Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,162
Ikiwa imebaki wiki moja kamili hadi kufikia ile tarehe 17 ya mwezi huu uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo la Kinondoni na Siha kufanyika, ni lazima chama cha upinzani cha Chadema kiwe makini sana na mbinu zinazoweza kufanywa na CCM katika kutaka "kuwapora" ushindi wao unaoelekea wa dhahiri wa ubunge katika majimbo hayo mawili.
Maeneo ambayo CCM wanaweza yawekea mikakati ya kuweka figisu figisu ni haya yafuatayo.
1. Mawakala wa Chama cha Chadema ni lazima wahakikiwe mapema na kuhakikishwa kuwa ni "wafia chama" na majina yao kupelekwa mapema ili zisiwepo bila za kutaka kuwaemgua.
2. Chadema ihakikishe kuwa vituo vya kupigia kura haviwi "siri" ya Tume ya uchaguzi, ili viwe na uwazi ili kuepusha wapiga kura mamluki kutoka maeneo mengine nje ya Kinondoni na Siha
3. Katika siku hizi za mwisho za kampeni timu ya kampeni ya Chadema ijikite katika kuelezea itawafanyia nini wakazi wa Kinondoni iwapo itaaminiwa na wakazi hao kwa kupewa kura na ijiepushe na lugha za "vijembe" kwa wapinzani wake, kwa kuwa tunafahamu kuwa Jeshi la Polisi liko upande wa CCM na ndiyo maana limeamua kuirekodi mikutano yote ya kampeni wanayoifanya Chadema, ili wapate sababu za "kumdesqualify' mgombea wa Chadema katika kipindi hiki cha lala salama
Mkishakiwa makini na hayo niliyowatip, basi ni dhahiri ushindi ni wenu na wao CCM ambao ni mabingwa wa kuwanunua wapinzani, mchezo huo utafikia MWISHO na hawatarudia tena kuwanunua wapinzani.
Maeneo ambayo CCM wanaweza yawekea mikakati ya kuweka figisu figisu ni haya yafuatayo.
1. Mawakala wa Chama cha Chadema ni lazima wahakikiwe mapema na kuhakikishwa kuwa ni "wafia chama" na majina yao kupelekwa mapema ili zisiwepo bila za kutaka kuwaemgua.
2. Chadema ihakikishe kuwa vituo vya kupigia kura haviwi "siri" ya Tume ya uchaguzi, ili viwe na uwazi ili kuepusha wapiga kura mamluki kutoka maeneo mengine nje ya Kinondoni na Siha
3. Katika siku hizi za mwisho za kampeni timu ya kampeni ya Chadema ijikite katika kuelezea itawafanyia nini wakazi wa Kinondoni iwapo itaaminiwa na wakazi hao kwa kupewa kura na ijiepushe na lugha za "vijembe" kwa wapinzani wake, kwa kuwa tunafahamu kuwa Jeshi la Polisi liko upande wa CCM na ndiyo maana limeamua kuirekodi mikutano yote ya kampeni wanayoifanya Chadema, ili wapate sababu za "kumdesqualify' mgombea wa Chadema katika kipindi hiki cha lala salama
Mkishakiwa makini na hayo niliyowatip, basi ni dhahiri ushindi ni wenu na wao CCM ambao ni mabingwa wa kuwanunua wapinzani, mchezo huo utafikia MWISHO na hawatarudia tena kuwanunua wapinzani.