo kwa CHADEMA miaka mingi iliyopita.

Muslim Brotherhood ilikuwa ni taasisi isiyo rasmi iliyojijengea misingi katika kila sekta ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Ni movement iliyokuwa imejijenga katika mioyo ya wamisri kwa muda mrefu. Ni movement iliyounganisha watu waliokuwa wanadai haki na usawa katika jamii.

Hakuna sehemu ambapo MB hawakuwepo, hata katika majela kwa sababu huko viongozi na wafuasi wao wengi walikuwa wanafungwa.

Wakati sahihi ulipowajia, MB wakachukua nchi kupitia chama kilichokuwa chini ya mwamvuli wao kwa sababu kulikuwa hakuna mbadala aliyekuwa na nguvu zaidi yao.

Naiona CHADEMA wakifuata mkondo huo huo.

Baada ya kupigwa marufuku kufanya siasa kwa miaka mitano, ilienda underground na kufanya maandalizi ya kuhamasisha, kuelimisha na kuwaandaa watu kwa ajili ya mabadiliko katika ngazi za msingi kabisa. Matokeo yake ndiyo tunayaona katika uchaguzi huu wa 2020.

Uchaguzi huu ni ngazi muhimu sana kwa CHADEMA katika kujiimarisha zaidi katika kila kona na sekta ya nchi hii. Wasirudi nyuma!

Maeneo machache ya kuboresha ili wafikie lengo hilo:
  • Inabidi waende mbali zaidi na kujenga mahusiano na vyama vingine vya siasa ndani na nje ya Afrika.
  • Wajipenyeze zaidi katika vyombo vya dola hasa Polisi na JWTZ na watafute jinsi ya kuonyesha wanakubalika huko. Mfano, CHADEMA kitaaminika zaidi na kuwa na nguvu zaidi kama kitaanza kuwa na support ya wazi kutoka kwa wanajeshi wastaafu. Wawape hawa wastaafu nafasi chache katika chama na zile za kugombea mfano Ubunge.
  • Sura ya kitaifa. Chama kifanye juhudi za makusudi kutafuta na kuwapa nafasi mbalimbali za juu za uongozi wa chama watu wa makabila tofauti na pia kuwasogeza karibu Waislamu. Hili la Waislamu linawakwamisha sana CHADEMA na sijui kwa nini hawalifanyii kazi. ACT imechukua wafuasi wengi ambao kimsingi CHADEMA wangeweza kuwapata muda mrefu sana kama wangeweka nia ya dhati.
Kuna makosa machache ya msingi ambayo Muslim Brotherhood waliyafanya baada tu ya kuchukua uongozi wa nchi yaliyopelekea viongozi wake kufungwa, wafuasi wao wengi kuuawa na kufungwa na movement nzima kufutiliwa mbali.

Haya nitakuja kuyaeleza siku nyingine ila itoshe tu kusema CHADEMA baada ya ushindi wasibweteke hata kwa sekunde.

Kuna njia nyingi zinaweza kutumika kuwakwamisha na kuwachafua, inabidi waanze kuzitambua mapema mbinu hizi kabla hata ya kupewa madaraka.

Mwisho, baadhi ya mabadiliko wanayopanga kufanya itabidi wayacheleweshe kwa muda wasije wakawa wanajifunga wenyewe vitanzi.
 
Acha propaganda za kulipwa hela ndogo hizo. CCM ndio ma-Musilim Brotherhoods wa Tanzania. Mnawalipa msheikh (wa BAKWATA) eti kuombea amani. Waombee haki pia. Hakuna amani sehemu yenye wizi na uonevu.
 
Muslim brotherhood ilijengwa kwa misingi ya kidini, siasa ilifuata baadae, ndio maana ina matawi nchi nyingi za kiarabu, ni religious movement hakuna huusiano na chadema hata kidogo.
 
MB ilijijenga katika nafsi za Wamisri tangia 1929 wakati wa uhai wa muasisi wake Hassan El Banna. Baadae walipotaka kuingia kwenye serikali walianza kupata vikwazo vingi vya ndani na vya nje pia

Miaka ya Gamal Abdul Nassir wafuasi wa Ikhwan Muslimin(Muslim Brotherhood) walilengwa sana na kuandamwa na vyombo vya dola na pia wakawa maadui wa Israel na nchi za Magharibi na hata zile zenye mrengo wa Kijamaa

Chadema ni chama halali cha kisiasa kilichoruhusiwa kuendesha shughuli za kisiasa ikiwa ni pamoja na kuwania udhibiti wa dola kupitia sandukua la kura
 
Kwani Chadema wanapanga kufanya mabadiliko yapi ?
Wao wakiwa madarakani wale
Wawaachie wengine waje nao wale
Waje tena maccm wale
Hivo hivo kila kundi liwe linakula keki ya taifa.
 
