Habari na udaku mwingi hapa ni ama Chadema au viongozi wa Chadema. Au zinahusu serikali lakini zimeibuliwa na wanachadema. Kama Chadema ikifutwa habari na udaku Hapa JF zitapungua kwa takriban nusu nzima. Habari zitakazobakia zitakuwa hazina mvuto hivyo wanajamvi watadoda. Na magazeti watauza nini?
Kwani vyama vingine vya siasa vimetokomea wapi? Hata ccm pia haipo tena kwenye screen!
Chadema ni chama tawala kwa sasa; habari zake ndizo zinauza story pole kwao mtanzania na vigazeti uchwara ambavyo hata mishahara inapatikana kwa bail out maana hawana biasahara tena
Kama ni mtu wa kufikiria huwezi kukitenga Chadema katika mijadala mbalimbali nchini Tz kwakuwa ndio chama pekee kilichoonesha kuwa na muelekeo. Na swali lako kama kitafutwa ni ndoto hizo. hata hivyo ukae ukijua kuwa mwanadamu na maisha hivyo kila kitu kinabadilika leo hatuwezi kuongelea Kampeni wakati watu tupo kwenye katiba na mambo mengine! Hivyo kila jambo na wakati wake!
Jamani hii mada haijasema Chadema itafutwa, hebu someni hicho kiswahi vizuri. Hii mada inakisifu chadama, hivyo kama ina kasoro ni hiyo ya kuwa biased toward Chadema.
Tanzania itakuwepo tu,mijadala itakuwepo hata bila ya cdm au ccm hata kile cha mnymwz na wpmb! So please don't dig your head deep into the sand to that extent!