Muslim brotherhood ilijengwa kwa misingi ya kidini, siasa ilifuata baadae, ndio maana ina matawi nchi nyingi za kiarabu, ni religious movement hakuna huusiano na chadema hata kidogo.
Dini kwao ni chaka la kujifichia
Hakuna Dini kwao...bali tamaa ya madaraka
 
This is JF we would wish to be. Very good critical analysis . Tofauti ya MB wao wanaongozwa na imani ya kiislamu. Lakini mengine yote ni sahihi . Chadema lazima iee na diversity ya makabila yote haswa kwenye uongozi. Lazima iweke misingi imara ya Social media baada ya kuwa na mainstream media kushindikana kutokana na sheria kandamizi.

Lazima wawahusishe watanzania waliopo jela ikiwezekana wawekeze kwenye wanasheria kutetea watu waliopo jela kuna mamia ya watanzania wapo ndani kwa makosa ya kiufundi na kushindwa kutetewa ipasavyo huko ndiko habari za chadema zitasambaa zaidi
 
Kuihusisha Chadema na kundi la Muslim Brotherhood utakuwa unakosea, wale jamaa walisimama zaidi kwa kutumia uungwaji mkono wa kidini tena kwa wale waislam wenye msimamo mkali.

Nakumbuka mmoja wa watu maarufu aliejiunga na kukifadhili chama hicho alikuwa mchezaji mahiri wa Al- Ahly ya Misri; Mohammed Aboutreika, japo baadae mali zake zilikuja kuwa confiscated kwasababu ya ufadhili wake na akafungwa gerezani.

Kwa upande wa Chadema hiki ni chama cha siasa, ambacho kinatakiwa kuwa na uungwaji mkono wa makundi yote ya kijamii bila kujali rangi, kabila, wala dini zao. Hivyo huwezi kuihusisha Chadema na MB kwasababu Chadema kufanana na MB watakuwa wanavunja sheria za kuundwa kwa chama cha siasa nchini.

Japo nakubaliana na wewe unapotaka Chadema itafute uungwaji mkono wa watu kutoka TISS na jeshini, na wapewe nafasi za kugombea kama ubunge. Hili litasaidia sana kuzuia mipango haramu ya kuchakachua kura hasa wakati wa kuhesabu na majumuisho mpaka mshindi anapotangazwa, wanahitajika watu wanaojua mbinu haramu za CCM.

Hili likiwezekana itakuwa safi sana, ila natilia shaka "guts" za hao watakaokuwa tayari kufanya hivyo, ni lazima wawe tayari ku-sacrifice pensheni zao kwasababu sidhani kama hii serikali ya CCM itawaacha salama, lazima watasumbuliwa kwa namna tofauti.
 
This is JF we would wish to be. Very good critical analysis . Tofauti ya MB wao wanaongozwa na imani ya kiislamu. Lakini mengine yote ni sahihi . Chadema lazima iee na diversity ya makabila yote haswa kwenye uongozi. Lazima iweke misingi imara ya Social media baada ya kuwa na mainstream media kushindikana kutokana na sheria kandamizi.

Lazima wawahusishe watanzania waliopo jela ikiwezekana wawekeze kwenye wanasheria kutetea watu waliopo jela kuna mamia ya watanzania wapo ndani kwa makosa ya kiufundi na kushindwa kutetewa ipasavyo huko ndiko habari za chadema zitasambaa zaidi


Watawekeza nini wakati pesa yote inaibiwa kijanja.
 
Abuu Jaahil Bro
Ni yule anaeyageuza maandiko kwa matamanio ya nafsi zao
Hebu kua kama Abuu Dharr usijitoe akili ukawa Abuu jahal.
Tatizo lenu nyinyi mnajiona bora na wachamungu zaidi kuliko watu wote.
Acheni kuzitukuza nafsi zenu.
 
This is JF we would wish to be. Very good critical analysis . Tofauti ya MB wao wanaongozwa na imani ya kiislamu. Lakini mengine yote ni sahihi . Chadema lazima iee na diversity ya makabila yote haswa kwenye uongozi. Lazima iweke misingi imara ya Social media baada ya kuwa na mainstream media kushindikana kutokana na sheria kandamizi.

Lazima wawahusishe watanzania waliopo jela ikiwezekana wawekeze kwenye wanasheria kutetea watu waliopo jela kuna mamia ya watanzania wapo ndani kwa makosa ya kiufundi na kushindwa kutetewa ipasavyo huko ndiko habari za chadema zitasambaa zaidi

Siasa za sasa na zijazo za Tanzania zinaenda kuzalisha movement inayoenda chini kwa chini ya mlengo wa siasa kali ambayo in the long run itakuwa linked na CHADEMA. Kama nilivyojaribu kuelezea hapa.

CHADEMA au chama chochote kingine cha siasa hakitaweza kuhimili (survive) kufanya siasa nchini kwa sasa bila kuradicalize siasa zao.
 
Siasa za sasa na zijazo za Tanzania zinaenda kuzalisha movement inayoenda chini kwa chini ya mlengo wa siasa kali ambayo in the long run itakuwa linked na CHADEMA. Kama nilivyojaribu kuelezea hapa.

CHADEMA au chama chochote kingine cha siasa hakitaweza kuhimili (survive) kufanya siasa nchini kwa sasa bila kuradicalize siasa zao.
Uliona mbali
 
Kwa watu wanaonijua vyema, nina karama na uwezo wa kusoma siasa za nchi fulani na kutabiri mabadiliko ambayo wengi wanakuwa bado hawajayaona. Haya si majisifu, nasema tu ukweli.

Nilifanya hivyo kwa Obama kabla hajawa maarufu sana, nilifanya hivyo kwa Uhuru Kenyatta wakati huo anashika nafasi za chini katika chaguzi kuu, nilifanya kwa Trump wakati wengine bado walikuwa wanamuona msindikizaji, nilifanya hivyo kwa Muslim Brotherhood kule Misri kabla hata vuguvugu la Arab Spring halijatokea na nilifanya hivyo kwa CHADEMA miaka mingi iliyopita.

Muslim Brotherhood ilikuwa ni taasisi isiyo rasmi iliyojijengea misingi katika kila sekta ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Ni movement iliyokuwa imejijenga katika mioyo ya wamisri kwa muda mrefu. Ni movement iliyounganisha watu waliokuwa wanadai haki na usawa katika jamii.

Hakuna sehemu ambapo MB hawakuwepo, hata katika majela kwa sababu huko viongozi na wafuasi wao wengi walikuwa wanafungwa.

Wakati sahihi ulipowajia, MB wakachukua nchi kupitia chama kilichokuwa chini ya mwamvuli wao kwa sababu kulikuwa hakuna mbadala aliyekuwa na nguvu zaidi yao.

Naiona CHADEMA wakifuata mkondo huo huo.

Baada ya kupigwa marufuku kufanya siasa kwa miaka mitano, ilienda underground na kufanya maandalizi ya kuhamasisha, kuelimisha na kuwaandaa watu kwa ajili ya mabadiliko katika ngazi za msingi kabisa. Matokeo yake ndiyo tunayaona katika uchaguzi huu wa 2020.

Uchaguzi huu ni ngazi muhimu sana kwa CHADEMA katika kujiimarisha zaidi katika kila kona na sekta ya nchi hii. Wasirudi nyuma!

Maeneo machache ya kuboresha ili wafikie lengo hilo:
  • Inabidi waende mbali zaidi na kujenga mahusiano na vyama vingine vya siasa ndani na nje ya Afrika.
  • Wajipenyeze zaidi katika vyombo vya dola hasa Polisi na JWTZ na watafute jinsi ya kuonyesha wanakubalika huko. Mfano, CHADEMA kitaaminika zaidi na kuwa na nguvu zaidi kama kitaanza kuwa na support ya wazi kutoka kwa wanajeshi wastaafu. Wawape hawa wastaafu nafasi chache katika chama na zile za kugombea mfano Ubunge.
  • Sura ya kitaifa. Chama kifanye juhudi za makusudi kutafuta na kuwapa nafasi mbalimbali za juu za uongozi wa chama watu wa makabila tofauti na pia kuwasogeza karibu Waislamu. Hili la Waislamu linawakwamisha sana CHADEMA na sijui kwa nini hawalifanyii kazi. ACT imechukua wafuasi wengi ambao kimsingi CHADEMA wangeweza kuwapata muda mrefu sana kama wangeweka nia ya dhati.
Kuna makosa machache ya msingi ambayo Muslim Brotherhood waliyafanya baada tu ya kuchukua uongozi wa nchi yaliyopelekea viongozi wake kufungwa, wafuasi wao wengi kuuawa na kufungwa na movement nzima kufutiliwa mbali.

Haya nitakuja kuyaeleza siku nyingine ila itoshe tu kusema CHADEMA baada ya ushindi wasibweteke hata kwa sekunde.

Kuna njia nyingi zinaweza kutumika kuwakwamisha na kuwachafua, inabidi waanze kuzitambua mapema mbinu hizi kabla hata ya kupewa madaraka.

Mwisho, baadhi ya mabadiliko wanayopanga kufanya itabidi wayacheleweshe kwa muda wasije wakawa wanajifunga wenyewe vitanzi.

Hivyo unathibitisha rais wetu ni dikteta kam wa Misri
 
Back
Top Bottom